Adverts

May 1, 2012

MEI MOSI DODOMA KUMEKUCHA ASUBUHI

  
Ndivyo sanamu ya mwalimu Nyerere ikionyesha kulinyoshea mkono jengo la chamacha Mapinduzi katika mji wa DODOMA ambapo asubuhi wafanyakazi wanaandamana kuelekea viwanja vya Jamhuri kwaajili ya maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei Mosi.
Hawa ni watu muhimu katika kuifanya miji yetu ilingane na hadhi zake, hapa wakiwa na zana zao katika maandalizi ya maandamano katika viwanja vya  Nyerere Square
  

Hapa ni waahadhiri wa chuo cha Mipango DODOMA wakibadilishana mawazo wakati wa maandalizi ya maandamano katika viwanja vya Nyerere square mjini DODOMA
  

Profesa Zilihona akizungumza na wahadhiri wengine wa chuo cha Mipango, anayeonekana kuchangia hapo ni Dr Malila, kulia  ni Bwana Haule afisa Habari na mawasiliano Chuo cha Mipango Dodoma
  

Ni katika kuhanikiza sherehe za Mi Mosi mjini Dodoma, chuo cha Mipango chajiakisi namna kinavyokabili changamoto za ajira kwa wahitimu wake
  

 

Mdau wangu wa siku nyingi toka tupoteane, Dr Ngumbi katikati akiwa na wafanyakazi wenzake wa halmashauri ya wilaya ya wilaya ya Mpwapwa katika viwanja vya Nyerere
  

Ni katika mazingira ya maandalizi ya maandamano hapa Nyerere square Dodoma endelea kuwa nasi tukufahamishe yanayojiri