Adverts

Jan 26, 2013

NDEGE YA ASILI KUTOKA MWANZA KWENDA MBEYA ILIPOGOMA KUENDELEA NA SAFARI

Inaelezwa kuwa sababu ya Ungo uliokuwa ukiendeshwa na kijana mmoja kati ya wawili waliokuwa wakiwahi kwenye msiba wa mama yao huko Mbeya, wakitokea mkoani Mwanza, ilishindwa kuendelea katika mji wa Singida baada ya kijana lena (asiyefahamu) vyema matumizi ya chombo hicho kukiuka masharti kwa kugeuka nyuma na matokeo yake chombo kushindwa kwenda mbele na kutua ghafla.

Kulingana na habari zilizokuwa hewani ITV jana wakati wakihojiwa vijana hao walieleza kuwa walikuwa safarini kutoka Mwanza kwenda mbeya na wangetumia muda wa saa moja mpaka mbeya na kuwahi msiba wa mama yao mpendwa

Kwa bahati mbaya mdogo mtu alikosea masharti kutokana na ugeni wake katika kutumia chombo hicho ambapo aligeuka nyuma kama alivyofanya mke wa Ruth kwenye biblia ambaye aligeuka nyuma na kutamani mambo ya sodoma na hatimaye kugeuka na kuwa jiwe la chumvi

Sasa dogo labda kwa kuhofia chombo kinavyovuma aliamua kugeua na kuchungulia kukokoni na ndipo hapo biashara ikawakata na kutua ghafla katika mji wa singida majira ya saa tisa usiku, ambapo walikamatwa na maafande waliokuwa patrol wakidhani vibaka, lakini katika mahojiano vijana wakaweka wazi teknolojia ya kusafiri kwa njia ya ungo

Ungo huwa na Tenki la Mafuta ambayo 'wajuvi' wanasema ni damu za watu.Kichupa hapo pembeni ndio tenki lenyewe!!



Hawa mashine zilizhemsha wakiwa angani huko Mwanza 'nadhani Radiator ilishindwa kufanya kazi vizuri' nyungo zikachemshaau mafuta yaliisha

  Udadisi umebaini kuwa ungo wa wachawi hutumia mafuta ambayo ni damu ya binaadamu.Huu ulishindwa kusafiri huko Mtwara.Tenki la Mafuta katika ungo huu ni kubwa...huenda huu una turbo kabisa!!!
picha na mwanza yetu blog