Adverts

Oct 17, 2011

Ivi kuna hasara gani ukifanya haya

Wanaume sometimes tunakuwa wabishi na tunashikiria mambo fulani ambayo hata hayana maana. Tuna poteza vionjo kidogo kidogo na siku tunajikuta kwenye ndoa zenye zero gravity bila hata wenyewe kujua inakuaje. Si wote najua kuna watu wanafanya kazi yao vizuri hata wake zao wanawahitaji 24 hrs. Mume akisafiri mke hana raha, akichelewa hata kama aetoa taarifa bado hata lala hadi arudi. Fikiria majibu yako ktk maswali yafuatayo na kama hata nusu ni siyo kazi ipo. naweza kua nakosea kwa malezi niliyo ppewa lakini ukweli utajulikana. 1. Ni mara ngapi umemwamusha mkeo kwa busu asubuhi?? 2. Ni mara ngapi umefua nguo yoyote ya familia iwe ya mtoto au ya mkeo, najua upo buse lakini mbona baa hukosi?? 3. Ni mara ngapi mkeo akikukuta nyumbani umewahi mpokea walau beg lake tuu?? 4. Ni mara ngapi umemtukana mkeo au umedharau bele ya watoto au hadi majirani wanajua?? 5.Ni mara ngapi ummemsaidia mkeo hata kusogeza kisu jikoni wengine hata wajawazito wanafanya kazi wakati jamaa anacheck manunited?? 6. Ni mara ngapi umekaa na wanao kuwambia habari nzuri za mkeo?? 7. Ni mara ngapi umeshiriki usafi wa nyumbani?? Tusiwalaumu wanapo kosea, tuwaonye kwa upole na kuogopa. Watatuheshimu kupita upepo. Attachment 39332
kutoka jamii forums
Attached Images