Adverts

Oct 27, 2013

ASKARI WA UMOJA WA MATAIFA KUTOKA TANZANIA AUWAWA DRC



Na Kenny Katombe na Chrispin Mvano

KINSHASA (Reuters) – Mmoja wa walinzi wa Umoja wa Mataifa kutoka nchini Tanzania  aliuawa na mwingine kujeruhiwa wakati wa siku ya tatu ya mapigano kati ya vikosi vya serikali na waasi katika mashariki ya Kongo siku ya Jumapili, wakati wakielekea kwenye  ngome ya waasi wa Rutshuru .

Mkuu wa  vikosi vya Umoja wa Mataifa nchini Kongo ( MONUSCO ) alisema mlinda amani kutoka Tanzania aliuawa wakati wa kupambana na waasi wa M23 katika mji wa Kiwanja, kaskazini ya mji mkuu wa mkoa Goma , mji mkubwa mashariki mwa Kongo.
"Askari alikufa wakati wa kulinda watu wa Kiwanja, " Martin Kobler , mkuu wa MONUSCO, alisema katika taarifa. Katika awamu ya kwanza  ya mapigano kati ya jeshi na waasi mwishoni mwa Agosti , waasai hao waliwauawa  askari wawili wa kulinda amani wa Tanzania.
Kufuatia miezi miwili ya utulivu  katika ukanda  wa mapigano, mapigano yamelipuka ghafla Ijumaa baada ya mazungumzo ya amani nchini Uganda kuvunjika baada ya  M23 kutaka viongozi wake wapewe msamaha kamili . Kila upande umekuwa ukilaumiwa na mwingine kuhusika na kuanzisha  mapigano.

Rais Joseph Kabila, ambaye wiki iliyopita alitishia kurejea kwenye  hatua za kijeshi , na kudai kuwa msamaha pekee kwa VIONGOZI wa M23  bila  masharti si haikubaliki.