Adverts

May 3, 2009

WANDISHI MBEYA WASIKITISHWA NA VIFO VYA WENZAO

Mkutano mkuu wa Chama cha wandishi wa habari mkoani Mbeya, umepokea kwa masikitiko taarifa ya vifo vya wanachama wake 6 katika kipindi cha miaka 3 iliyopita. Kifo cha hivi karibuni ni cha Mhariri Mkuu wa Radio Uhuru Deogratius Kiduduye aliyefariki Lagos Nchini Nigeria alikoenda kwaajili ya maombi katika Kanisa la Synagogue church of All Nation linaloongozwa na Nabii Tb Joshua. Deo alikuwa mwanachama wa chama hicho hadi alipohamia jijini Dar es salaam kuchukua majukumu ya uhariri katika kituo cha Radio Uhuru, ambapo katika kipindi chote cha uhai wake amekuwa akitoa ushauri namna ya kuiendeleza klabu hiyo. Wanachama wengine waliofariki dunia ni pamoja na Niko Mwakatumbula, John Lubungo, Silvester Kikungwe, Rose Nkuba, Albano Wikedzi, Erasto Palick na Mariam Ngole ambao kwa pamoja wamefariki katika vipindi tofauti vya miaka mitatu ya uongozi uliomaliza muda wake hapo jana. Wanachama waliozungumza na blog hii wamesema katika jumuiya ya wanachama 60 kupotelewa na wanachama wake 8 ni jambo la kusikitisha na kumwomba mungu awatunze na kuwafikisha mahala salama marehemu wote hao. AMEN