Adverts

Mar 25, 2011

Haya Ndiyo Aliyoyasema Sumaye Kuhusu Matamko/ Shutuma Za UVCCM Zidi Yake

Nimejiunga na TANU tangu mwaka 1966, mimi ni mwana CCM tangu kuanzishwa kwake 1977 na ni mjumbe wa NEC Sina uhusiano mbaya na UVCCM, sina uhusiano mbaya na yeyote ambaye ni mwana CCM. Napenda kuongelea kuhusu 2015, sijaamua kama nitagombea au sitagombea Wananchi ndio wenye uwezo wa kila jambo katika nchi, wananchi ndio wanaopiga kura na ndio wanaoamua nani awe kiongozi na nani asiwe. Makundi matatu yanayoamua nani awe kiongozi ni WANANCHI, CHAMA anachotoka mwanasiasa na DOLA Kwanini nimewaita? Kumeibuka malumbano ndani ya CCM na UVCCM kutokana na matamshi ambayo yanakanganya na mimi ni mmojawapo ambaye nimeshambuliwa sana. Nipo hapa kwa niaba yangu mwenyewe, sijatumwa na yeyote na SIMSEMEI YEYOTE. Nipo hapa kama Frederick Sumaye. Ningeyapeleka kwenye chama hasa NEC lakini kwakuwa na wenzangu wameanza kwa mtindo wa kuitisha vyombo vya habari nami nafuata utaratibu huo Lengo si kushindana wala kupimana nguvu, lengo ni kuweka uwazi kwa wananchi watambue uhalisia Baada ya kuona wananchi wanavyoyapokea maandamano ya CHADEMA na kwa hamasa kubwa nilishauri CCM itoe ushirikiano kwa serikali kwa kuyajibu wanayotoa CHADEMA ili kuweza kuweka hali halisi. Mimi kusema CCM ifanye sikumaanisha MIMI SIMO. Aidha, sijasema serikali isifanye kazi yake. Waziri Wassira amefanya kazi ya serikali vema tu Katika utaratibu wa kawaida, chama kinafanya kazi yake baadae serikali inakuja kumalizia yanayobakia. Kama kazi ya siasa haijafanyika vema na chama basi serikali hubeba lawama zisizostahili. Malumbano ya kisiasa hujibiwa kisiasa, CCM walitakiwa kuwajibu CHADEMA na si kazi ya serikali kufanya kazi ya kisiasa CCM inafahamu kazi ya kisiasa na kimekuwa kikifanya hivyo tangu zamani. Viongozi wetu wamekuwa wakifanya hivyo kwenye kila ngazi. Ni shughuli ya chama na haihitaji maamuzi ya vikao. Akiongea Sumaye linaonekana tatizo kubwa na tena ni utovu wa nidhamu. Nimeshutumiwa na hata kutukanwa na wengine ndani ya chama Nifafanue: Nimeshutumiwa kuwa namshutumu mwenyekiti wa chama. Nilijibu nikadhani mambo yameisha kumbe ndo kwanza yameanza. Nimeshutumiwa na UVCCM Pwani kuwa - Sumaye na Lowassa wana mpango wa kukivuruga chama ili wafikie malengo yao 2015 Kama Lowassa na Sumaye wanautaka urais 2015, kwanini washirikiane? 2015 kutakuwa na marais wawili? Hakuna sehemu hata moja ambapo niliwahi kumtaja rais katika maongezi yangu, madai kuwa namtukana na kumchafua rais ni tuhumu za uwongo kabisa UVCCM wanadai sisi tumeshiba na sasa tumevimbiwa... Tuwaache nao wale kama sisi. Haya ni matusi na kejeli na inasikitisha sana Ina maana UVCCM wana mgombea wao ndo maana wengine tunaonekana kero kwao kwani tunamvurugia mtu wao. Vijana wenye tamaa ya KULA ni hatari kwa taifa Eti vijana wanataka wamweke mtu wao ili wale? Imenishtua sana! Wanadai tunakibomoa chama, wanadai kuwa tunataka rais atoke kaskazini. Kwa madai yao nchi itaendelea kusonga mbele na wanatupa pole tunaodhani rais lazima atoke kaskazini. Ubaguzi huu wa ukanda tena kutoka UVCCM mkoa wa Pwani usipochukuliwa hatua utalipeleka pabaya taifa! UVCCM wana mpango wa kupambana kina Sitta na Sumaye. Wanataka hawa wasipewe nafasi katika chama, wanadai watapigana ndani na nje ya chama kuhakikisha watu hawa hawapewi nafasi. My comment: Sitta yashaanza kumkuta ya UVCCM huko Tabora! Kuna maoni mengine yanaweza kuwa na athari kwa chama hivyo ni juu ya kiongozi husika kuangalia athari ya kutoa maoni husika. Serikali yoyote iliyochaguliwa kidemokrasia LAZIMA itasemwa na kukebehiwa. Kiongozi yeyote na chama chochote kilichochaguliwa kidemokrasia, kitasemwa na watu watakikebehi. Si ajabu Nimeshtushwa SANA na kauli ya UVCCM mkoa wa Pwani kuwa suala la rais ajaye 2015 lipo mikononi mwa rais Kikwete! Hili linanishtua, siamini kama rais Kikwete anamjua rais ajaye 2015 Sasa hivi mtu yeyote akiongea ndani ya CCM ataambiwa anautaka urais, hii inaweza kuwaziba wengi midomo Nawaomba watanzania, yeyote atakayejaribu kutumia njia za udanganyifu kwa RUSHWA, KUTENGANISHA WATU, tumkatae kwa nguvu zote Tunakosa muda wa kujielekeza katika mambo ya msingi tunaanza siasa za kupakana matope - Sumaye Nategemea nimeeleweka, sitarajii kuibua malumbano na sitarajii kurejea kuongea na waandishi juu ya hili. Mimi ni mwana CCM na sipo chama chochote cha siasa zaidi ya hiki. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika MASWALI SWALI: Kwanini hujaandika barua CCM? JIBU: Mimi sijaandikiwa barua, sijibu kwa barua SWALI: Mtu akikutukana ujue KATUMWA NA BABA na ndo maana baba kakaa kimya. Kwanini usijiondoe CCM? JIBU: Ukiona mtoto anamtukana mtu mzima uelewe ametumwa ama anamtukanisha mtu mzima lakini kwa hili la sasa yote yamo. Maana hatujakaa kutuma vijana. Siwezi kutoka CCM sababu ya vijana SWALI: Toka miaka ya 70 kwanini watu wa kaskazini wanasemwa vibaya? Hawafai? Toa ufafanuzi kuhusu kauli yako ya 2005 kuwa ATAKAYEINGIA KWA KUCHAFUA WATU KWA KALAMU ATATUMIA VISASI kuongoza. JIBU: Nilishasema awali, ubaguzi wa kimaoeneo ni hatari sana na si kwa kaskazini tu. Kuhusu suala la U-Kaskazini haina maana maana haijawahi kutoa rais hata akitokea Bagamoyo leo akawa anafaa hakuna neno. Tusitazame watu kwa wanakotokea ama dini zao na rangi zao. Hata bungeni kuna kauli za kibaguzi, tumezikemea bila kujali eneo. Pili, ya 2005: Ni tabia mbaya kuchafuana hata kama ni udiwani, niliyasema na bahati hayajatokea. SWALI LA KUBENEA: Vijana wamejitokeza kutetea mafisadi, unatoa rai gani? Lakini ultimatum wanazotoa si sahihi, labda watoe ushauri. JIBU: Vijana wanatetea mafisadi ama nani, sijui... ila misemo yao inanitisha SWALI LA BBC: Imejitokeza kuzungumza mambo ya chama nje ya chama, kama chama mnalionaje hili haliwaaibishi? JIBU: Future ya CCM ni nzuri ila kuna mambo LAZIMA yafanyike. Yale madhaifu lazima tuyaondoe. kutoka www.mjengwa.blogspot.com
"