Adverts

Oct 26, 2013

ASKOFU MSTAAFU RAYMOND MWANYIKA AFARIKI DUNIA



Askofu mstaafu wa kanisa katoliki Jimbo la Njombe, Raymond Mwanyika amefariki dunia jana mkoani Njombe.
Taarifa iliyotolewa na kanisa katoliki Njombe inaeleza kuwa Mwanyika amefariki 24 October,2013


Askofu Mwanyika alizaliwa mwaka 1930 huko kijiji cha Uwemba-Njombe,baada ya makuzi na majiundo yake ya kiroho na kimwili alipata daraja takatifu la Upadre 11/10/1959;mnamo 16/01/1971 Baba Mtakatifu Paulo VI alimteua kuwa askofu wa Njombe,na 25/04/1971 alisimikwa kuwa Askofu rasmi wa Jimbo la Njombe.

June,8 2002 Askofu Mwanyika alipumzika na nafasi yake kuchukuliwa na Askofu Maluma.

Askofu Mwanyika amekuwa Padre kwa miaka 54 na Askofu kwa miaka 42,atakumbukwa kwa majitoleo yake ktk kuwahudumia watu wa Njombe bila kujali tofauti zao za kiimani,alikuwa mstari wa mbele ktk kuendeleza huduma za jamii kama hospitali na shule,huduma za maji na umeme ktk maeneo mengi ya Njombe,Makete mpaka Ludewa.

Anatarajiwa kuzikwa 29/10/2013 ndani ya kanisa katoliki la Njombe(Njombe Cathedral)....Bwana alitoa na Bwana ametwaa,jina lake lihimindiwe.
hapa ni baadhi ya taarifa  muhimu juu yake kwa mujibu wa jarida pepe la  Vatican
DateAgeEventTitle
1930
BornUwemba
11 Oct 195929.8Ordained PriestPriest
16 Jan 197141.0AppointedBishop of Njombe, Tanzania
25 Apr 197141.3Ordained BishopBishop of Njombe, Tanzania
8 Jun 200272.4ResignedBishop of Njombe, Tanzania
24 Oct 201383.8DiedBishop Emeritus of Njombe, Tanzani
AMINA