Adverts

Dec 10, 2013

SIMANZI- DIWANI WA VITI MAALUM CCM -KATA YA ITAKA MBOZI HATUNAYE TENA

Enzi za maisha yake Mh Diwani Salome Lazaro Kibweja akiwa katika moja ya vikao vya baraza la madiwani Mbozi

Baadhi ya waliomfahamu Mh Kibweja wakishindwa kujizuia kulia katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi leo asubuhi 

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Mbozi Erick Minga akizungumza na menejiment ya halmashauri ya wilaya katikati ni afisa Utumishi na raslimali watu bwana Lulandala na kushoto ni Dr Mkombachepa mkurugenzi wa halmashauri hiyo

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Dr Charles Mkombachepa akizungumza kwa ufupi namna ratiba ya mazishi itakavyokuwa


Baadhi ya waheshimiwa madiwani wakiwa wametulia ukumbini kabla ya kuanza kuaga mwili wa marehemu

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi Mh Erick Minga akitoa taarifa ya msiba huo, sambamba na kusoma historia ya marehemu Salome Kibweja 


Afisa Usafirishaji wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi Paschal Chuwa akitoa ufafanuzi kwa mwenyekiti wa halmashauri hiyo Erick Minga kabla ya kuanza safari ya kuuepeleka mwili wa marehemu kijiji cha Itaka kwaajili ya Mazishi


Na Danny Tweve-Mbozi
Aliyekuwa diwani wa viti maalumu wa kata ya Itaka -Salome Lazaro Kibweja ameagwa rasmi na watumishi na waheshimiwa madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi leo asubuhi tayari kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika mchana huu kijijini kwake Itaka.

Salome alifariki usiku wa kuamkia 8 decemba katika hospitali ya rufaa ya Mbeya baada ya kuugua kwa muda mfupi akiwa anashiriki sherehe ya kipaimara ya mtoto wa dadayake jijini Mbeya

Salome Kibweja aambaye alizaliwa mwaka 1975 alihitimu darasa la saba 1991 na akaingia kwenye siasa na kugombea viti maalumu mwaka 2010 ambako alishinda viti maalumu.

kulingana na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi Erick Minga, akiwa kwenye sherehe hiyo siku ya jumamosi Disemba 7 alianza kujisikia kuumwa kichwa ambapo alipelekwa kwenye zahanati ya jirani na eneo la sherehe na baadaye kufikishwa hospitali ya rufaa ya Mbeya.

Mazishi ya Mheshimiwa Kibweja yatafanyika katika kijiji cha Itaka leo mchana