Adverts

Oct 8, 2012

MPISHI MAARUFU KUTOKA INDIA ATIA TIMU BONGO NA KUTOA SOMO

Mpishi maarufu Duniani kutoka nchini India Sanjeev  Kapoor (kulia) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam jinsi vyakula vya asili vinavyoweza kuwavutia watalii kwenda kutembelea nchi mbalimbali na hivyo kukuza utalii wa nchi husika huku Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Nchini Dkt. Aloyce Nzuki akimsikilia kwa makini. Mpishi Kapoor amekuja nchini kwa ajili ya kuandaa vipindi vya runinga ambavyo vitahusu mapishi ya vyakula vya  asili ili kutangaza utalii wa kiutamaduni nchini India.


Mpishi maarufu Duniani kutoka nchini India Sanjeev  Kapoor (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Nchini Dkt. Aloyce Nzuki leo jijini Dar es Salaam kitabu kinachoonyesha aina mbalimbali za mapishi alizoziandaa katika kipindi cha mapishi kijulikanacho kama Khana Khazana kinachorushwa na Televisheni ya Taifa ya India.  Mpishi Kapoor atakuwepo nchini kwa muda wa wiki mbili kwa ajili ya kuandaa vipindi vya runinga ambavyo vitahusu mapishi ya vyakula vya  asili ili kutangaza utalii wa kiutamaduni nchini India. 

Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Nchini Dkt. Aloyce Nzuki akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kitabu alichopewa na mpishi maarufu Duniani kutoka nchini India Sanjeev  Kapoor  kinachoonyesha aina mbalimbali za mapishi alizoziandaa katika kipindi cha mapishi kijulikanacho kama Khana Khazana kinachorushwa na Televisheni ya Taifa ya India. Mpishi Kapoor atakuwepo nchini kwa muda wa wiki mbili kwa ajili ya kuandaa vipindi vya runinga ambavyo vitahusu mapishi ya vyakula vya  asili ili kutangaza utalii wa kiutamaduni nchini India. 


Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Nchini Dkt. Aloyce Nzuki (kushoto) akimkaribisha mpishi maarufu Duniani kutoka nchini India Sanjeev  Kapoor ili aweze kuongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es salaam ili aweze kuongea nao kuhusu umuhimu wa vyakula vya asili katika sekta ya utalii wa utamaduni. Kulia ni Naibu Meneja Mkuu wa Hoteli ya Serena Daniel Sambai ambayo imegharamia gharama za  chakula na maladhi kwa mpishi huyo kwa kipindi chote  atakachokuwepo nchini. 
Picha na Anna Nkinda - Maelezo