Adverts

May 1, 2013

MEI MOSI UWANJA WA SOKOINE, KUMEKUCHA

 Uwanja wa Sokoine ambao unakumbukwa kwa hotuba aliyoitoa mwalimu Nyerere Mwaka 1995 ambayo imeendelea kuwa ujumbe wa kila siku kwenye vyombo vya habari hasa kwenye harakati za kusaka madaraka ya kuingia Ikulu
 Mpiga picha wa TBC akiwa tayari kwa kazi ya kuleta  picha na hatmaye kuunganishwa moja kwa moja kwenye matangazo yanayoendelea kupitia kituo hicho katika uwanja wa sokoine mjini Mbeya
 Wandishi wa habari wakiendelea kufanya kazi zao uwanjani hapo.

 Bendi ya Sikinde wakitumbuiza kwenye uwanja wa sokoine wakati wa maadhimisho kabla mhe Rais hajawasili uwanjani hapo kupokea maandamano
 Mkuu wa mkoa wa IRINGA Christine Ishengoma akiwasili uwanjani hapo na kusalimiana na timu ya mapokezi
 Hapa Mkombe Zanda wa Star Tv akizungumza na mpigapicha katika safu ya mawasiliano Ikulu Fred Maro katika uwanja wa sokoine
 aisee Mbeya yetu Mnatisha, picha zenu nimekuwa nikizifuatilia " ndivyo anavyoeleza Fred Maro wakati wakisalimiana na Joseph Mwaisango mwandishi wa Mbeya yetu
 Mwandishi mkuu wa Mbeya yetu Joseph Mwaisango akisalimiana na mdau Fred Maro kwenye uwanja wa sokoine
 Ngoma ya kabila la wasafwa ikiburudisha wakazi watu waliofurika uwanja wa sokoine kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi
Timu ya Uhuru Publication ikiwa uwanjani hapo kunadi bidhaa wanazozizalisha ambapo gazeti lao leo lilipata soko uwanjani hapo

Na Timu ya INDABA BLOG

Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi mkoani Mbeya yameambana na ukaguzi mkali katika milango ya kuingilia ambapo mabango na zana zote zimekuwa kichekiwa kwa vyombo

Hatua hiyo inalenga kuimarisha usalama uwanjani hapo kwa kuzingatia kuwa ni jukumu muhimu katika kuwezesha nchi kutulia

Imeelezwa kuwa mabango yenye ujumbe wa kejeli yamekuwa yakiishia mikononi mwa maofisa wa idara za usalama na kufanyika screening ya ujumbe unaoingizwa uwanjani
Kwa ujumla uwanja wa sokoine umefurika huku kila kona kukiwa na makundi ya watu wanaotaka kuingia na kushuhudia kupanda ama kimya kwa mishahara na mambo mengine ya wafanyanyakzi ambao kwa namna moja ama nyingine wanaathiri maisha ya kila siku ya ndugu zao

hadi wakati huu saa 5.15 bado kupo shwari na mandamano yanasubiri kiongozi wa nchi Mh Rais Jakaya Kikwete aingie ndipo waendelee na shughuli za kupita mbele ya jukwaa na kukaguliwa