Adverts

Jun 30, 2011

KWA SUPU YA MAKONGORO SONGEA MPO JUUU

Wafanyabiashara wa supu ya magongoro wakiandaa kwa ajili ya wateja wao katika stand kuu wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma,ambayo uuzwa kati ya tshs 1000 na 1500 kutegemea na ukubwa,
PICHA  NA MUHIDIN AMRI

KAMBALE BWANA KWA UBWABWA HASA VIJIJINI!!

Mchuuzi wa Samaki wakavu aina ya perege  ambaye alikataa kutaja jina lake akipanga kitiwep hicho katika mazingira ambayo siyo lasama klwa walaji kama alivyokutwa na mpiga ppicha wetu mjini Namtumbo hivi karibuni-PICHA NA MUHIDIN AMIR

CHINGA WA SONGEA KWAO KAMA JADI KILA SIKU KILOMETA 200

Vijana wanauza nguo za mitumba wakitembeza nguo hizo mitaani mjini Songea ,kufuatia manispaa  hiyo kuvunja vibanda vyao vilivyjengwa bila kufuata utaratibu kwa lengo la kuweka manispaa hiyo katika hali ya usafi-Picha na mdau Muhidin Amir Ndolanga!

Jun 28, 2011

MWANAMKE KIJEBA APATIKANA BRAZIL ANA MIAKA 120!!

Bi Mkubwa Kijeba!!!
Jina lake anaitwa Maria Lucimar Pereira na ameripotiwa kuwa na umri mkubwa duniani kwa kugonga miaka120. Ndiyo ! siyo 120 namba ni miaka mia ishirini akiwa hai duniani!!

Wafanyakazi wa Taasisi ya huduma za hifadhi ya jamii nchini Brazil   INSS walimbaini kikongwe huyo wakati wakifanya mapitio ya kawaida ya kumbukumbu za kuzaliwa  kwa watu wao wanaowahudumia.
Kwa mujibu wa habari iliyochapishwa Ijumaa kwenye usiku kwenye mtandao wa nchini humo wa
 Folha de Sao Paulo  ilionyesha kuwa bi Mkubwa huyo alizaliwa September 3, 1890.
Bi Pereira is mzawa wa nchi hiyo na anaripotiwa maisha yake yote kuyatumia ama kukulia akiwa vijijini katika kaskazini kusini mwa Brazil katika jimbo la Amazon karibu na mji wa Feijo  unaokadiriwa kuwa na watu 32,261
jamani muda mdogo naomba muendelee kutafsiri.....
When social workers found her birth records they radioed the isolated indigenous community where she lives (there is no mobile service) and arranged to have her brought to the nearest town to confirm her identity.
She is apparently from the kaxinawa indigenous ethnic group, and reportedly she speaks only a few words in Portuguese.
The social workers are still trying to verify if there were any mistakes made on her birth certificate, but no irregularities have cropped up as of yet.
If it is verified that Ms Pereira really is 120, she would instantly become the world’s oldest living person - by far.
Oddly enough, earlier this week Brazilian woman Maria Gomes Valentim passed away. She was 114, and at the time of her death regarded by the Guinness Book of World Records as the oldest living person.
As for Ms Pereira, it’s said she has 10 kids and 22 grandchildren.

HIVI PENYEWE MNAPOSEMAQ DONDOSHA MKONO WA SWETA NDIYO NINI? NYEEE!!!

Bagia za Iringa  unazikumbuka? sasa kampeni ni kudondosha Mkonosweta  yaani kuondoa kofia ya asili kwa wanaume!! aka kutahiri ili kupunguza risk ya maambukizi. Kampeni hii imeshika kasi mkoani humo


Mabango ya HAMASA ya kuwataka wanaume wakaondoe mikono ya sweta bure, tayari mwitikio umekuwa mkubwa kwa umri wa vijana ingawa shida ni kwa wazee wanaonekana kujishauri sana kabla  ya kufanya maamuzi, si unajua masuala haya ni silka na imani

TUKIKOSA SAMAKI HUWA TUNAVUA NGADO!!! HII KOROGORO KWENYE MIFEREJI

Dogo huyo aliyetambulisha kama Husein akivua ngado katika mfereji unaopita nje ya ofisi za Hood mjini morpogoro ingawa alisema wakati mwingine hubahatisha samaki wadogo aina ya Kampale!!!

JAMANI HOOD HAWA NDEGE ULIOFUGA NI MAPAMBO AMA MAMBO MENGINE?

Ukiingia ofisini kwenye yard za Kampuni ya Hood unakutana na vurugu za ndege hawa njiwa wakiruka huku na kule huku wakiwa wamehifadhiwa magunia ya ufuta kama chakula, najiuliza ni mapambo, kitoweo ama mambo yeeeeetu yaleeee!!!!!!

Hood Bus likiingia getini kwenye ofisi zake Morogoro

LORI LA SERIKALI MOROGORO HOI LAKINI LIMO BARABARANI

Gari la serikali Mkoani Morogoro likikatiza barabara lakini sura yake huko mbele ni majeraha matupu kiasi cha kuhatarisha usalama barabarani, baada ya safari ya kilometa moja eneo la Kihonda likashindwa kuendelea na safari.

ALJAZEERA RESTAURANT KULA DAKIKA 10!!!!

Hapo ndipo Aljazeera restaurant ambapo abiria anayetokea Dar ama Mbeya lazima apapitie, sasa cha kufurahisha ni matangazo ya ABIRIA KULA DAKIKA KUMI!!!  hivi wataalamu tuambieni biunadamu anatakiwa achukue dakika ngapi wakati wa kula?

Bidhaa zilizopo zinazingatia mahitaji ya makundi mbalimbali wapo wanaotaka vitu vigumu vigumu na wale wa vitu laini!!!!

Hapa mahudhulio zaidi ni akina dada !!!Chipsi kuku!!!

Unakokwenda lazima uende na zawadi, pitia hapa nunua halafu unapokelewa kwa heshima siyo mikono mitupu!!!

Twanga tuuuuu!!! ongea mpaka basi, Aljazeera imeunganishwa kwa mawasiliano bila kujali mazingira yake kuwa porini!

DODOMA UMEME JANA USIKU ILIKUWA HIVII!!! UNAPAPASA KWA MKONO TOI

Hotelini kwangu mambo yalikuwa hivi!!!!!!!!!!!

Mitambo ya Umeme iliyopo Msamvu

WADAU WAELEZEA MBINU YA KUTANGULIZA MAFUNZO KABLA YA FEDHA ITASAIDIA

BW. Kita kutoka wilaya ya Mbarali akizungumza katika mahojiano jijini Dodoma kuhusiana na hatua ya Foundation for Civil Society kuzijengea uwezo asasi kabla ya kutoa fedha zao ili kuepusha matumizi mabaya na usimamizi mbovu wa miradi hiyo
Mdau mwingine kutoka YES Tanzania wilayani Ileje akizungumzia ufadhiri huo ambao utasaidia kuwafikia vijana walio vijijini

Jun 27, 2011

Muammar Gaddaf Suggest to arrest

The International Criminal Court has issued an arrest warrant for Libyan leader Col Muammar Gaddafi, accusing him of crimes against humanity. The court had grounds to believe he had ordered attacks on civilians during Libya's four-month uprising, it said. The Hague-based court also issued warrants for two of Col Gaddafi's top aides - his son Saif al-Islam and intelligence chief Abdullah al-Sanussi. Thousands of people are believed to have been killed in the conflict.
Anti-Gaddafi forces said on Monday they had launched a new push towards Tripoli, with heavy fighting near the strategic town of Bir al-Ghanam, to the south-west of capital. The rebel defence minister told the BBC that forces opposed to Col Gaddafi may also make a move on the capital from the east.-By Rashid Mkwinda with International Correspondents.

DODOMA ASUBUHI HII> FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY YAANZA KUJENGA UWEZO WA USIMAMIZI RUZUKU KWA MASHIRIKA 39 NCHINI


Afisa kutoka Foundation for Civil Society Bw. Omary Jechu akizungumza kwenye mafunzo hayo yanayohusisha waratibu wa Mashirika/Miradi na wahasibu wao katika mafunzo ya siku sita ya usimamizi wa fedha za miradi iliyoombwa na  kupitishwa ambapo mashirika 39 kutoka nchini kote yanashiriki. Mafunzo hayo yanafanyika katika hoteli ya Dodoma 




Mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo hayo Bi Neema Yobu akizungumza kwenye mafunzo hayo katika ukumbi wa Mazengo




Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakiwa makini kufuatilia yanayotolewa na mwezeshaji ili hatimaye kupunguza kasoro mbalimbali zinazojitokeza katika utekelezaji wa miradi inayofadhiriwa kupitia ruzuku kutoka Foundation for Civil Society

Afghanistan: Eight-year-old girl 'used in attack'


An eight-year-old girl has been killed after insurgents used her in a bomb attack on police in southern Afghanistan, the government has said.
The interior ministry said insurgents gave the girl a package and told her to take it to a police vehicle, detonating it as she approached.
No-one else was killed in the explosion, in Uruzgan province.
The incident came a day after an attack on a hospital which killed at least 38 people in the east of the country.
Dozens were injured. Elderly people, pregnant women and children were said to be among the casualties.
'No respect'
A statement by the ministry described the Uruzgan incident as a "crime and a shameful act".
The area where the alleged incident happened is very remote, and it was not possible to independently verify the reports.
"The child, pure-hearted and in good faith, took the bag and moved towards the police vehicle," it said.
"As she got close to the police vehicle, the enemy detonated the bomb by remote control, killing the innocent child."
The governor of Char Cheno district, where the attack took place, told the BBC the girl was from the nearest village.
She was told nothing would happen to her, he said, adding that the perpetrators had "no boundary, no respect for anything".
Correspondents say insurgents have recruited both adult women and recently male children to carry out suicide attacks, though the Taliban denies recruiting children.
End..

Jun 25, 2011

MAZIWA NI MUHIMU KWA AFYA YA MTOTO

Kijana wangu Christian siku alipofurahia fulsa ya maziwa aliyowekewa na babaye

KILIMO KWANZA LEO TUNAWALETEA KALENDA YA MAZAO YA MPUNGA NA ALZETI



TEOFILO KISANJI UNIVERSITY WAZINDUA MAKTABA YAO LEO



Haya ndiyo mazingira ya chuo kikuu cha Teofilo Kisanji kama yalivyoonekana leo hii wakati wa uzinduzi wa maktaba na Ukumbi wa Mikutano, nilikuwa na safari zangu nikakutana na shughuli hii ingawa sikuifuatilia kiundani

FAMILY HEALTH INTERNATIONAL YAANZA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA KUIMARISHA AFUA ZA UKIMWI KWENYE MIRADI YA UJENZI WA BARABARA YA TUNDUMA HADI SUMBAWANGA

Moja ya ofisi za Kampuni ya CCC inayojenga barabara Lot 1 kutoka Tunduma hadi Ikana wilayani Mbozi

Baadhi ya wataalamu wa kampuni hiyo wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na maofisa kutoka FHI wakati wa kutoa mrejesho juu ya utekelezaji wa afua za kudhibiti maambukizi mapya kwenye eneo la mradi mradi unaolenga kuikinga jamii na wafanyakzi wa mradi huo


Magari ya Kampuni ya Consolidated Construction Company yakiwa yard
Mfanyakazi wa Kampuni ya CCC akiwasiliana huku akiwa na kitabu cha kurekodi mwenendo wa magari, nyuma yake ni sehemu ya ujenzi wa makazi ya wataalamu wa kampuni hiyo ambao kwa sasa wanaishi hotelini.



Bw. Ipyana kutoka FHI akitoa maelezo namna ambavyo mradi huo umeweza kutekelezwa kwa kipiundi cha kuanzia mwezi Februaly mpaja sasa na changamoto zilizopitiwa wakati wa utekelezaji

BARAZA LA MADIWANI MBOZI LATISHIA KUKAMATA WATAKAOJIPENDEKEZA KUNUNUA KAHAWA MBICHI WILAYANI HUMO

Waheshimiwa madiwani wa baraza la Mbozi wakifuatilia mjadala katika kikao cha kufunga mwaka wa fedha wa serikali ambapo pamoja na mambo mengine wamekubaliana kusitisha mara moja ununuzi wa kahawa cheri baada ya kubainika kuchangia kushusha ubora wa zao hilo na kuwapunja wakulima

Kamati ya uchaguzi ikihesabu kura za nafasi ya Makamu Mwenyekiti ambapo madiwani wawili walikuwa wakiwania nafasi hiyo kutoka vyama vya CHADEMA  na CCM

Mgombea wa nafasi ya Makamu mwenyekiti wa Halmashauri Mbozi MH Mwesya kutoka Kata ya Tunduma akiwa amepozi kusubiria matokeo ya kura za uchaguzi huo ambapo aliweza kuambulia kura 7 kati ya 43 zilizopigwa

Mh Bernard Sichilonga Diwani wa Ivuna akisubiria Matokeo ya uchaguzi wa nafasi aliyokuwa akiitetea ya Makamu mwenyekiti  ambapo aliibuka na ushindi wa kura 36

Katibu TawalaWilaya ya Mbozi Leonard Magacha akisisitiza mpango wa kukamata watu watakaojihusisha na ununuzi wa kahawa mbichi

Mwenyekkiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mbozi Elick Minga aklitangaza rasmi vita dhidi ya makampuni yanayonunua kahawa Mbichi wilayani humo ambapo imeelekezwa kuwa wananchi wachukue uamuzi ikiwa ni pamoja na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola na mwanasheria wa  halmashauri hiyo atasimamia mashauri hayo

Jun 23, 2011

WILAYA YA MBOZI YATANGAZA VITA NA KAMPUNI YA LIMA INAYONUNUA KAHAWA MBICHI

Na Danny Tweve
Uongozi wa wilaya ya Mbozi pamoja na baraza la Madiwani la halmaashauri ya wilaya hiyo kwa kauli moja wametangaza vita dhidi ya kampuni yoyote itakayobainika kununua kahawa Mbichi maarufu kama kahawa cheri.

Msimamo huo umetangazwa kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichoketi leo katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya, ambapo imeelezwa kuwa tayari watendaji wa vijiji, kata pamoja na jeshi la polisi wameshapewa maelekezo kutekeleza agizo hilo.

Akichokoza maelekezo hayo Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Elick Ambakisye amesema, kwa muda mrefu kampuni na wafanyabiashara wametumia uelewa mdogo wa baadhi ya wakulima katika kujinufaisha kwa kununua kahawa cheri ambayo bei zake ni sawa na kuwaibia wakulima wakati bei ya sasa ya kahawa kavu ni mara 100 ya bei wanayouza kahawa cheri.
Alisema hali hiyo imefikia hatua kuwafanya wananchi kurejea kwenye ukoloni wa kipato ambacho wamekuwa waklizalisha kwa jasho kubwa lakini wachache wanajinufaisha, na kwamba kampuni itakayokutwa ikifanya manunuzi hayo mwaka huu ni kuwakamata watendaji wake.
Akichangia kwa upande wa serikali kuu katibu tawala wilaya ya Mbozi Magacha akkizungumza kwa niaba ya mkuu wa wilaya alisema msimamo huo utatoa mfano mwaka huu kwakuwa kampuni ya Lima baada ya kuona imebanwa wilayani ikapita njia zake za vichochoroni na kufanikiwa kupata leseni ya kununua kahawa, wakati ambapo haikubaliki katika eneo ambalo wanataka kununua.
Alisema ili kuonyesha hasira za wananchi, kampuni hiyo ikituma watendaji wake vijijini wakamatwe na kuchukuliwa hatua papo hapo na kwamba maelekezo yameshatolewa kwa mamlaka za dola wilayani humo.

Mwaka jana wilaya ya Mbozi imejiingizia zaidi ya Bilion 100 kutokana na mauzo ya kahawa yake kupitia vikundi vya wakulima katika mnada wa moshi ambapo halmashauri ya wilaya iliweza kukusanya zaidi ya shilinmgi 1.5 Bilion ikiwa ni ushuru wa zao hilo.
Kampeni za kumlinda mkulima zilianza kutekelezwa mwaka jana ambapo watendaji wa kampuni ya Lima walikamatwa wakati fulani wakinunua kahawa cheri vijijini na baadaye kuachiwa, lakini msimamo wa mwaka huu unalenga kuhakikisha kahawa hiyo haiuzwi  ikiwa mbichi kutokana na bei yake kupanda mara dufu hadi kufikia 20,000 kwa kilo vijijini kwa kahawa kavu.

Wakati tamko hilo likitolewa kuna taarifa kuwa kuna watu wanazunguka vijjini kununua kahawa cheri kwa bei ya shilingi 50,000/ kwa ndoo ya plastiki ya lita 20 hali ambayo inawarusha roho wakulima na kushindwa kuvumilia kuuza kwenye soko rasmi na badala yake kuuza kwenye soko la kahawa cheri ili washike haraka hiyo pesa ya fasta fasta.
Ikiwa msimamo wa wilaya hiyo utasimamiwa vyema kuna kila dalili za ushindi wa mkulima wa wilaya ya Mbozi kuendelea kufanywa kichwa cha mwendawazimu cha kujifunzia kunyoa.
Wakati hayo yakiendelea tuhuma za aliyetoa leseni hiyo zinaelekezwa kwa waziri mwenye dhamana na kilimo kutokana na bodi ya Kahawa kukataa tangu mwaka jana mchezo wa kuuza kahawa cheri. Inaelezwa kuwa kampuni ya Lima ilienda kumwona mh waziri wa Kilimo ili kuiruhusu kununua kahawa hatua ambayo iliwezesha leseni hiyo kuagizwa kutolewa na mh waziri.

Pamoja na hatua hiyo, kuna tishio kuwa kuna uwezekano wa kusababisha uharibifu wa mali na hata kusababisha maafa vijijini wakati kampuni hiyo itakavyojihusisha na ununuzi huo ikiwa  maelekezo yaliyotolewa yatatekelezwa kwakuwa imeelezwa wazi kuwa magari ya kampuni hiyo yakikutwa yakinunua kahawa cheri hatua za ndani ya vijiji na zile za kidola zichukuliwe.

Tangazo hilio pia limeelezwa kusimamiwa na waheshimiwa madiwani.