Adverts

Mar 25, 2011

MASHOSHOROZA(TRENI) ZA TAZARA ZIFANYIWE MABORESHO

 Hizi taa za Treni zimeshachakachuliwa vioo vyake kwahiyo unalala kimachale hasa ukiwa kwenye deka!
 Mbu kibao hakuna net!!! jamaa wa upande wa pili wa deka langu nilimvizia akiwa amelala nikabonyeza kamera kutaka ushahidi wa huduma za TAZARA!  blanketi na shuka pia changamoto zingine hazifuliwii!

 Hapa sikulenga kuwaonyesha hawa jamaa wakiwa wamekaa kwenye second class ila nilitaka nionyeshe hiyo soketi pembeni haifanyi kazi waya zake zilishachakachuliwa nikashindwa kupost matukio yote kwa siku hiyo kwakuwa hakukuwa na chaji kwa laptop
 Hapa ndiyo TOILET aka mariwatoni, kwa treni la Express la zambia wanajitahidi kufanya usafi na kuweka maji wakati wote, lakini nimeambiwa express ya Bongo ni bongo kweli kweli hakuna cha maji wala nini, unaenda huku na chupa yako ya maji!!!!!