Adverts

Jul 5, 2013

KILIMO CHA MAZAO YA CHAKULA CHA SISITIZWA


Na  Angela Kivavala dsj

Wana nchi wa wilayani mbozi wameshauliwa kujijengea utamaduni wakuhifadhi akiba ya chakula kwenye kaya zao ili kuziwezesha kaya zao kuwa na chakula cha hakiba kwa msimu

Hayo yalisemwa katika maadhimisho ya siku ya selikali za mitaa yaliyofanyika katika wilaya ya mbozi kata ya igamba kijiji cha hatelele  yaliyo kuwa na kaulimbiu isemayo amani uadilifu na uwajibikaji ninyenzo muhimu katika mchakato wa katiba mpya na ustawi wa serikali za mitaa.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Makamu mwenyekiti wa Halimashauri ya wilaya ya Mbozi   Ndugu Allan Mgula  alipokuwa ana hutubia wananchi wa wilaya ya mbozi katika maadhimisho hayo

“ nawaomba wananchi wa wilaya hii ya Igamba mshirikiane katika kulima  na kuhifadhi mazao ya chakulatuogope kuwa ombaomba keani ni aibu kuomba chakula”

Pia aliwapongeza wanakijiji wa Hatelele walio jitangaza kuwa ni waadhilika wa ugonjwa wa ukimwi na kwamba kuwa wa wazi kuta punguza kasi ya maambukizi ya ugonjwa huu wa ukimwi wilayani

Aidha aliwasisitizawananchi wa wilaya ya Mbozi kushirikiana katika mikutano ya hadhara ili wawezekusomewa taarifa za mapato na matumizi kila baada ya miezi mitatu.

Ndugu Mgula aliwataka wananchi wa wilaya ya Mbozi kuudhuria katika vikao vya mabaraza ya mchakato wa kupata katiba mpya ya Tanzania

Aliwataka wananchi wa wilaya ya Mbozi kuwapeleka watoto wa kiume”kutahiliwa” kufanyiwa usafi kwani kufanya hivyo kutapunguza magonjwa ya zinaa kwa watoto wa kiume na pia huduma hizo hutolewa bure kwenye hospitali ya wilaya

Maadhimisho hayo yali hudhuriwa na wa fanya kazi wa Halmashauri ya wilaya Madiwani wa kata Wenyekiti wa wa vijiji wenyeviti wa matawi watendaji wa vijiji makatibu wa tawi naChifu wa kijiji na wananchi wa wilaya ya Mbozi.