Adverts

Oct 27, 2013

BREACKING NEWS.......JAMAL MALINZI AWA RAIS MPYA TFF


Taarifa zilizoufikia mtandao huu kutoka chumba cha kuhesabia kura kwenye mkutano mkuu wa uchaguzi wa TFF ni kwamba Mgombea urais wake Jamal Malinzi ameshinda kwa kura nyingi mbele ya mgombea mwenzake Athuman Nyamlani.
Inaelezwa kuwa Malinzi amejizolea kura 73 kati ya 125 zilizopigwa huku Athumani Nyamlani akiambulia kura 52.
Mchaka mchaka huoulianza kwa Nyamlani kuanza kuongoza wakati wa kuhesabu kura ambapo kura za kwanza 36 kwa 14 za Malinzi ziliamsha shangwe kwa wafuasi wake,lakini baadaye hali ilibadilikwa kwa Malinzi kuweka "gap" kubwa hadi kura 67 kwa 41.
Hali hiyo iliendelea kuwa tamu kwa upande wa kundi la Malinzi kwa mtindo wa Tieni tieni kwa moyo mmoja" na ikiwa hadi mwisho Malinzi akaibuka kidedea huku Tenga akitamka kuwa atampa ushirikiano. Matokoe hayo yalitolewa rasmi saa 8.21 Usiku

Matokeo hayo yalitanguliwa na matokeo mengine ya chaguzi za awali ambapo ilipofika kwa makamu wa rais Walace Karia aliibuka kidedea kwa kuwafunika  Nassib Ramadhan na Iman  Madega  a.ka. Seneta