Adverts

Aug 14, 2012

PICHA KUTOKA BUNGENI JIONI YA LEO

Waziri wa habari, vijana, utamaduni na michezo Dkt. Fenela Mkangara(kulia) akijadili jambo na Naibu waziri wa Ujenzi Eng. Gerson (katikati) wabunge wa viti maalum Maulida Komu (kushoto) nje ya ukumbi wa bunge ambako mkutano wa nane unaendelea.

Mbunge wa Ilala Mussa Zungu Azzan (kulia) akiongea jambo na Mbunge wa Kigoma Kaskanzini Zitto Kabwe (kushoto) katika viwanja vya Bunge leo mjini Dodoma wakati wakiingia ndani ya ukumbi wa bunge kwa ajili yakuhudhuria mkutano wa nane, kikao cha arobaini na saba kinachoendelea mjini humo.

Msemaji Mkuu kambi ya upinzani wizara ya Maliasili na Utalii Mchingaji Peter Msingwa akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu uamuzi wa Serikali wa kuwafukuza kazi watumishi watatu wa wizara hiyo badala ya kuwachukulia hatua wwatumishi wote waliohusika kwenye sakata la usafirishaji wa wanyama pori kupitia Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro kwenda Quatar. Kulia ni Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi akifuatiwa na Mbunge wa Musoma mjini Vicent Nyerere.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitoa wosia kwa wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika mitihani ya kidato cha sita kwa mwaka 2012 bungeni leo mjini Dodoma. Wanafunzi hao 10 wasichana na 10 wavulana wamepewa cheti , kopyuta ya pakato (laptop) na fedha taslimu shilingi laki mbili kwa kila mmoja.

Wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika mitihani wa kidato cha sita kwa mwaka 2012 wakiwa katika picha ya pamoja nje ya ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma. Wanafunzi hao 10 wasichana na 10 wavulana wamepewa cheti na Waziri Mkuu, kopyuta ya pakato (laptop) na fedha taslimu shilingi laki mbili kwa kila mmoja.
Picha na Anna Nkinda – Maelezo

WAZIRI MKUU PINDA ATOA CHANGAMOTO KWA WANAFUNZI KUWA NA NIDHAMU ILI WAFAULU

NA MAGRETH KINABO- MAELEZO, DODOMA
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewataka wanafunzi wote nchini kuwa na nidhamu , kujituma na kufuata maelekezo vizuri ya walimu wao na kuepuka makundi mabaya ili kuweza kupata mafanikio katika masomo yao.
Aidha Waziri Mkuu Pinda amewaasa wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kuhitimu kidato cha sita wa mwaka huu kutumia uhuru vizuri watakaoupata kwenye maisha ya vyuo vya elimu ya juu bila kurudi nyuma katika maendeleo ya masomo yao.
Kauli hiyo ilitolewa leo na Waziri Mkuu, Pinda Bungeni mjini Dodoma kabla ya kuwatunuku vyeti vya kuwapongeza wanafunzi hao 19 kati 20 waliofanya vizuri katika mtihani huo,kutoka shule mbalimbali nchini, ambapo mmoja wao, Jamal Juma yuko nje ya nchi.
Wanafunzi hao ambao wote walipata ufaulu wa daraja la kwanza katika mtihani huo, saba kati yao wanatoka katika shule ya wasichana ya Marian, watatu Mzumbe, wawili Fedha na wengine wawili Kibaha. Waliobakia mmoja mmoja anatoka Kilakala, Ufundi Ifunda, Tabora girls, Tabora boys, Minaki na Mpwapwa.
“Mmefanya vizuri. Mnastahili ! Hongereni Sana. Tunataka ufaulu wenu uwe mzuri zaidi kwa vile sasa ninyi mnakweda kujenga weledi. Mnakuwa wataalamu wa fani Fulani. Tumieni muda wenu kujifunza zaidi kutafuta maarifa zaidi na kuvumbua mambo makubwa zaidi yatakayowasaidia ninyi wenywe na jamii kwa ujumla kujiletea maendeleo,” alisema Waziri Mkuu Pinda.
Aliongeza kuwa ni vizuri utaratibu huo wa kuwatambua wanafunzi bora uwe endelevu na ikiwezekana wapatiwe fursa ya kuendelezwa katika vyuo vikuu vya kipekee nje ya nchi hususan kwenye fani zitakazojenga uwezo kwa taifa.
Waziri Mkuu alisema kati ya shule 10 ,ambazo wanafunzi hao wanatoka, wawili ni kutoka shule za kata, ambao ni Ester Marcel toka shule ya sekondari ya wasichana ya Olele Kilimanjaro na Brighton Lema toka shule ya sekondari ya Kitangiri, Mwanza.
“Napenda niwape pongezi za pekee wanafunzi hawa kwa jihudi kubwa walizozionesha. Kufaulu kwao kunadhihirisha kwamba shule hizi za kata tukiweka bidii kwa kuziwezesha zaidi zitafanya vizuri zaidi kama ilivyo katika shule nyingine,” alisisitiza .
Waziri Mkuu pia aliwataka walimu wote nchini kushirikiana na wazazi na serikali kwa pamoja kufundisha watoto kwa bidii ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao kama wanafunzi hao waliotunukiwa vyeti hivyo.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa alisema wanafunzi hao watazawadiwa pakato (laptop) na sh. 200,000, pia kila shule iliyotoa mwanafunzi bora itazawadiwa sh. milioni moja katika hafla maalum itakayofanyika jioni.
Wanafunzi hao wanatoka katika mchepuo wa PCM ambao ni 16 na mmojammoja toka mchepuo wa PGM, CBA, ECA na HKL.
Naye Spika wa Bunge la Jamhuri, Anna Makinda aliwataka wanafunzi hao kuwa makini na makundi kwa kuyasilikiza huku wakitumia akili zao huku akitoa changamoto shule nyingine kujitahidi kufanya vizuri.
MWISHO.

TAASISI ZA WAMA NA EOTF HAZITUMII RASILIMALI ZA SERIKALI

NA MAGRETH KINABO- DODOMA, MAELEZO
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora,Kapteni George Mkuchika amesema kuwa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo(WAMA) na Taasisi ya Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote(EOTF) zilianzishwa na kuandikishwa kwa mujibu wa sheria inayotawala taasisi hizo na wala hazitumii rasilimali za serikali.
Kauli hiyo ilitolewa na Waziri Mkuchika wakati akijibu swali Bungeni la Mbunge wa Viti Maalum(CHADEMA) , Naomi Kaihula ililoulizwa na Leticia Nyerere Viti Maalum (CHADEMA) kuwa kuwekuwepo na tabia ya wake wa marais hapa nchini kuunda NGO’S na kuzisajili kama taasisi zao binafsi wakati zinatumia rasilimali za serikali.
Je seriklai itaweka lini utaratibu wa kufanya taasisi hizo ziwe za kisheria ili hata wake wa marais wanapomaliza muda wao wapokezane vijiti kana urais unavyofanywa.
Waziri Muchika akifafanua kuhusu swali hilo alisema ni kweli zipo taasisi zinazoendeshwa wake za marais .Hivyo taasisi hizo hufanya shughuli zake kama zilivyo taasisi nyingine zisizo za kiserikali. Ipo taasisi ya WAMA iliyoanzishwa na Mke wa Rais wa Awamu ya Nne Mama Salma Kikwete na EOTF iliyoanzishwa na Mke wa Rais wa Awamu ya Tatu , Mama Anna Mkapa
Aliongeza kuwa kama zilivyo taasisi zingine za hiari na zisizo za kiserikali (NGO,S). Taasisi hizo ziliundwa kutegemea na jinsi Mke wa Rais navyopenda kujishughulisha na shughuli za kijamii.
Alisema inawezekana kabisa akatokea Mke au Mme wa Rais ambaye hana utashi au mapenzi ya kujishughulisha na shughuli za kijamii. Hivyo kutokana na mazingira hayo serikali haioni sababu za kuweka utaratibu wa kufanya taasisi hizo ziwe za kisheria ili wake / waume za marais wanapomaliza muda wao wapokezane vijiti.
Aliongeza kuwa kwa kufanya hivyo tutakuwa tunawalazimisha kufanya shughuli wasizo na utashi nazo.
Akijibu swali la nyongeza la Leticia liliouliza kuwa Watanzania wananufaikaje na taasisi hizo bila tofauti za kiitikadi. Waziri Mkuchika alisema hakuna anayefanya kazi kwa kubagua na alizipongeza taasisi hizo kwa kufanya kazi mijini na vijijini huku akiwataka Watanzania kuanzisha taasisi mijini na vijijini .
Alisema jumla ya wanafunzi 939 wamenufaika kielimu kupitia (WAMA). Pia WAMA imetoa msaada wa vitanda na magodoro katika wodi za wakina mama na imetoa kiasi cha fedha sh. milioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wanawake ya MEWATA, ambazo ni msaada kutoka Taasisi ya Nakayama, Japan.
Aidha alisema ina mpango wa kutoa vifaa vya hospitali vyenye thamani y a dola za Marekani milioni tatu kupitia msaada wa Project Care, Marekani vinavyotarajia kuingia nchini.
Alisema taasisi ya EOTF imetoa mafunzo kwa wajasiliamali mbalimbali.
Mwisho.

Aug 11, 2012

HATIMAYE NYENYEMBE AREJEA KUVAA VIATU VYAKE KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MBEYA

Mwenyekiti mpya wa Mbeya Press Club aliye simama ndugu Christopher Nyanyembe akitoa Shukrani zake
Ilikuwa ni mapema baada ya uchaguzi ambapo kiongozi mpya Christopher Nyanyembe alipongezana na mpinzani wake, kiongozi huyo mpya ameshinda kwa kura 27

 Waandishi wa habari wakiwapongeza viongozi wapya
Hii Ndio kamati kuu Iliyo chaguliwa katika kuendesha Klabu ya waandishi Mbeya, akiwemo mwandishi mkuu wa Mbeya yetu Ndugu Joseph Mwaisango wa Kwanza kulia kwa walio simama.

KUTOKA MBEYA YETU BLOG

Aug 10, 2012

MKUTANO MKUU WA MBEYA PRESS CLUB WAENDELEA KYELA

Mwenyekiti wa Mbeya press club Christopher Nyenyembe akizungumza kwenye mkutano mkuu ulioketi wilayani Kyela ambapo wadau wa sekta ya habari wameshiriki kupima na kutathmini maendeleo ya sekta hiyo mkoani mbeya
Mwenykiti wa Halmashauri ya wilaya yaKyela akifungua mkutano huo

Beyonce and Jay Z Named World's Highest-Paid Celebrity Couples

Forbes Magazine just named Jay and Bey the highest paid celebrity couple in the world. Together they made $78 million - from May 2011 to May 2012. Beyonce - $40m, Jay Z - $38m. And Beyonce took a break for most of the year. Na wa o! :-)



 From Forbes Magazine,

Take Beyonce Knowles and Jay-Z, for example. Last year’s runners-up on the list of The World’s Highest-Paid Celebrity Couples, the duo has now climbed one spot to top this year’s ranking. Knowles, who took a break from her hectic touring schedule in 2011 to give birth to daughter Blue Ivy Carter, still collects big paychecks from old hits. Besides, the singer’s new album went platinum in the U.S., not to mention her non-musical ventures and endorsement deals, which all helped to bring her total earnings between May 1, 2011 and May 1, 2012 to $40 million, according to data from the latest Celebrity 100 list.
And as the male half of music’s first couple, Jay-Z isn’t far behind his wife. The hip-hop mogul made millions from Watch the Throne, his musical collaboration with pal Kanye West, and even more from the tour that followed. Add to that a bevy of non-musical enterprises such as ad firm Translation and cosmetics company Carol’s Daughter and the result is a staggering $38 million that he has brought home in twelve months, putting the couple’s annual income at $78 million.

Dear lord, what happened to Naomi Campbell's hair?

 
This is a clear example of what happens when we women keep wearing weaves over an extended period of time. But some of us can't just do without our weaves..

SEKRETARIETI YA AJIRA YATANGAZA RATIBA YA USAILI MWEZI HUU


Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Bw. Xavier Daudi akifafanua jambo kwa Waandishi wa habari (hawapo pichani) na kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Sekretarieti ya Ajira, Bw. Bakari Mahiza.

Sekretarieti ya Ajira imetangaza ratiba ya usaili kwa mwezi Agosti, 2012 kwa waombaji nafasi za kazi katika Taasisi za Umma kwa wale waliokidhi vigezo. Tangazo hilo limetolewa leo na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Bw. Xavier Daudi alipokuwa akiongea na Waandishi wa habari ofisi kwake.
Daudi amesema usaili huo utafanyika katika Mikoa sita ambayo ni Dodoma, Morogoro, Manyara, Arusha, Dar es Salaam na mkoa wa Pwani.
Amesema usaili umeanza tarehe 6 hadi 7 Agosti, mwaka huu kwa mkoa wa Manyara, wilaya ya Babati kwa nafasi za Mtendaji wa Kata, Kijiji na Madereva, ilihali kwa mkoa wa Dodoma umeanza tarehe 7-9 Agosti, 2012 katika Chuo cha Serikali za Mitaa, Hombolo kwa nafasi Wahadhiri wasaidizi, Afisa Utumishi, Afisa Tawala, Watunza kumbukumbu, Madereva na Wasaidizi wa Ofisi.
Aidha, usaili utafanyika pia katika Chuo cha Mipango Dodoma (IRDP) kuanzia tarehe 10-14 mwezi huu kwa kada za Afisa Ugavi, Afisa Utumishi, Mkutubi na Afisa Mitaala. Wakati katika Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Biashara (COASCO) utaanza tarehe 15-16 Agosti kwa kada za Wakaguzi wa hesabu wa ndani, Wakaguzi Wasaidizi wa hesabu wa ndani na nafasi ya Katibu Mahususi.
“Kwa mkoa wa Morogoro usaili utafanyika tarehe 15-16 mwezi huu katika Taasisi ya Tanzania Official Seed Certification Institute (TOSCI) kwa kada za Wakaguzi Wasaidizi wa hesabu wa ndani, Afisa Kilimo, na kwa Katibu Mahususi”. Alisema Daudi.
Ameongeza kuwa kwa mkoa wa Arusha usaili utafanyika tarehe 10-11 Agosti katika Tume ya Mionzi Tanzania (TAEC) kwa nafasi za Wataalamu wa Mionzi, Fizikia, Uhasibu, Ukatibu Mahususi, Msaidizi wa Ofisi na Ulinzi. Aidha, usaili utaendelea katika mkoa wa Pwani, wilaya ya Bagamoyo katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA) kwa nafasi ya Mkufunzi na Mkufunzi Msaidizi daraja la kwanza na la pili.
Katibu amesema usaili huo utamalizikia kwa mkoa wa Dar es Salaam ambao unatarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 23 hadi 31 Agosti kwa awamu hii ambao utakuwa kwa Vyuo vya elimu ya juu ikiwemo Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na Chuo cha Biashara (CBE). Aidha, utafanyika pia katika Taasisi ya Utafiti wa Samaki Tanzania (TAFIRI) na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) ambao utahusisha nafasi za Wakufunzi, Afisa Utumishi, Afisa Mitaala, Afisa Viwango, Madereva na Katibu Mahususi.
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira amesema nia ya kufanya usaili katika mikoa husika kwanza ni kufikisha huduma karibu na wateja wetu na pia kuwapunguzia gharama za kusafiri mbali na eneo alilokuwa ameomba kazi husika. Aliongeza kuwa ili kupata maelezo zaidi juu ya usaili huo ni vyema wakatembelea tovuti ya Sekretarieti ya Ajira ambayo ni www.ajira.go.tz ili kupata ufafanuzi zaidi.


U.N. cautions enemies of the Somali peace process

The United Nations Security Council has warned al-Shebab militants against trying to impede the peace process in Somalia. (AFP)
The United Nations Security Council has warned al-Shebab militants against trying to impede the peace process in Somalia. (AFP)

By AFP,UNITED NATIONS

The United Nations Security Council warned al-Qaeda-linked al-Shebab rebels on Thursday against trying to impede the peace process in Somalia.

The 15 council members hailed the adoption of a new provisional constitution earlier this month by the Somali National Constituent Assembly, saying it marked an “important milestone” in the eastern African nation’s transition toward “more stable and accountable governance.”

“The members of the Security Council strongly condemn ongoing attempts, including by the Shebab, to undermine the transition process,” they said in a statement.

“They recall in this regard the Security Council’s willingness to take measures against both internal and external actors engaged in actions aimed at undermining the peace and reconciliation process.”
The council members called for new members of parliament to be chosen “as quickly as possible, and in a transparent manner,” stressing that the lawmakers should be picked “without fear of violence or intimidation.”

The UN’s special representative to Somalia, Augustine Mahiga, has reported instances of bribes and intimidation in the designation process for new members of parliament.

Aug 9, 2012

ROLI LASHINDWA KUPANDA MLIMA NA KUFUNGA BARABARA MBOZI

Kreti za soda zikiwa zimemwagika barabarani  baada ya kupinduka kwa roli mali ya Kanji lanji ambalo lilikuwa limebeba creti 1800

Hilo ndilo roli lililokata njia  likionekana kwa mbali

Huu ndiyo msururu wa magari kwa upande mmoja wa barabara

BIBI HUYU AKIWA KWENYE FOLENI YA KUCHUKUA SODA


ABIRIA WANAOTUMIA BARABARA YA MBEYA –TUNDUMA LEO WAMEONJA ADHA YA BARABARANI BAADA YA GARI LA MIZIGO LILILOBEBA MASANDUKU YA SODA KUPINDUKA NA KUFUNGA BARABARA HADI  JIONI HII .
GARI HILO LENYE NAMBA ZA  USAJI T 788 AEY MALI YA KAMPUNI YA KANJI LALJI YA MBEYA, LILIKUWA LIKIPELEKA SODA MKOANI RUKWA AMBAPO KUTOKANA NA UZITO WA MZIGO LILIOBEBA LILISHINDWA KUPANDA MLIMA WA SENJELE NA DEREVA KUAMUA KUOKOA UHAI WAKE KWA KUKATA NJIA.

BAADA YA TUKIO HILO ABIRIA WALIOKUWA KWENYE MABASI YANAYOTUMIA BARABARA HIYO WAKAFANYA SHEREHE YA KUNYWA NA KUSAZAA SODA HIZO BILA KUJALI TAHADHARI ILIYOKUWA IKITOLEWA NA MMOJA WA WAHUSIKA KWENYE ROLI HILO ALIYEJITAMBULISHA KAMA DEREVA WA GARI LILIPATA AJALI PETER NAMLAZAR

HATA HIVYO WATU WALIENDELEA KUCHANGAMKIA SODA HIZO LICHA YA ULINZI WA POLISI KUWEPO ENEO HILO.

LICHA YA KUTOKUTOKEA MAAFA YEYOTE KWA WALIO KUWEMO KWENYE GARI HILO, UNYWAJI OVYO WA SODA ZILIZOANGUKA ENEO HILO LIMETAJWA KUWA NI HATARI KWA MAISHA HASA KUTOKANA NA VIPANDE VYA CHUPA KUCHANGANYIKA NA SODA HIZO

Aug 5, 2012

WAZEE WATAKA KIPAUMBELE KWENYE HAMASA YA SENSA

Mratibu wa sensa wilaya ya Mbozi Eliud Mwakibombaki akizungumza kwenye uzinduzi huo

Baashi ya watu waliohudhulia uzinduzi huo

Mzee Mdalavuma akifuatiwa na Mkuu wa wilaya wakiwa meza kuu

Dr Michael Kadeghe Mkuu wa wilaya ya Mbozi akiwahamasisha wananchi kushiriki kwenye zoezi la sensa

Kikundi cha Ngoma cha Ndili miongoni mwa vikundi vilivyoshiriki kwenye zoezi la uzinduzi wa kampeni ya hamasa  ya sensa jioni ya leo uwanja wa kituo cha mabasi cha Mlowo


Na Danny Tweve  

BAADHI YA WAZEE WILAYANI MBOZI WAMEPENDEKEZA KUSHIRIKISHWA WAKATI WA UHAMASISHAJI WA ZOEZI LA  SENSA KUTOKANA NA UKWELI KWAMBA BADO KUNA IMANI  NA MILA POTOFU KWA JAMII WILAYANI HUMO , HASA  INAPOFIKIA HATUA YA KUHESABU WATOTO KUWA NI UCHURO KWA KAYA ZAO.

AKIZUNGUMZA KWENYE UZINDUZI WA KAMPENI KWAAJILI YA HAMASA YA SENSA WILAYANI HUMO, MWENYEKITI WA CCM WILAYA MBOZI MZEE ALOYCE MDALAVUMA, AMESEMA NJIA PEKEE NI KWA WAZEE MAARUFU KUTUMIKA HASA MAENEO YA VIJIJINI KATIKA KUTOA UFAFANUZI JUU YA UMUHIMU WA ZOEZI HILO ILI KUPATA MWITIKIO MKUBWA NA KUWEZESHA MAFANIKO YA JUU YA ZOEZI LA SENSA

AMESEMA KWA JAMII YA WANYIHA KUHESABU WATOTO KATIKA HALI YA KAWAIDA HAIKUBALIKI, LAKINI KWAKUWA ZOEZI LA SENSA LINAFAHAMIKA VYEMA UMUHIMU WAKE NI VYEMA WANANCHI NA HASA WAZEE WAKAHAMASISHWA KUSHIRIKI VYEMA KWENYE UHESABUJI  ILI KUWEZESHA UPATIKANAJI WA TAKWIMU SAHIHI

KWA UPANDE WAKE MZEE BENNY MWANG’AMBA AMESEMA KUNA HAJA KWA VIONGOZI WA DINI WILAYANI HUMO KUTUMIA VITABU VITAKATIFU IKIWEMO BIBLIA AMBAPO KUNA ENEO INAZUNGUMZIA MAJIRA AMBAYO YESU ALIZALIWA ULIKUWA WAKATI WA SENSA YA WATU NA KWAMBA NJIA HIZO ZITAWEZESHA WATU KUFUNGUKA NA KUACHA USIRI KWENYE TAARIFA ZA FAMILIA ZAO

MAPEMA KATIKA TAARIFA YAKE MRATIBU WA SENSA WILAYA YA MBOZI BWANA ELIUD MWAKIBOMBAKI AMESEMA WILAYA YA MBOZI IMETEUA JUMLA YA MAKARANI 1471 WATAKAOSIMAMIA MAENEO YA UHESABUJI 230 AMBAPO MIONGONI MWAKE MAKARANI  460 WATAJIELEKEZA KATIKA DODOSO REFU

AMESEMA KATIKA MAANDALIZI YA ZOEZI HILO MAFUNZO YA WAHESABUJI YANATARAJIWA KUANZA JULAI TISA KATIKA VITUO VINNE VYA VWAWA, IGAMBA, ITAKA NA MAHENJE AMBAPO WAKUFUNZI WAMESHATENGWA KWA MAENEO HAYO ILI KUFANYA MAANDALIZI YATAKAYOFANIKISHA ZOEZI HILO
AKIZINDUA ZOEZI HILO KWA KUPIGA KING’ORA MKUU WA WILAYA YA MBOZI DR MICHAEL KADEGHE AMESEMA , PAMOJA NA KUANZISHA MASHINDANO YATAKAYOBEBA UJUMBE WA SENSA KUANZIA NGAZI YA KIJIJI PIA WILAYA IMEJIPANGA KUHAKIKISHA KUWA ZOEZI HILO LINAFANIKIWA NA HASA MAENEO YA VIJIJINI

DK KADEGE AMESEMA KATIKA KUFANIKISHA ZOEZI HILO WILAYA IMESHATUMA TIMU YA UHAMASISHAJI AMBAPO PAMOJA NA MAMBO MENGINE TIMU HIYO INAPOKEA CHANGAMOTO NA MAPENDEKEZO YA KUFANIKISHA ZOEZI HILO KUTOKA KWA VIONGOZI WANGAZI ZA JUU NA WALE WA JAMII ILI HATIMAYE WAKATI WA UTEKELEZAJI ZOEZI HILO LIWEZE KUWA LA MAFANIKIO

Aug 4, 2012

Complete Baby Care Instructions for New Parents Video

: Complete Baby Care teaches new mothers how to care for their baby.

Mbunge wa Monduli(CCM)Atoa Katoni Za Tende na Jozi 100 Za Kanzu Kwa Ajili ya Waislam wa Monduli

Mh
Lowassa akimkabidhi sheikh Simba sehemu ya tende hizo.Wengine pichani
kushoto ni Sheikh wa Mto wa Mbu Sheikh Nasib Idd Nasib Mnyema Kkatibu wa
Bakwata wilaya ya Monduli Idd Idoya na Ustadh Swalehe Ramadhan .
Waziri
Mkuu aliyejiuzulu na Mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa, ametoa
katoni kadhaa za tende pamoja na jozi 100 za kanzu kwa ajili ya Waislam
wa Monduli.Akipokea msaada huo, sheikh wa wilaya ya Monduli Sheikh
 Mwinshehe Mwinyimgeni Salum Simba, alimshukuru mh Lowassa kwa utaratibu
wake huo ambao amekuwa akiufanya kila mfungo wa mwezi mtukufu wa
Ramadhan kwa Waislam wa Monduli.

kutoka swahili villa

KATIBU WA CCM TAWI LA NORTH LONDON NEEMA KUMBA AJITOSA UCHAGUZI UVCCM, TAIFA

 KADA  wa  Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia umoja wa vijana wa CCM
(UVCCM) na Msomi wa  digrii ya uchumi, Neema Kumba
Neema akikabidhiwa fomu jana na Sophia Duma Makao Makuu ya UVCCM jijini Dar es Salaam .
--
DAR ES SALAAM, TANZANIA

KADA  wa  Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia umoja wa vijana wa CCM
(UVCCM) na Msomi wa  digrii ya uchumi, Neema Kumba, amejitosa kwenye
uchaguzi mkuu wa umoja huo Taifa kwa kuchukua kugombea nafasi ya NEC na
uwakilishi UWT.



Akizungumza na waandishi wa habari mapema jana, Agosti 3, jijini Dar es
Salaam, muda mfupi baada ya kukabidhiwa fomu hiyo na Mkuu wa Idara ya
Oganizesheni na siasa UVCCM, Taifa, Sophia Duma,




Kumba ambae awali alikua Katibu wa CCM, tawi la North London, Nchini
Uingereza, alipokua akichukulia digrii yake ya uchumi, alisema lengo ni
kuakikisha mikakati thabiti  inajengeka kwa  kiwango kikubwa miongoni
mwa vjana na wanawake wote nchini.




“Kwa umakini wangu na maarifa niliyoyapata kwenye elimu na uwepo wangu
ndani ya chama, ndani na nje ya nchi, ni wakati sasa na mimi kuwasaidia
wenzangu hasa Vijana na wanawake ambao mara nyingi wamekua wakisahauriwa
 na huu ndio wakati wa kuwainua” alisema Kumba.




Mbali na kuchukua fomu hiyo ya NEC na uwakilishi UWT, Taifa, pia tayari
alisha chukua fomu ya kuwania nafasi ya Mwenyekiti Uvccm, Wilaya Ilala.




Mpaka sasa tayari wanachama mbalimbali wa UVCCM, wamejitokeza kuchukua
fomu za kuwania uongozi ambapo mwisho wa kurudisha fomu hizo, Agosti 6.

Gazeti la NIPASHE: Magufuli amtega Meya wa Arusha hoja ya Lema

Gazet
Hoja ya kukiondoa kituo kikuu cha mabasi katikati ya jiji ambayo ilitumiwa na aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) kujinadi katika kampeni zake za uchaguzi mkuu ulipita, sasa ametwishwa Meya wa Jiji Gaudence Lyimo (CCM).

Aliyemtwisha zigo hilo ni Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli na alifanya hivyo wakati akifungua mkutano wa wadau wakuu wa Mfuko wa Bodi ya Barabara uliofanyika jijini hapa juzi.

Magufuli alikuwa akizungumzia mikakati ya kuondoa foleni inayoanza kulinyemelea jiji la Arusha ambapo alisema moja ya ufumbuzi ni kuihamisha stendi hiyo ya mabasi.

“Ni vizuri Meya upo hapa, wekeni mikakati ya kuhamisha ile stendi, hakuna haja ya mabasi yote yanayokuja Arusha lazima yaingie katikati ya jiji,” alisema na kuongeza, “tena katika jiji hili mnaweza kuwa na stendi tatu za mabasi makubwa katika maeneo tofauti kulingana na mahitaji.”

Alitaja maeneo hayo ambayo ni nje ya jiji kuwa ni kwa mabasi yanayotokea barabara ya Moshi, yanayotokea Dodoma na Babati na stendi nyingine ni kwa mabasi yanayotokea barabara ya Namanga.


Hoja ya kuhamisha stendi ilikuwa ni moja ya ajenda katika mikutano ya kujinadi kuwania ubunge wa Arusha Mjini iliyokuwa ikihubiriwa na Lema ambaye pamoja na stendi pia alizungumzia azma yake ya kuhamisha soko kuu lililopo katikati ya jiji.

Hata hivyo, Lema hakufanikiwa kutimiza azma yake baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, kumvua ubunge mapema Aprili, mwaka huu, baada ya mahakama kuridhika kwamba alitumia lugha ya kashfa dhidi ya aliyekuwa mgombea kwa tiketi ya CCM, Dk. Batilda Burian.

Lema amekata rufaa kupinga hukumu hiyo na kesi bado haijapangiwa tarehe ya kusikilizwa.

Katika hatua nyingine Magufuli alisema wizara yake itahakikisha ujenzi wa barabara itakayounganisha kati ya barabara ya Arusha – Babati na Arusha – Namanga inajengwa na kukamilika ili magari yatokayo maeneo ya Babati kwenda Namanga na kinyume chake yasilazimike kupita katikati ya mji.

Alisema hayo wakati akijibu maelezo ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, ‘aliyemchomekea’ ombi hilo katika maelezo yake ya awali kabla waziri huyo hajafungua mkutano huo.

“Najua Mkuu wa Mkoa Mulongo ‘amenichomekea’ ujenzi wa barabara hii ili kuhakikisha magari yatokayo Babati kwenda Namanga na kurudi yasilazimike kupita mjini ili kupunguza foleni…nasema wizara itasaidia ujenzi huo ili ikamilike,” alisema.

Chanzo Nipashe

Aug 2, 2012

KULIPIA FIRE SASA TRA


Kuna taarifa ambayo ilitolewa na imetangazwa kwenye vyombo vya habari kuhusu ulipaji wa kodi ya FIRE na ROAD LICENCE,tangazo hilo linawataarifu wamiliki wote wa vyombo vya moto wanapokwenda kulipia kodi yao ya mwaka ya Road Licence watakakiwa pia kulipia na kodi ya FIRE ambayo mwanzoni haikua inalipiwa hapo TRA 

  KUANZIA JULY 2012 HUDUMA ZA FIRE ZITAKUWA ZINALIPIWA TRA WAKATI WA KU-RENEW NA BEI NI;
CC 1 - CC 500 10,000/=

CC 501 - CC 1500 20,000/=

CC 1501 - CC 2500 30,000/=

CC 2501 na kuendelea 40,000/=

BARAZA LA MADIWANI MBOZI KUKETI IJUMAAM

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya  wilaya ya Mbozi Levison Chilewa akizungumza wiki iliyopita baada ya baraza hilo kuahirishwa

Waheshimiwa madiwani wakiwa ukumbini kabla ya baraza la wiki iliyopita kuahirishwa

Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya Bi Mtunguja akisikiliza maelezo ya Mkuu wa mkoa, anayemfuatia ni Mbunge wa Mbozi mashariki Mh Zambi

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Kandoro akiwanyoshea vidole madiwani katika moja ya maeneo aliyoyasisitiza kuhusiana na kujibu hoja za mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali

Aug 1, 2012

ASKARI TRAFIKI AFARIKI KATIKA AJALI YA ROLI JIONI HII

 ASKARI POLISI WA KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI ANAYEFAHAMIKA KWA JINA LA JOSEPH AMEFARIKI DUNIA KWENYE AJALI YA ROLI ILIYOTOKEA JIONI HII KATIKA ENEO LA SENJELE WILAYANI MBOZI BAADA YA GARI HILO KUHARIBIKA MFUMO WA BREKI LIKIWA MTELELEMKONI NA KUMLAZIMU DEREVA WA GARI HILO KURUKA

INAELEZWA KUWA ASKARI HUYO ALIKUWA AMEOMBA LIFT KWENDA MJINI MBEYA AKITOKEA KITUO CHAKE CHA KAZI ENEO LA MLOWO WILAYANI MBOZI AMBAPO AKIWA NJIANI NDIPO AKAKUMBWA NA MASAIBU HAYO



PICHA ZOTE NA INDABA BLOG