Adverts

Mar 25, 2011

"Matajiri" wanavyodhalilisha watawala waroho

Zuma amwagiwa pombe Kituko kilitokea hivi karibuni nchini Afrika Kusini ambapo rais Jacob Zuma alimwagiwa pombe na mwananchi mmoja. Zuma ambaye anasifika kwa kupenda vimwana na matanuzi alipatwa na mkasa huu mjini Durban nchini mwake. Japo yaweza kuchukuliwa kama bahati mbaya, huu ni ushahidi kuwa watawala wetu wanajifanyia mambo hovyo hovyo hasa kutokana na kujiingiza kwenye shughuli zinazoweza kuhatarisha usalama na hata madaraka yao. Inakuwaje kiongozi wa nchi ajikute kwenye mazingira rahisi kumwagiwa pombe? Kuna siku watanaswa vibao kutokana na kuwa na shughuli haramu za siri. Kwa habari zaidi, BONYEZA HAPA
"