Adverts

Nov 30, 2010

HAYA YOTE YAPO DUNIANI: MTOTO ALIYEZALIWA UBONGO NJE

 Hivi ndivyo kichwa cha mtoto kinavyoonekana
Matroni wa wodi ya kina mama bi. Haule akimhudumia mtoto na aliyembeba ni Bi Sabina Lyombo mama wa mtoto





Na Sekela Mwasubila, Ulanga


Mtoto mmoja katika hospitali ya Wilayani Ulanga mkoani Morogoro amezaliwa ubongo ukiwa nje baada ya kukosa ngozi ya kichwa huku akiwa mwenye afya njema.



Akiongea na mwandishi Kaimu Mganga Mkuu (W) Dkt Amani Kombe amesema kuwa tukio hilo lilitokea siku ya jumatatu majira ya saa tatu usiku baada ya mama wa mtoto kujifungua mtoto huyo wa kiume hospitali hapo.



Aliongeza kuwa hali ya mtoto kuzaliwa na kukosa ngozi ya kichwa hutokea wakati wa uumbaji wa viungo mbalimbali vya mwili wa mtoto na hali hiyo huweza kusababishwa na ukosefu wa madini mbalimbali kwa mama wakati wa ujauzito aidha ni tukio la kwanza kutokea katika hospitali hiyo ya wilaya.





Naye mama wa mtoto bi. Silvia Lyombo (20) ambaye ni ujauzito wake wa kwanza alisema kuwa hakupata matatizo yoyote ya kiafya wakati wa ujauzito na alijifungua katika hali ya kawaida mtoto mwenye uzito wa kilo 2.9 na kuwa ananyonya kama kawaida na hana tatizo lolote zaidi ya kukosekana kwa ngozi ya kichwa aidha hakuna dawa zozote ambazo alizitumia katika kipindi chote cha ujauzito wake.



Hata hivyo wataalamu wa hospitali ya wilaya walisema kuwa watampeleka mtoto huyo katika hospitali kubwa mkoani Morogoro kwa uchunguzi zaidi wa nini kifanyike kukabiliana na tatizo la mtoto huyo ambaye hadi sasa yupo hai na afya njema.



indaba2010

PINGAMIZI LA UBUNGE IRINGA MJINI LATINGA MAHAKAMANI


Katibu wa mheshimiwa Monica Mbega bwana Charles Charles akizungumzia pingamizi lililowekwa dhidi ya Mchungaji Msigwa(picha kwa hisani ya francis godwin blog)

MBUNGE wa zamani wa jimbo la Iringa mjini na mkuu wa mkoa wa KIlimanjaro ambaye alikuwa mgombea ubunge jimbo la Iringa mjini kupitia chama cha Mapinduzi (CCM) Monica Mbega amefungua kesi namba 3 ya mwaka 2010 katika mahakama kuu kanda ya Iringa akipinga matokeo yaliyompa ushindi mgombea mbunge wa chama cha Demokrasia na maendeleo (chadema) mchungaji Peter Msigwa.




Katibu wa CCM wilaya ya Iringa mjini Charles Charles alithibitisha mbele ya waandishi wa habari leo ofisini kwake kuhusiana na Mbega kwenda mahakamani kupinga ushindi wa mchungaji Msigwa wa Chadema kwamadai ya kuwepo kwa kasoro zaidi ya 10 zilizopata kujitokeza siku ya uchagua mkuu octoba 31 ikiwemo ya vituo vya kupigia kura kuhamishwa dakika za mwisho na kufanya baadhi ya wapiga kura kutopiga kura.



Kasoro nyingine ni ile ya tofauti ya matoke yaliyotangazwa na msimamizi wa uchaguzi jimbo la Iringa mjini ambayo kwa mujibu wa Mbega kuwa yalionyesha kutofautiana kwa kura kama 800 na sehemu ila matokeo ya pili yaliyotangzwa bila kuwepo kwa wakala wala mgombea wa CCM yanaonyesha mgombea huyo wa CCM alipitwa kwa kura zaidi ya 2000 na mgombea wa Chadema.



Hivyo alisema kuwa kutokana na kasoro hizo na nyingine nyingi mgombea huyo wa CCM Mbega amelazimika kwenda mahakamani kupinga matokeo hayo ya uchaguzi mkuu .



Charles alisema kuwa matokeo ya kwanza ya ubunge yaliyotangazwa na msimamizi wa uchaguzi yalionyesha mgombea wa NCCR-mageuzi Mariam Mwakingwe alikuwa amepata kura 950 na Monica Mbega (CCM) alikuwa amepata kura 16,916 huku mchungaji Msigwa akipata kura 17742 na kuwa matokeo hayo yalitangazwa huku mawakala wa CCM wakiwepo na kupokea hivyo.



Japo baadaye msimamizi wa uchaguzi alitangaza matokeo mapya ambayo mgombea wa CCM wala wakala wake hakuwepo ambapo matokeo hayo Msigwa yalimpa ushindi mkubwa Msigwa kwa kupata kura 17,352 wakati Mgombea waNCCR Mageuzi Mwakingwe akipata kura 1292 .



Hivyo alisema kuwa ukitazama matokeo hayo unapata picha halisi ni jinsi gani ambavyo msimamizi wa uchaguzi alivyoshindwa kutoa matokeo sahihi ya jimbo hilo na kuwa hadi sasa mgombea wa CCM hajapata nakala ya matokeo hayo mapya ambayo ndiyo yamempeleka Msigwa bungeni.



Pia alisema kuwa kasoro nyingine ni ile ya idadi ya wapiga kura katika baadhi ya vituo kuonekana kubwa zaidi ya wale waliojiandikisha na sehemu nyingi idadi ya waliopiga kura na wasio piga kura ukijumlisha unakuta kuna tofauti kubwa ya kura kuzidi.



Hata hivyo alishindwa kutaja wakili anayesimamia kesi hiyo kwa madai kuwa atajulikana pindi kesi hiyo itakapoanzwa kusikilizwa pamoja na kujua idadi ya halisi ya kasoro zilizotolewa na Mbega ambaye hakuweza kupatikana kuelezea suala hilo.



Kwa upande wake Mchungaji Msigwa alipoulizwa kuhusiana na madai hayo ya Mbega kwenda Mahakamani kupinga ushindi wake alisema kuwa hata yeye amekuwa akisikia kuwepo kwa suala hilo japo hadi jana alikuwa hajapatakufikishiwa taarifa yoyote rasmi toka mahakamani juu ya kuwepo kwa kesi hiyo.



"Mimi mwenyewe nimekuwa nikisikia kama Mbega amekwenda mahakamani kupinga ushindi wangu ila mimi sijapata taarifa rasmi za kuitwa mahakamani japo ni haki yake ya msingi kwenda mahakamani"alisema Mbunge Msigwa alipoulizwa kwa njia ya simu na mwandishi wa habari hizi.



indaba2010

MH MBEGA APELEKA PINGAMIZI MAHAKAMANI KUPINGA USHINDI WA MCHUNGAJI MSIGWA

Taarifa kutoka mtandao wa mdau Francis Godwin unaonyesha kuwa Mh Mama Monica Mbega Mahuvi amefikisha mahakamani pingamizi lake lakutaka matokeo ya uchaguzi wa nafasi ya ubunge kwa jimbo la Iringa mjini yatenguliwe na mahakama kuu

MH Rais anapowafunda mawaziri wake

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikutana kwa mara ya kwanza na baraza lake jipya la mawaziri ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi(picha na Freddy Maro)


Spika makinda ziarani namibia

Mhe. Anne Makinda (Mb)Spika wa Bunge na Makamu Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Jukwaa la mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika, SADC-PF (kulia) akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu wa Jukwaa hilo Mhe. Essau Chiviya , wakati wa kikao cha Kamati Tendaji mjini Swakompmund, Namibia tarehe 29/12/2010 baada ya kupitia agenda na maandalizi ya Mkutano wa 28 wa SADC-PF utakaofunguliwa na Rais wa Namibia Mhe, Hifikepunye Pohamba tarehe

CHILIGATI ANAPOMKABIDHI TIBAIJUKA ILANI

Mh. Chiligati akikabidhi Ilani ya CCM kwa Mh. Tibaijuka ili kutekeleza kwa ukamilifu ahadi za chama hicho kwenye sekta ya Ardhiindaba2010

MASHINDANO YA KUKIMBIZA BAISKELI DODOMA

indaba2010

Makamu wa Rais akutana na Mawaziri wa ofisi yake leo

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Mohamed Gharib Bilal katikati, akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri wa Ofisi yake wakati Mawaziri hao walipokwenda Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es salaam leo, kwa ajali ya kujitambulisha rasmi. kushoto Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mhe. Dk. Teresya Luoga Hovisa, katikati Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Mhe. Samia Hassan Suluhu.indaba2010

ILO; bongo Tunaathiriwa na nchi zinazozotuzunguka zenye maambukizi makubwa ya UKIMWI

Na Danny Tweve


Iringa.



Shirika la kazi duniani tawi la Tanzania limetaja Tanzania kuwa katika hatari zaidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI kutokana na kupitiwa na barabara kutoka nchi zenye kiwango cha juu cha maambukizi.



Akizungumza kwenye mafunzo ya waelimisharika wa masuala ya mapambano dhidi ya UKIMWI katika maeneo ya Kazi,



Mratibu wa Mradi wa Kuongeza Uwezo wa kiuchumi na Kupunguza hatari ya Maambukizi kwenye Njia za Usafirishaji kwa chini ya ILO upande wa Tanzania Bi Tulanoga Matimbwi ameeleza hayo jana mjini Iringa wakati akielezea mwelekeo wa mradi huo.

Amesema wakati Tanzania kwa upande wake kiwango cha maambukizi ni 5.7% nchi zinazolisha(feed) barabara kuu ya TANZAM zina maambukizi makubwa hii ikienda sambamba na barabara ya Dar es Salaam hadi Namanga.



Alitolea mfano kuwa nchi zilizo kwenye ukanda wa barabara ya TANZAM hali ya maambukizi ni kubwa kuanzia Zambia ambako kiwango cha maambukizi ni 15.03%,Malawi 14.02%,Zimbabwe 24%,Afrika Kusini 18% Botswana 23.9% na Msumbiji 12%.



Kutokana na hali hiyo amesema ni muhimu kuimarisha jitihada za kukabiliana na maambukizi mapya kwenye vituo vinavyopitiwa na barabara hizo kuu, ili kupunguza madhara ya mwingiliano huo.



Ameainisha kuwa uelimishaji katika mipango yake unalenga zaidi kwenye maeneo ya kazzi katika sekta binafsi na sekta ya umma na kwamba kupitia miundo iliyopo katika ngazi za wilaya itawezesha kufanikisha mapambano hayo.



Mafunzo hayo yanahusisha washiriki kutoka Mikoa ya Mbeya, Iringa, Dar es Salaam na NJORUMA na wengi wao ni kutoka asasi zinazojengea uwezo vikundi vya kijamii, waratibu wa UKIMWI na maafisa ushirika.

Baada ya dozi hii nawatakia kilalakheri katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe mosi Decemba, Mungu awabairi na kuwajaza nguvu wale wote wanaopata huduma majumbani na wanaopata dawa katika maeneo mbalimbali nchini mwetu na duniani kote. Mchango wenu katika maendeleo ya nchi bado tunautegemea msikate tamaa tupo pamoja nanyi katika kuhakikisha kuwa afya zenu zinaendelea kuimarika kwa kuimarisha huduma za tiba majumbani lakini pia katika kliniki za CTC. ahsante
indaba2010

LUKUVI AKIWA KWENYE OFISI YAKE

Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Fanuel Mbonde akiwatambulisha Mawaziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Mary Nagu (Mb) anayeshughulikia (Uwekezaji na Uwezeshaji) na Mhe. William Lukuvi (Mb) anayeshughulikia (Sera Uratibu na Bunge) kwa Wakuu wa Idara, Vitengo na Taasisi zilizoko chini ya Ofisi hiyo (hawako pichani), tarehe 29 Novemba, 2010 wakati Mawaziri hao waliporipoti Ofisi ya Waziri Mkuu kuanza kazi rasmi baada ya kuapishwa.

MAWAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU WATETA NA WATENDAJI WAO

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge) Mhe. William Lukuvi (Mb), akisalimiana na Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Bibi Fatma Mrisho wakati wa mapokezi ya Waziri huyo katika viwanja ya Ofisi ya Waziri Mkuu alipowasili kuanza kazi yake rasmi tarehe 29 Novemba 2010. Nyuma ya Waziri ni Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Fanuel Mbonde.

Nov 28, 2010

Niombe radhi wadau mtandao ulicrash kidogo

Ndugu wadau sikuwa hewani kwa muda wa wiki tatu kutokana na kuathiriwa na teknolojia kwani kila nikiingiza password ilikuwa inanikatalia sijui kuna fundi alinifanyia maufndi yake. nimerejea baada ya kutafuta waganga wa fani hiyo
thanks for being patient
indaba2010

KAMPUNI YA UNYIHA YATOA MSAADA WABATI 100 KUJENGA MABWENI

Mkurugenzi wa Unyiha Associate bwana Charles Chenza akikabidhi hundi yenye thamani ya milioni za kutosha bati 100 kwaajili ya ujenzi wa hosteli katika shule za sekondari wilayanI Mbozi katika mkoa wa Mbeya ambako ndiko alikowekeza. Msaada huo ulipokelewa na  kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi bwana Lington Ngaikwela
i ndaba2010

TEKNOLOJIA YA UJENZI WA LAMI KWA KUTUMIA NGUVU KAZI HII HAPA

Shirika la maendeleo la JAPAN limetambulisha teknolojia mpya ya ujenzi wa lami kwa kutumia nguvu kazi ambapo majaribio yake yanafanywa katika mkoa wa Mbeya.

zifuatazo hapa ni shemeu  ya picha za utekelezaji wa majaribio ya mradi huo unaosimamiwa na kampuni ya Eight Japaniese Engineering Company EJEC

 PICHA ZOTE KWA HISANI YA EJEC/JICA

NAUZA GARI KITU CHA KISASA

 NAUZA GARI HILO US$15,000 WASILIANA KWA NAMBA YANGU KULIA KWENYE BLOG HII
 INATUMIA DIESEL CC 2900 KILOMETA 77,000 IMESHALIPIWA NI KUONDOKA NAYO TU

indaba2010

Nov 18, 2010

UNGA WA BILION 1 MILION 322 WADAKWA BODA YA TUNDUMA

Na Danny Tweve
Mbozi

Watu wawili raia wa Afrika Kusini walikamatwa jana wakiwa na shehena ya madawa ya kulevya yenye thamani ya dola za Kimerekani 822,000 sawa na pesa za madafu za kibongo Bilion 1 Milion 322  wakiwa kwenye mchakato wa kuzivusha kutoka bongo kuelekea Bondeni kwa Mandela.


Akielezea tukio hilo Meneja wa Mamlaka ya Mapato mkoa wa Mbeya Rogasian Shirima alisema kuwa walipata dokezo toka kwa raia wema kuhusu kuvushwa kwa madawa hayo na ndipo walipoongeza umakini katika ukaguzi mpakani na kufanikiwa kukamata madawa hayo.

Shirima alimtaja dreva wa gari aina ya Nissan Hardy Board pick up lenye namba za usajili CA 508-650 kuwa ni Vuyo Jack (29) akiwa na mwanamke mwenye asili ya Asia Anastacia Cloete (25) kuwa walibeba jumla ya kilo 42.5 za madawa ya kulevya wakitokea Dar es Salaam na kuelekea Cape town nchini Afrika ya Kusini.

Katika zoezi la upimaji mzigo huo ilibainika kuwepo kwa Cocaine paketi 26 zenye uzito wa kilo 28.5, Heroin paketi 3 za uzito wa kilo 3.5 na Morphine paketi 8 za uzito wa kilo 10.75.

Makasha ya dawa  hizo  zilipofunguliwa  zilikuwa na mihuri ya Pakistan na nembo au chata za Ng’e na nyoka aina ya Cobra ambapo polisi wa kitengo maalum hapo mpakani walipima na kuthibitisha dawa hizo . (chemical identification)

 Aidha alama za nyoka na ng’e zimefahamika kuwa ni moja ya vitambulisho vinavyotumiwa na maharamia wa dawa za kulevya kutambulisha dawa aina ya Cocaine na Heroine.

Dereva wa gari hilo Vuyo Jack alipohojiwa juu ya yeye kupakia mzigo huo alidai kuwa yeye aliingia hapa nchini na kwenda Mazimbu Morogoro kwenye kambi ya wakimbizi ambapo alikutana na kundi la watu saba akiwepo mtanzania mwenye asili ya kiasia ambao walimkodi awasafirishie almasi hadi Cape town kwa ahadi ya kumlipa dola za kimarekani 10,000.

“Walidai niwape gari ili wakapakie almasi hizo ambapo walichukua gari hilo wakiniacha Morogoro na kwenda nalo Dar es Salaam ambako walipakia mzigo huo, baada ya wiki moja walinipigia simu kwamba wananiletea gari nianze safari ambapo waliniambia kuwa almasi hizo zimewekwa ndani ya dash bodi” alielezea.

Akielezea zaidi alisema kuwa mhindi ndiye alimwonyesha almasi kipande kimoja na kumwambia kuwa wamepakia nyingi hivyo awe mwangalifu njiani.

Hata hivyo haikuwa rahisi kujua kwa mbinu iliyotumika kwani pakati hizo za madawa ya kulevya yalifichwa kwenye maeneo mbali mbali ya gari ikiwepo kwenye chesesi, mashavu ya gari na maeneo zilimoungiwa taaa za mbele na za nyuma.
Aidha maeneo mengine dawa hizo zilifichwa ndani ya milango, sehemu  inayotenganisha AC na rejeta pamoja na kwenye mabomba ya kupitisha hewa ndani ya gati  ambapo iliwalazimu wakaguzi kuwaita mafundi magari waliobomoa sehemu mbalimbali za gari hilo na kutoa madawa.

Uchunguzi umebaini kuwepo kwa usafirishaji mkubwa wa dawa za kulevya  kutokana na mbinu kubwa ya wafanyabiashara hao ambao maafisa wa TRA siyo rahisi kung’amua.

mwisho
indaba2010

Nov 16, 2010

MH MAKINDA ANAPOTIA MGUU MJENGONI NA USAFIRI WA SPIKA

Aminia mama Mheshimiwa MAKINDA  naamini mjengo utatulia aaall zeeee besst   indaba2010

Nov 15, 2010

salam za OB kwa JK


Rais wa Marekani,Barrack Obama







Kwa niaba ya Marekani, Ninawapongeza watu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukamilisha uchaguzi mkuu hivi karibuni na kuendeleza utamaduni wenu wa kuendesha chaguzi za vyama vingi toka mwaka 1992.



Ninatarajia kufanya kazi na Rais Jakaya Kikwete na wabunge wa Bunge la Kumi tunapoendelea kujenga na kuimarisha ubia wa muda mrefu na wenye mafanikio kati ya mataifa yetu katika kuendeleza malengo ya pamoja ya maendeleo na kukabiliana na changamoto nyingi za kimataifa zinazotukabili.



Aidha, ninatoa pongezi zangu za dhati kwa Rais wa Zanzibar Ali Mohamed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais Seif Sharif Hamad, serikali mpya ya Umoja wa Kitaifa na zaidi sana kwa watu wa Zanzibar ambao wameweka historia kwa kufanya uchaguzi wa amani baada ya miaka kadhaa ya chaguzi zilizogubikwa na machafuko.



Kama nilivyomueleza Rais Kikwete nilipokutana naye katika Ikulu ya White House hapo mwaka 2009, Watu wa Marekani wanawaunga mkono Watanzania wote katika jitihada zenu za kuimarisha utawala wa kidemokrasia na uwazi, kutumia kikamilifu fursa za Muungano wenu na kuhakikisha kuwa hatua mlizopiga na mafanikio mliofikia katika kujenga amani na ustawi wa kudumu hayarudi nyuma.

Nov 9, 2010

WATOTO WANNE WAJIFICHA UVUNGUNGI MWA HOOD NA KUSAFIRI HADI DAR

Basi la Abood lenye namba za usajiri T542 AZE limenusurika kupata ajali jana baada ya Watoto wane wakazi wa mji mdogo wa Mbalizi mkoani Mbeya, kujificha na kukalia mdumowa breki kwenye chesisi ya basi hilo na kusababisha mfumo wa breki kushindwa kufanya kazi.


Habari kutoka kwa mmoja wa abiria waliosafiri na basi hilo Bwana Edmund Makombe na kuthibitishwa na kondakta wa basi hilo bwana Ayoub Nassoro, Watoto hao walikuwa wamejilaza kwenye mfumo wa breki na wengine kwenye chasis.

Imeelezwa na watoto hao kuwa walipanda waliingia kwenye basi hilo alfajiri katika kituo kikuu cha mabasi cha Mbeya na kujificha uvunguni kwenye chasis ambapo mmoja wao alijilaza kwenye waya za breki, na kwamba wakiwa karibu na hotel ya aljazeera iliyopo Ruaha Mbuyuni walishitukia dereva akisimamisha gari kwenye moja ya maeneo yanayofanyiwa matengenezo.

Kwa mujibu wa Kondakta wa basi hilo Ayoub Nassoro maarufu kama Nyerere , anasema wakati gari limesimama kwaajili ya kusubiri magari kupishana alienda kuchungulia uvunguni kwaajili ya kuangalia hali ya tairi na ndipo alipowakuta watoto wawili wakiwa wamekilaza kwenye difu ya nyuma.

Anasema kuwa baada ya kuwatoa hao wawili, walimweleza kuwa wapo wengine uvunguni humo na katika kuchugulia wakawakuta kwenye chasis huku mmoja akiwa ameshikilia waya za mfumo wa breki.

Watoto hao wamejitambulisha kwa majina ya Frank John (12), Fabi Yusuph (12), Christopher Tweve (10) na Yohaba Robart (12) wote wakazi wa Mbalizi nje kidogo ya jiji la Mbeya.

Wakizungumza katika hoteli ya Aljazeera ambako walinunuliwa chakula na wafanyakazi wa kampuni ya Abood na baadaye kuachwa ili warejeshwe mbeya na mabasi yanayoelekea Mbeya , wamesema sababu za kurtoroka kwao ni kutokana na hali ngumu ya maisha na kwamba walitegemea kwenda Dar es salaam kutafuta maisha.


Wanadai kuwa tayari kuna wenzao ambao wameshasafiri kwa utaratibu huo na kwamba hawana mawasiliano ingawa wanaamini wapo Dar es salaam na huenda wana maisha mazuri ndiyo sababu wakashawishika nao kwenda huko.
Licha ya kondakta kuelezea kuwa gari lilisimama katika utaratibu wa kawaida wa kulichunguza, mmoja wa abiria ambaye alikuwa karibu na kiti cha dereva anaeleza kuwa alimsikia dereva akimwelekeza kondakta huyo aangalie kwenye mfumo wa breki baada ya kubaini kuwa mzito tofauti na siku zingine.

Anaesema akiwa anaagalia uvunguni alibaini kijana huyo akiwa amejilaza kwenye waya wa breki na ndipo alipotoa taarifa kwa dereva kuwa kuna watu uvunguni.

Mashuhuda wa tukio hilo wameonekana kushangazwa na ujasiri wa watoto hao ambao wakati wakitolewa uvunguni walikuwa wamechafuka sana kutokana na vumbi la uvunguni kuwatanda usoni huku wakiwa wamechoka.

Nov 4, 2010

WALIOTEMBEZA JENEZA TUNDUMA WATINGA MAHAKAMANI

Vijana wawili wamepandishwa jana kwenye Mahakama ya mwanzo ya Vwawa wilayani Mbozi kwa kosa la kutembeza jeneza lililofunikwa bendera ya chama cha mapinduzi pamoja na msalaba katika mji mdogo wa Tunduma baada ya kutangazwa ushindi wa kiti cha ubunge kupitia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA jimbo la Mbozi Magharibi.


Waliopandishwa kizimbani ni Selemani Ibrahimu maarufu kama mwarabu na Maneno Halongo wote wakazi wa mji wa Tunduma.


Wakisomewa shitaka lao mbele ya Mh hakimu wa mahakama ya mwanzo Vwawa Ismail Karuta, mwendesha mashitaka wa polisi koplo Pascal Mkondya aliieleza mahakama kuwa mnamo Novemba 2 mwaka huu saa 7 mchana katika mji wa Tunduma watuhumiwa walibeba sanduku mfano wa jeneza na bendera ya CCM wakiimba nyimbo za mazishi kitendo ambacho kilikuwa cha uvunjifu wa amani.

Alisema chini ya sheria ya maadili ya Uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani namba 124 ya 1985 sura ya 342 kifungu kidogo cha 2 d pamoja na tangazo la serikali namba 273 la agosti 2010 ambalo linakataza vitendo vyenye lengo la kudhalilisha ama kukikashifu chama kingine.



Pamoja na kukana shitaka hilo, washitakiwa hao walishindwa kutimiza masharti ya dhamana baada ya hakimu Ismail Karuta kuwataka kudhaminiwa na watu watatu ambao ni watumishi wa serikali pamoja fedha kwa maneno kiasi cha shilingi 500,000/=. Watuhumiwa walipelekwa mahabusu hadi novemba 17 kesi yao itakapoanza kusilikilizwa.



Danny tweve Mbozi

indaba2010

Nov 2, 2010

CHADEMA YAVUNA UBUNGE MBOZI MAGHARIBI, CCM MBOZI MASHARIKI

Na Danny Tweve Mbozi.

Matokeo ya ubunge katika majimbo mawili ya Mbozi mashariki na Magharibi yanaonyesha vyama vya CCM na CHADEMA kugawana majimbo.
Wakati chama cha Mapinduzi kikichukua jimbo la Mbozi Mashariki kupitia mgombea wake Godfrey Zambi, Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimechukua jimbo la Mbozi Magharibi kupitia Mgombea wake David Silinde.

Akitangaza matokeo hayo Msimamizi wa majimbo hayo mawili Bw. Levison Chillewa ametangaza kuwa kwa jimbo la Mbozi Mashariki Godfrey Zambi wa CCM amepata kura49,095, wakati Allamis Mwampamba (CHADEMA) kura 31,997 na Nkunyutila Siame kupitia CUF amepata kura 839.

Kwa upande wa jimbo la Mbozi Magharibi Msimamizi huyo alimtangaza David Silinde CHADEMA baada ya kupata kura 20835, huku mgombea wa chama cha mapinduzi Dr Luka Siame akipata kura 20,203 na kasabuni Asukile ca CUF akiwa na kura 220.

Kwa upande wa madiwani jimbo la Mbozi mashariki CCM imechukua viti 16 kati ya 18 vilivyopo huku viti viwili vikienda CHADEMA kwa miji ya Vwawa na Mlowo. Jimbo la Mbozi magharibi CCM imeshinda viti 12 vya Udiwani na ChADEMA viti viwili ( 2) vya miji ya Tunduma na Ndalambo.



MWISHO