Adverts

May 3, 2009

MBEYA PRESS YAPATA VIONGOZI WAPYA

Mwandishi wa TBC bwana NICO MWAIBALE jana aliibuka kwa ushindi wa kimbunga kuwa mwenyekiti wa chama cha wandishi wa habari mkoa wa mbeya. Katika uchaguzi huo ambao haukupata uwakilishi kutoka Umoja wa Vyama vya wandishi wa habari mikoani UTPC, ulifanyika kwa amani katika ukumbi wa chuo cha wafanyakazi Mbeya. Mwaibale ambaye katika nafasi ya uenyekiti alikuwa akishindana na mwenyekiti aliyemaliza muda wake bwana Christopher Nyenyembe, aliibuka na kura 26 dhidi ya 10 za Nyenyembe. Makamu mwenyekiti alichaguliwa Jane Lawa ambaye hata hivyo hakuhudhulia kwenye uchaguzi huo kwa kulamba kura 20 dhidi ya 15 za Richard Kilumbo. Katibu mkuu alichaguliwa Patrick Kossima (27) na kumshinda Kenneth Mwazembe (9), Katibu msaidizi alichaguliwa Merali Chawe kwa kura 31 za Ndiyo kati ya 36 zilizopigwa.(chawe hakuwa na mpinzani). Mweka hazina alichaguliwa Pendo Fundisha aliyepata kura 31 za Ndiyo na kura 3 za hapana baada ya kukosa mshinani, wajumbe wa kamati kuu walichaguliwa Danny Tweve aliyepita bila kupingwa baada ya kuwania nafasi hiyo peke yake. Wajumbe wengine katika kamati hiyo waliochaguliwa kwa kushindanishwa ni pamoja na Ester Macha, Sada Matiku. Kamati zingine waliochaguliwa ni Charles Mwakipesile(Nidhamu), Festo Sikagonamo (Mafunzo na Ujenzi) na Emanuel Simfukwe (Uchumi). Kwa uchaguzi huo Chama cha wandishi wa habari mkoa wa Mbeya kimetimiza masharti na maelekezo mapya ya UTPC kwa kila klabu kuwa na uwakilishi sawa kijinsia katika nafasi zote za maamuzi. Tunamshukuru bwana Christopher Nyenyembe kwa Uongozi wake kwa kipindi cha miaka 3 iliyopita ambapo ameiwezesha klabu kupata heshima ndani ya nchi kutokana na wanachama wake watatu akiwemo yeye mwenyewe kutwaa tuzo za uandishi bora wa habari za uchunguzi kwa miaka miwili.MBEYA PRESS CLUB >>> PEOPLE’S VOICE