Adverts

Jul 9, 2013

MBOZI YAKABILIWA NA CHANGAMOTO KATIKA SEKTA ZA ELIMU NA AFYA



Na Angela kivavala
Halmashauri ya wilaya Mbozi ina kabiliwa na tatizo la ukosefu wa shule za sekondari za kidato cha tano na sita.

Wilaya ina jumla ya shule za sekondari 55 ambazo kati ya hizo 40 ni za serikali na 15 ni za binafsi.kati ya shule hizo ni sita tu zenye elimu ya kidato cha tano na sita ambapo ya serikali ni moja nane za watu binafsi.

Kutokana na hali hiyo watoto wanaohitimu kidato cha nne wanalazimika kwenda nje ya wilaya ya Mbozi hususani  katika jiji la Mbeya kujiunga na kidato cha tano hali ambayo inawaingiza kwenye gharama kubwa wazazi wao

Aidha changamoto nyngine ni kasi ya ongezeko la watu ambapo ni matokeo ya kuzaliana kwa kasi ambapo kulingana na takwimu za sensa ya mwaka 2012, Mbozi ina jumla ya wakazi 446,339  na kati yake 55% wakiwa ni vijana na watoto.

Kwa mwaka wa fedha  2012/2013 hadi kufikia  Januari, 2013 jumla ya vyumba vya madarasa 11 vilijengwa katika shule 4 zilizopo Wilayani Mbozi na  vyumba vyote vilikuwa vimekamilika na kupokea wanafunzi 398 waliofaulu ambayo ni sawa na asilimia 100 ya wanafunzi waliokuwa wamekosa nafasi. 
 
Wilaya ina shule za msingi 160 ambazo kati ya hizo 158 sawa na 99% zinamilikiwa na Serikali na shule mbili (2) ni za watu binafsi.  Shule hizo zina jumla ya wanafunzi 93,516, ambao 45,789 sawa na 49% ni wavulana na 47,727 sawa na 51% ni wasichana.  Aidha shule hizo zina jumla ya walimu 2,000

 Changamoto zinazo ikumba sekta hii ya elimu ni pamoja  na upungufu wa walimu 464 kati ya mahitaji ya walimu 2,564 na kuwa na shule moja tu yenye kidato cha tano na sita ya serikali na shule moja ya binafsi. 
Kwa upande wa Sera ya Afya ya Tanzania inataka kila kijiji kuwa na zahanati.  Wananchi wamejenga zahanati 20 ambazo zipo hatua mbali mbali za ujenzi na 3 zimekamilika na zimeanza kutumika mwezi Januari 2013.

  Hivyo, jumla ya vijiji vyenye zahati hadi sasa ni 72 kati ya vijiji 101 vilivyopo katika Wilaya ya Mbozi ifikapo 2015 takribani vijiji 82 vitakuwa na zahanati. 

Kulingana na taarifa iliyotolewa kwenye maadhimisho ya serikali za mitaa  wilayani humo ,Sekta ya afya ina changamoto ya upungufu wa wafanyakazi na vitendeakazi  vikiwemo vifaa tiba pamoja na watoa huduma kwa ujumla.

Hayo yalisemwa katika taarifa ya utendaji ya halmashauri ya wilaya ya Mbozi kwa wananchi wa wilaya ya Mbozi katika  maadhimisho ya siku ya selikari za mitaa  yakiwa na lengo la kutoa mwanya kwa jamii kutambua na kuzifahamu shughuli za huduma mbali mbali zinatolewa na Taasisi za Serikali za Mitaa yaani Halmashauri Majiji, Manispaa na za wilaya.
Mafanikio hayo yametokana na Kuhamasisha na kuhimiza wananchi kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa madarasa, ushiriki wao ulitoa mchango mkubwa katika kufanikisha zoezi hiliMshikamano wa viongozi wakuu wa Serikali na halmashauri katika wilaya kufuatilia, kusimamia na hususani waheshimiwa madiwani.