Adverts

Mar 25, 2011

MJAMAICA AAMUA KUSHUKA KWENYE TRENI NA KUONYESHA MAZINGAOMBWE KWA ABIRIA WENZAKE

 Mjamaica aliyefahamika kwa jina la Fernando akizungumza na wandishi wa dtweve.blogspot juu wakati akijiandaa kutoa vimbwanga kwenye behewa la daraja la pili TAZARA jana katika moja ya stesheni ambako alishuka na kuanza kufanya mazingaombwe.

 Kisa cha kuonyesha mazingaombwe ni baada ya kuhama kutoka daraja la tatu na kuja kujificha daraja la pili chumba ambacho mwandishi wa mtandao huu alikuwemo, sasa akaanza kuomba kaptula kutoka kwenye begi la Mwandishi wa mtandao huu, jambo ambalo kidogo lilikuwa gumu kwani siyo kawaida kuvaliana nguo na mtu usiye mfahamu labda  mkeo!!, lakini jamaa aling'ang'ania huku akizungumza kingereza cha kuunga unga akiitaja kama Puantalelo, hii ilitokana na yeye kutaka afue suruali yake haraka halafu aikaushe, sasa hapo ndipo watu wakataka waone anaikaushaje haraka naye akawaambia mbona rahisi tu, ngoja niwaonyeshe vimbwanga vingine kabla sijakausha! ilibidi nizame na nitoe kaptula yangu hiyo na ndipo akawa huru na kutoka nje ya behewa na kuanza kufanya show hadharani kama anavyoonekana. Alichonifurahisha zaidi yeye anaona tu Tanzania sawa na jamaica ni nchi ya kijamaa kwa hiyo kila kitu yeye alikuwa anaomba, naomba maji ya kunywa, naomba sijui nini!!!! bahati mbaya treni la express la jana lilikuwa la wazambia hawana huo utaratibu wa kuombana ilikuwa  balaa kwake akaanza kutukana Boushiiiiiiiiiit mother.....f.....c...k nakadharika ikawa kituko kwenye treni hilo, manake walimg'ang'ania aende third class hadi wakamfikisha
Wanufaika wa show yake wakiwa wanachungulia dirishani wakati akifanya mambo yake hapo ilikuwa stesheni ya Mbeya