Adverts

Nov 14, 2012

MGAMBO KUKABA NAFASI ZA RAIA KWENYE MAKAMPUNI YA ULINZI


Na  Magreth Sikambale

Mafunzo ya awali ya Mgambo yaliyodumu kwa kipindi cha miezi mitatu yakishirikisha vijana 80 kutoka kata za Iyula na Ruanda wilayani Mbozi ,yamefungwa rasmi leo na Ruteni kanali Emanuel Mwikuka.
Akifunga mafunzo hayo, Kanali Mwikuka ametoa wito kwa vijana nchini  kujtokeza na kushiriki  katika mafunzo hayo ili kuimarisha ulinzi na usalama wa Taifa na wanchi wenzao  ujumla.
Alisema hayo wakati akijibu risala ya washiriki hao iliyoeleza kuwa vijana wengi wamekua wakikwepa kujiunga na mafunzo hayo kwa dhana kuwa mafunzo hayo ni mateso na hayana umuhimu kwao.
Kanali Mwikuka amesema,  mafunzo hayo hayataishia hapo bali kutakuwepo kozi nyingine kwa wale walio fuzu.
Ameongeza kuwa lengo la kuweka msukumo kwenye  mafunzo hayo ni kwa ajili ya kuimarisha ulinzi, na kwamba  jeshi lina mpango wa kuondoa wananchi walio ajiliwa katika sekta ya ulinzi  ambao hawajafuzu mafunzo ya Mgambo  na badala yake nafasi zao zitachukuliwa na waliohitimu mafunzo ya mgambo.
“vijana  mtakuwa na  nafasi kubwa yakupata ajira katika ngazi za Serikali na Sekta binafsi” aliongeza Kanali Mwikuka.
Sambamba na hayo pia aliweza kuwatunuku vyeti washiriki wa 5 waliyofanya vizuri katika mafunzo hayo Rebeka Mbembela, Jonas Mgala, Musa Mgala, Heneriko Shonde, na mwile Stanlesi.
Katika risala iliyosomwa na Elia Japhet, wahitimu hao walieleza kuwa mafunzo yao yalianza mwezi Julai mwaka huu na kwamba walianza mafunzo hayo ni 120 hata hivyo kutokana na sababu mbalimbali washiriki 40 waliishia njiani.
Mbali na hayo  taarifa fupi  ilisomwa na mshauri wa mgambo wa wilaya ambapo amesema vijana hao wameweza kujifunza mambo muhimu yanayotakiwa kufundishwa katika mafunzo ikiwemo elimu juu ya rushwa toka Takukuru, ulinzi na usalama wa  nchi.

Katika Maadhimisho hayo Kanali Mwikuka pia alikagua gwaride la wahitimu wa mgambo kabla ya kuwatunuku zawadi washindi mbalimbali.


MAFUNZO YA MGAMBO MBOZI YAFIKIA UKINGONI w


Kanali Emanuel Mwikuka  ambaye alimwakilisha Mshauri wa mgambo mkoa

Add caption

Mgambo wakila kiapo mbele ya mgeni rasmi

Gwaride la Mgambo katika maonyesho ya kugfunga mafunzo tarafa ya Iyula


Wakipita kutoa heshima mbele ya mgeni rasmi, hii ni staili ya SOOOOSI UP SOOOS UP

Hapa wakiwa kwenye hatua za awali za Paredi

Askari wa Mgambo wakionyesha uwezo wao katika kukamili matukio mbalimbali ya kivita

Wahitimu wa mafunzo ya Mgambo wakiwa kwenye maonyesho ya medani za kivita




PICHA NA CHARLES SHITINDI

Nov 11, 2012

Msaidizi wa askofu wa KKKT Dayosisi ya Konde Mchungaji Geofrey Mwakihaba akitamka neno la baraka kabla ya kuuweka mche wa mparachihi  kwenye shimo tayari kuupanda ikiwa ni hatua ya kuzingua program ya sharika, majimbo na taasisi za Kilutheri kwenye Dayosisi hiyo katika upandaji wa miti kama sehemu ya hifadhi ya mazingira.


Msaidizi wa askofu  mchungaji Mwakihaba akipanda mche wa mparachichi kwenye kituo cha watoto kinachoendelea kujengwa kwenye usharika wa Vwawa

Mkuu wa Jimbo la Magharibi Mch. Mwambola akizungumzia uendelezaji wa program ya hifadhi mazingira kwenye sharika za jimbo hilo


Mwanafunzi wa  kipaimara  akipanda mti kama sehemu ya uzinduzi wa zoezi la upandaji miti Makanisani na kwa waumini lililoanza msimu huu kwa KKKT dayosisi ya Konde

Pia familia ya Danny Tweve imeshiriki kwenye ibada  hiyo ikikumbuka miaka minne iliyopita ambapo Mch Mwakihaba ambaye alifungisha ndoa hiyo hapakuwa na matunda haya kwa mtoto wa kiume  na aliyebebwa 


Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Dayosisi ya Konde, imetoa maelekezo kwenye majimbo na sharika zake kujielekeza katika utekelezaji wa mipango ya kuhifadhi mazingira ili kuepusha  madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na kushindwa kutawala vyema mazingira kwenye maeneo yao.
Akizungumza kwenye ibada ya Kipaimara  katika usharika wa  Vwawa wilayani Mbozi Msaidizi wa Askofu Mch. GEOFREY MWAKIHABA amesema utaratibu uliobuniwa na uongozi wa jimbo la Magharibi utasaidia kuwakumbusha waumini na wananchi kwa ujumla juu ya uhifadhi wa mazingira
Amesema jimbo hilo limeanzisha utaratibu wa kupanda miti kila msimu wa mvua unapoanza na kwamba kanisa linatumia fulsa ya ibada maalumu kama za kipaimara na ubatizo kwenye nyakati hizo kuzindua kampeni za upandaji miti  kama kanisa, na waumini wake.
Amefafanua kuwa hatua hiyo pia itasaidia watoto kujihusisha zaidi na shughuli za kutunza mazingira kutokana na kuandaliwa katika malezi yao wakijua umuhimu wa raslimali rafiki za mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji na uhifadhi wake