Adverts

Nov 14, 2012

MGAMBO KUKABA NAFASI ZA RAIA KWENYE MAKAMPUNI YA ULINZI


Na  Magreth Sikambale

Mafunzo ya awali ya Mgambo yaliyodumu kwa kipindi cha miezi mitatu yakishirikisha vijana 80 kutoka kata za Iyula na Ruanda wilayani Mbozi ,yamefungwa rasmi leo na Ruteni kanali Emanuel Mwikuka.
Akifunga mafunzo hayo, Kanali Mwikuka ametoa wito kwa vijana nchini  kujtokeza na kushiriki  katika mafunzo hayo ili kuimarisha ulinzi na usalama wa Taifa na wanchi wenzao  ujumla.
Alisema hayo wakati akijibu risala ya washiriki hao iliyoeleza kuwa vijana wengi wamekua wakikwepa kujiunga na mafunzo hayo kwa dhana kuwa mafunzo hayo ni mateso na hayana umuhimu kwao.
Kanali Mwikuka amesema,  mafunzo hayo hayataishia hapo bali kutakuwepo kozi nyingine kwa wale walio fuzu.
Ameongeza kuwa lengo la kuweka msukumo kwenye  mafunzo hayo ni kwa ajili ya kuimarisha ulinzi, na kwamba  jeshi lina mpango wa kuondoa wananchi walio ajiliwa katika sekta ya ulinzi  ambao hawajafuzu mafunzo ya Mgambo  na badala yake nafasi zao zitachukuliwa na waliohitimu mafunzo ya mgambo.
“vijana  mtakuwa na  nafasi kubwa yakupata ajira katika ngazi za Serikali na Sekta binafsi” aliongeza Kanali Mwikuka.
Sambamba na hayo pia aliweza kuwatunuku vyeti washiriki wa 5 waliyofanya vizuri katika mafunzo hayo Rebeka Mbembela, Jonas Mgala, Musa Mgala, Heneriko Shonde, na mwile Stanlesi.
Katika risala iliyosomwa na Elia Japhet, wahitimu hao walieleza kuwa mafunzo yao yalianza mwezi Julai mwaka huu na kwamba walianza mafunzo hayo ni 120 hata hivyo kutokana na sababu mbalimbali washiriki 40 waliishia njiani.
Mbali na hayo  taarifa fupi  ilisomwa na mshauri wa mgambo wa wilaya ambapo amesema vijana hao wameweza kujifunza mambo muhimu yanayotakiwa kufundishwa katika mafunzo ikiwemo elimu juu ya rushwa toka Takukuru, ulinzi na usalama wa  nchi.

Katika Maadhimisho hayo Kanali Mwikuka pia alikagua gwaride la wahitimu wa mgambo kabla ya kuwatunuku zawadi washindi mbalimbali.