Adverts

Dec 29, 2011

Serikali Yaanza Kutia Alama Nyumba Zitakazobomolewa Mabondeni Jijini Dar es Salaam

Mkazi wa Jangwani bondeni, Dar es Salaam, Mohamed Zuberi akilalamika mbele ya wanahabari jana, kuhusu utaratibu unaotumiwa na maofisa wa Manispaa ya Ilala kuhakiki nyumba zao zitakazobomolewa kufuatia amri ya Serikali.
Mkazi wa Jangwani, Dotto Ngoyeji akieleza malalamiko yake mbele ya wanan habari, kwamba Serikali inatakiwa kuata utaraibu kuwatendea haki katika mchakato huo wa kuhakiki nyumba zao.
Mmoja wa maofisa wa kutoka Manispaa ya Ilala, akiweka alama katika moja ya nyumba eneo la Jangwani.
Mama mkazi wa Jangwani, Dar es Salaam eneo lililokumbwa na mafuriko hivi karibuni, akiwa na huzuni baada ya nyumba yake kuwekwa alama ya kubomolewa na wakati wa mchakato wa kuhakiki nyumba hizo uliokuwa unafanywa na Maofisa wa Manispaa ya Ilala.Picha Zote na Richard Mwaikenda