Adverts

Feb 28, 2011

Mambo ya Nyama Choma Umasaini

Nyama ya Ng'ombe ambayo imechomwa na kuhifabdhiwa juu ya mti kusubiri walaji.
walaji tulifika na kabla ya kupiga picha nilikatiwa mbavu nikajichana.
Ulaji qwa nyama kwa Morani wa Kimaasai ni wa kijamaa, watu huzunguka duara na mwenye nyama hukaa kati kati kisha kumkabidhi mkubwa katika kundi hilo na kukata kata kwa wote.
Hapa ndo nyama inakatwa katwa na kila mtu anapata kipande hadi nyama inakwisha.
Hapa tulisha shiba nyama na kupiga picha ya pamoja na vijana wa kimasaai kutoka kijiji cha Mabwegere, Wilayani Kilosa mkoani Morogoro.
"