Adverts

Dec 29, 2014

LIGI KUU YA VODAOM YAINGIA RAUNDI YA 9




Wakati raundi ya nane ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inakamilika leo (Desemba 29 mwaka huu) kwa mechi tatu, ligi hiyo itaingia raundi ya tisa Januari 3 mwakani kwa mechi tano.

Coastal Union itacheza na JKT Ruvu katika Uwanja wa Mkwakwani, Ruvu Shooting itaikaribisha Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Mabatini, Azam itakuwa mwenyeji wa Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Azam Complex, Stand United itakuwa mgeni wa Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri wakati Mbeya City na Yanga zitaoneshana kazi kwenye Uwanja wa Sokoine.

Ligi hiyo ambayo itachezwa mfululizo (non-stop) hadi itakapomalizika Mei 9 mwakani, itakamilisha raundi ya tisa Januari 4 mwakani kwa mechi kati ya Mgambo Shooting na Simba kwenye Uwanja wa Mkwakwani, na Tanzania Prisons itakayokuwa mwenyeji wa Ndanda kwenye Uwanja wa Sokoine.

Nayo mechi kati ya Mtibwa Sugar na Stand United ambayo jana ilivunjwa na mvua dakika ya 6 imemaliziwa leo ambapo timu hizo zimetoka sare ya bao 1-1.

Wakati huo huo, mechi ya ligi iliyochezwa jana usiku kwenye Uwanja wa Azam Complex imemalizika kwa wageni Ruvu Shooting kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Ruvu. Bao hilo lilifungwa kipindi cha kwanza kwa mkwaju wa penalti uliopigwa na Hamisi Kasanga.  

MBAO FC YAKAMATA USUKANI SDL
Timu ya Mbao FC ya Mwanza imekamata uongozi wa Kundi B la michuano ya Ligi Daraja la Pili (SDL) baada ya jana (Desemba 27 mwaka huu) kuizamisha JKT Rwamkoma ya Mara mabao 2-1.

Kwa matokeo hayo katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mbao FC imeitoa kileleni JKT Rwamkoma baada ya kufikisha pointi tisa kwa kushinda mechi zote tatu dhidi ya Arusha FC, Pamba na JKT Rwamkoma.

Mbao FC inafuatiwa na JKT Rwamkoma yenye pointi sita, Arusha FC pointi sita wakati Bulyanhulu na Pamba zikiwa za mwisho kwa pointi moja kila moja. Kundi hilo litakamilisha mzunguko wa kwanza Januari 3 mwakani kwa mechi kati ya JKT Rwamkoma na Arusha FC, na Bulyanhulu na Mbao FC.

Katika kundi A, Mji Mkuu (CDA) na Singida United ndizo zinazochuana kileleni kwa kufikisha pointi saba kila moja. Timu hizo zinafuatiwa na Milambo yenye pointi nne, Mvuvumwa FC yenye pointi moja wakati Ujenzi Rukwa ni ya mwisho ikiwa haina pointi.

Hata hivyo, Mvuvumwa FC na Milambo ziko nyuma kwa mechi moja. Mechi hiyo ya kukamilisha raundi ya tatu kati ya timu hizo itachezwa kesho (Desemba 29 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.

Kiluvya United imeendelea kuchachafya kundi C baada ya kushinda mechi zote ne ilizocheza, hivyo kufikisha pointi 12. Inafuatiwa na Mshikamano yenye pointi saba huku Abajalo ikiwa katika nafasi ya tatu kwa pointi 6.

Nafasi ya nne inashikwa na Transit Camp yenye pointi nne, Cosmopolitan yenye pointi mbili ni ya tano wakati Kariakoo ambayo haina pointi ni ya mwisho. Hata hivyo, Cosmopolitan na Kariakoo zina mchezo mmoja mkononi.

Mechi zinazofuata za kundi hilo ni Januari 3 mwakani kati ya Kariakoo na Mshikamano na Mshikamano (Ilulu), Transit Camp na Abajalo (Mabatini), na Cosmopolitan na Kiluvya (Karume).

Kundi D, vinara bado ni Njombe Mji yenye pointi 12 ikifuatiwa na Wenda yenye pointi sita wakati Volcano FC iko nafasi ya tatu ikiwa na pointi tano. Mkamba Rangers ina pointi nne, Town Small Boys ina pointi moja wakati Magereza FC haina pointi.

Katika kundi hilo leo (Desemba 28 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Town Small Boys na Magereza itakayochezwa Uwanja wa Majimaji mjini Songea.  Januari 3 mwakani kutakuwa na mechi kati ya Town Small Boys na Njombe Mji, Volcano FC na Magereza, na Wenda na Mkamba Rangers.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

MCHEZO WA KIMONDO NA KMC (TESSEMA) WARUDISHWA TAREHE 05/01


Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania TFF limefanya marekebisho ya Ratiba ya mchezo baina ya Kimondo SSC na KMC zamani TESSEMA uliopangwa awali kuchezwa January 07,2015 na sasa utachezwa January 05,2015.

hatua hiyo inatokana na maombi ya Timu ya Kimondo ambayo ina michezo ya ugenini mfululizo kuanzia kwa takribani siku 14 hivyo kuigharimu timu hiyo katika kuendesha kambi za ugenini

Kimondo iliwasilisha maombi yake TFF kuomba mchezo wake na KMC kurejeshwa nyuma ili kuipunguzia timu hiyo gharama kwakuwa ilikuwa na michezo miwili jijini Dar es salaam na baada ya hapo ingechukua siku 8 kusubiri mchezo na KMC hali ambayo ingeiathiri hasa kwenye suala zima la usafiri

Mabadiliko hayo kulingana na TFF yanahusisha mchezo namba 81 tu na kwamba michezo mingine itaendelea kama ilivyopangwa.

Dec 28, 2014

KIMONDO YAANZA DURU YA PILI YA LIGI DARAJA LA KWANZA KWA KUMTOA NISHAI KOCHA WAKE ALIYELALA MBELE

TIMU ya Kimondo ya Mbozi, jana Jumamosi ilianza vyema safari ya kuwania kucheza ligi kuu baada ya kuibabadua timua Villa Squard ya Jijini Dar es salaam bao 1-0 katika mchezo mkali uliofanyika uwanja wa Karume.
Mchezo huo ambao ulichezwa kwa dakika 103 ulimalizika kwa ushindi huo mnono uliopatikana mnamo dakika ya 39 kupitia kwa Mwamba Timoth Mkumbwa

Licha ya jitihada za hapa na pale za kocha wa Villa Squard ambaye katika duru la kwanza alikuwa akiifundisha Kimondo kabla ya kuitekelekeza bila maelezo yoyote, alishuhudia jahazi lake likizama kwa bao hilo moja.

Nov 9, 2014

KIMONDO YAWAPIGISHA KWATA WAPIGANAJI WA MLALE JKT, YAWABANJUA 2-1 KWAO



JKT MLALE HOII MBELE YA KIMONDO!!! YAAMBULIA TWO KWA MOJA!!!
Timu ya Kimondo SSC ya Mbozi imeendeleza ubabe tangu irejee nyanda za juu kusini baada ya kuibabua mabao 2-1 Timu ya Masoja ya Mlale Jkt katika uwanja wa majimaji Mjini Songea.

Ikicheza ugenini kwa kujiamini, Kimondo ilijikuta ainakubali kufungwa bao la mapema na kuwaamsha wenyeji Mlale JKT kwa kusherehekea dakika 30 za mwanzo

Kimondo iliamka kwa kasi na kuanza kupeleka mashambuzi kwenye lango la Mlale, ambapo mashambulizi hayo yalidumu kwa muda na kuwapatia bao la kusawazisha.
Kipindi cha Pili mchakamchaka wa Kimondo uliendelea na kuwawezesha kupata bao la pili na hadi mchezo unamalizika wenyeji wameondoka uwanjani wakiuguza maumivu ya kichapo kwenye uwanja wa nyumbani.
kwa mchezo wa leo Kimondo imefikisha pointi 11 ikiwa imeshinda michezo 4 na kufungwa 4 imeshinda magoli 10 na imefungwa mabao 8 ikipanda hadi nafasi ya nne kwenye kundi lao ambalo linaongozwa na timu za Majimaji na Friends Rangers zikifuatiwa na Lipuli na  Kurugenzi
Jumatano Kurugenzi itakuwa mgeni wa Kimondo kwenye uwanja wa CCM Vwawa kujiwinda katika michezo ya lala salama kabla duru la kwanza halijagonga ukingoni.  

Nov 6, 2014

LIGI DARAJA LA KWANZA, KIMONDO KWAO WAMOOOO

Kimondo ya Mbozi imezinduka kwenye uwanja wake wa Nyumbani baada ya kuifanyia mahaba African Sports ya Tanga mabao 2-0 kwenye mchezo wa ligi daraja la kwanza.

Mchezo huo wa katikati ya wiki ulifanyika uwanja wa CCM  Vwawa, ambapo mchaka mchaka wake ulionekana tangu kuanza kwa mchezo huo ambapo mabao mawili yalipatikana chini ya dakika 20 za kipindi cha kwanza.

Licha ya jitihada za African Sport ya Tanga kuonyesha jitihada binafsi za wachezaji wake, kuna wakati walipotezwa maboya kwa zaidi ya dakika 20 wakizungushwa kwa staili ya haingaisha bwege kutokana na gonga za hapa na pale za Kimondo

African Sport walipata nafasi mbili muhimu ambazo zingewapa ushindi mnono lakini wachezaji wake hawakuwa makini kutupia langoni kutokana na kuwa wazito kama wamefungiwa mawe miguuni.

Hata hivyo Kimondo inapaswa kujilaumu kwa kukosa nafasi nyingi zaidi ambazo zingeweza kubadili ubao wa magoli hata kusomeka 10-0 kama wachezaji wake wangeacha mambo ya "show game" na kurudhika na mabao mawili waliyokuwa wamepata.

Kutokana na matokeo hayo Majimaji ya Songea na Friends Rangers zinagombana kileleni zikiwa na Pointi 15, zikifuatiwa na Lipuli imefikisha pointi 13,Kimondo ikiruka kutoka nafasi ya saba hadi ya tano

Kumekuwepo malalamiko kwa timu wenyeji kutumia viwanja vyao vya nyumbani vibaya, mchezo unaolalamikiwa ni pamoja na Kimondo na Lipuli wiki iliyopita ambapo licha ya Kimondo kufungwa kwa miundombinu, mashabiki wa Iringa waliamua kuhamia Kimondo kuishangilia kutokana na kandanda saafi walillolionyesha licha ya kuminywa!
"Kuna wakati mlinzi wa Lipuli aliudaka mpira ndani ya penarti box, maajabu ya musa mwamuzi aliuchukua mpira kwenye eneo la penalti na kuutoa nje ya 18  hadi mashabiki  wa Lipuli wakaanza kuzomea baada ya makosa hayo kuwa  ya wazi mno!! anaeleza mmoja wa mashabiki walioshuhudia mchezo huo

UTEUZI WA WAKUU WA MIKOA

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telegrams : "CABINET"
DAR ES SALAAM
Telephone : 2116898, 2116900/6
E-mail : chief@ikulu.go.tz
E-mail : ikulu@ikulu.go.tz
Fax : 2113425/2116914/2117272
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD
11400 DAR ES SALAAM.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amefanya uteuzi wa wakuu wapya wanne wa Mikoa, amewahamisha wengine sita na ameamua kuwa wengine watatu watapangiwa kazi nyingine.
Taarifa iliyotolewa mjini Dodoma jioni ya leo, Jumatano, Novemba 5, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue inasema kuwa, Wakuu wapya wa Mikoa ni Bi. Halima Omari Dendego ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Dkt. Ibrahim Hamisi Msengi ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Bi. Amina Juma Masenza ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa na Bwana John Vianney Mongella ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
Taarifa inasema kuwa kabla ya uteuzi wake Bi. Dendego alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Dkt. Msengi alikuwa  Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Bi. Masenza alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela na Bwana Mongella alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha.
Taarifa hiyo inasema kuwa Wakuu hao wapya wa Mikoa wataapishwa kesho, Alhamisi, Novemba 6, 2014 saa saba mchana, Ikulu, Dar es Salaam.
Aidha, taarifa hiyo imesema kuwa Wakuu wa Mikoa ambao watapangiwa kazi nyingine ni Kanali (Mst) Fabian Massawe wa Kagera, Dkt. Christine Ishengoma wa Iringa na Kanali Joseph Simbakalia wa Mtwara.
Wakuu wa Mikoa ambao wamehamishwa vituo vya kazi ni Bwana Magesa S. Mulongo ambaye anakwenda Mkoa wa Mwanza kutoka Arusha, Dkt. Rehema Nchimbi ambaye anakwenda Mkoa wa Njombe kutoka Dodoma, Bwana Ludovick John Mwananzila anakwenda Tabora kutoka Lindi, Kepteni (Mst) Anseri Msangi anayekwenda Mkoa wa Mara kutoka Njombe na Mhandisi Everist Ndikilo ambaye anakwenda Arusha kutoka Mwanza.
Wengine waliohamishwa ni Luteni (Mst) Chiku A.S. Galawa ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kutoka Tanga, Dkt. Rajab Rutengwe ambaye anakwenda Mkoa wa Tanga kutoka Katavi, Bi Fatma Mwasa ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita kutoka Tabora na Bwana Magalula S. Magalula ambaye anahamishiwa Lindi kutoka Geita.
Taarifa hiyo imesema kuwa Wakuu wa Mikoa ya Dar es Salaam, Kigoma, Kilimanjaro, Manyara, Mbeya,Morogoro, Pwani, Rukwa, Shinyanga, Ruvuma, Singida na Simiyu watabakia kwenye vituo vyao vya sasa.
Aidha, Rais Kikwete amefanya uteuzi wa Wakuu wapya wa Wilaya, kuhamisha baadhi yao na kutengua uteuzi wa baadhi. Taarifa kamili itatolewa na Waziri Mkuu baada ya kuwa wamepangiwa vituo vya kazi.

Mwisho.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
05 Novemba,2014

RAIS ATEUA MAKATIBU WAKUU NA KUHAMISHA WENGINE

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telegrams : "CABINET"
DAR ES SALAAM
Telephone : 2116898, 2116900/6
Fax : 2113425/2116914/2117272
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD
11400 DAR ES SALAAM.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amefanya uteuzi wa Makatibu Wakuu wa Wizara kwa kuteua Makatibu Wakuu wanne wapya na kuhamisha mmoja.
            Aidha, Rais Kikwete amefanya uteuzi na uhamisho wa Makatibu Tawala wa Mikoa.
Taarifa iliyotolewa mjini Dodoma jioni ya leo, Jumatano, Novemba 5, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa walioteuliwa kuwa Makatibu Wakuu ni Dkt. Donan Mmbando ambaye anakuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Yohana Budeba ambaye anakuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mhandisi Mbogo Futakamba kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Dkt. Adelhelm James Meru ambaye anakuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Maliasili.
Kabla ya uteuzi wake, Dkt Mmbando alikuwa Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Budeba alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Uvuvi na Mifugo, Mhandisi Futakamba alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maji na Dkt. Meru alikuwa Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA).
Aidha, taarifa hiyo imesema kuwa Rais Kikwete amemhamisha Bibi Maimuna Tarishi kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii kwenda kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria
Kuhusu uteuzi na uhamisho wa Makatibu Tawala wa Mikoa, Rais Kikwete amemteua Bw. Charles Pallangyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita, Bw. Adoh Steven Mapunda, Mkurugenzi Mtendaji, Manispaa ya Bukoba kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Bw. Severine Kahitwa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro na Dkt. Faisal Issa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza.
Wakati huo huo, Rais Kikwete amemteua Kanali (Mst) Joseph Simbakalia, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, kuwa Mkurugenzi Mkuu wa EPZA.
Uteuzi huo unaanza leo na Makatibu Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa wataapishwa kesho, Alhamisi, Novemba 6, 2014, Ikulu, Dar es Salaam.
Mwisho.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
05 Novemba,2014

Nov 1, 2014

MAKOCHA 35 KUSHIRIKI KOZI YA LESENI C YA CAF





Tanzania Football Federation
Affiliated to FIFA, CAF and CECAFA

3rd Floor, PPF Tower, Garden Avenue / Ohio Street
P.O.  Box  1574, Dar es  Salaam, Tanzania     .    Telefax:   + 255-22-2861815
E-mail: tanfootball@tff.or.tz     .    Website: www.tff.or.tz








Release No. 168
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Oktoba 31, 2014
MAKOCHA 35 KUSHIRIKI KOZI YA LESENI C YA CAF
Makocha 35 wameteuliwa kushiriki kozi ya ukocha ya Leseni C ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) itakayofanyika mjini Morogoro kuanzia Novemba 5 hadi 19 mwaka huu.

Kozi hiyo itaendeshwa na Mkufunzi wa CAF, Sunday Kayuni na itafanyikia Mchikichini College ambapo washiriki wote wanatakiwa kuwasilisha vyeti vyao vya ukocha vya ngazi ya Kati (Intermediate) pamoja na vyeti vya kitaaluma vya elimu ya sekondari (academic).

Washiriki wa kozi hiyo ni Abdulmaliki Nemes (Airport FC), Ahmed Haule (Kilimanjaro Talented Youth Sports Centre), Ally Jangalu (Moro Kids), Amri Saidi (Mwadui FC), Athuman Kambi (Morogoro), Charles Mwakambaya (Burkina Faso FC),  Damian Mussa (Alliance One) na Daudi Sichinga (Kasulu United).

Denis Maneva (Shule ya Msingi Logo), Edgar Juvenary (JUT- Mlale), Hamisi Mangolosho (Shule ya Msingi Mtimbwilimbwili), Henry Ngondo (Chalinze Academy), Issa Hamisi (Polisi Kilimanjaro), Jumanne Chale (Dar es Salaam), Kizito Mbano (Masasi Alliance), Martin Saanya (Magereza Morogoro) na Masoud Gumbwa (Sokoine University Academy).

Mbwana Makata (Oljoro JKT), Mrage Kabange (Kagera Sugar), Muhibu Muhibu (Stand United FC), Nsubuga Solomon (Kishoto FC), Nyamtimba Muga (Kizuka Secondary), Oscar Mirambo (Makongo), Rashid Abdallah (Tech Fort Academy), Renatus Shija (Rhino Rangers), Safari Nyerere (Elimu Sports Academy) na Said Lyakuka (Kizuka Stars).

Simeon Mwesa (Mtibwa Sugar U20), Simon Shija (Tabora), Suleiman Mtungwe (Ruvu Shooting), Swalehe Allawi Abdul (Alliance Academy), Yasin Bashiri (Kick Off Sports Academy) na Zuberi Katwila (Mtibwa Sugar).

Wakati huo huo, kutakuwa na kozi ya wiki mbili ya ukocha ya ngazi ya Kati (Intermediate) itakayofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Desemba 29 mwaka huu.

Makocha wote wanaotaka kushiriki kozi hiyo wanatakiwa kutuma maombi katika Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA).
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Oct 28, 2014

CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU CHA ZAMBIA CHAIJIA JUU TIMU YA WANAWAKE YA TAIFA


Football Association of Zambia (FAZ) Photo: FOOTBALL ASSOCIATION OF ZAMBIA.

PRESS STATEMENT.

October 28, 2014

POSITION ON THE "SHEPOLOPOLO".

The Football Association of Zambia has noted with dismay the high level of indiscipline exhibited by the Senior Zambia National Women’s Soccer team after their elimination from the 2014 Africa Women’s Championships in Namibia.

This kind of behavior where a group of young ladies want to hold the Association to ransom is alien to football and cannot be tolerated and condoned.

Never in the recent past has the Association been made to fulfill so many international fixtures and tournaments as has been the case, the last two years, beginning with the qualification of the Under 17 women’s team to the Junior World Women’s Championships in Costa Rica. This was followed by the qualification of the Senior Women’s Team to their maiden Africa Women Championships in Namibia. And then came the qualification of the boys Under 17 and 20 teams to the Africa Youth Championships to be held in early 2015. This is besides the numerous local training camps for the local national team that are costing the Association dearly. 

These fixtures and tournaments have taken a heavy toll on the Association’s finance base which has resulted in many sacrifices being made especially with regard to meeting costs for its various sub-committee meetings and other pertinent needs.
 
The Under 17 and 20 boys teams have both qualified to their respective 2015 African Youth Championship finals with little or nothing from the Association but pride and dedication to duty. The players from these two teams have not held the Association to ransom despite only getting their FIFA approved stipends from the Football Association of Zambia.

It must be further stated that the Association does not receive any form of financial assistance and support from the Government to fulfill programs both for the women and boys junior national teams. FAZ relies on the resources realized from sponsorships and gate revenue from International matches by the Senior National Team to meet these international fixtures.

It has been the resolve of the Association that neglecting junior and women’s programs will negate and impact negatively on the performance of the Senior National Team which is the torch bearer of Zambian football.
In must be emphasized that FAZ has sacrificed a lot of its time and resources to ensure that women and junior national programs are fulfilled, even to the extent of depleting the Association’s resources to the barest minimum. 

There are so many players and officials who have sacrificed for this country who have never displayed this callous disregard for authority. 
In this regard, The Football Association of Zambia will be taking steps to address issues of the women national football teams going forward.

George M Kasengele
GENERAL SECRETARY.
PRESS STATEMENT.

October 28, 2014

POSITION ON THE "SHEPOLOPOLO".

The Football Association of Zambia has noted with dismay the high level of indiscipline exhibited by the Senior Zambia National Women’s Soccer team after their elimination from the 2014 Africa Women’s Championships in Namibia.

This kind of behavior where a group of young ladies want to hold the Association to ransom is alien to football and cannot be tolerated and condoned.

Never in the recent past has the Association been made to fulfill so many international fixtures and tournaments as has been the case, the last two years, beginning with the qualification of the Under 17 women’s team to the Junior World Women’s Championships in Costa Rica. This was followed by the qualification of the Senior Women’s Team to their maiden Africa Women Championships in Namibia. And then came the qualification of the boys Under 17 and 20 teams to the Africa Youth Championships to be held in early 2015. This is besides the numerous local training camps for the local national team that are costing the Association dearly.

These fixtures and tournaments have taken a heavy toll on the Association’s finance base which has resulted in many sacrifices being made especially with regard to meeting costs for its various sub-committee meetings and other pertinent needs.

The Under 17 and 20 boys teams have both qualified to their respective 2015 African Youth Championship finals with little or nothing from the Association but pride and dedication to duty. The players from these two teams have not held the Association to ransom despite only getting their FIFA approved stipends from the Football Association of Zambia.

It must be further stated that the Association does not receive any form of financial assistance and support from the Government to fulfill programs both for the women and boys junior national teams. FAZ relies on the resources realized from sponsorships and gate revenue from International matches by the Senior National Team to meet these international fixtures.

It has been the resolve of the Association that neglecting junior and women’s programs will negate and impact negatively on the performance of the Senior National Team which is the torch bearer of Zambian football.
In must be emphasized that FAZ has sacrificed a lot of its time and resources to ensure that women and junior national programs are fulfilled, even to the extent of depleting the Association’s resources to the barest minimum.

There are so many players and officials who have sacrificed for this country who have never displayed this callous disregard for authority.
In this regard, The Football Association of Zambia will be taking steps to address issues of the women national football teams going forward.

George M Kasengele
GENERAL SECRETARY.

Oct 24, 2014

KOZI YA MAKOCHA YAANZA LEO



Release No. 164
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Oktoba 23, 2014

RAIS WA TOC KUFUNGA KOZI YA MAKOCHA
Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Gulam Rashid kesho (Oktoba 24 mwaka huu) atafunga kozi ya makocha ya Leseni C ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).

Hafla ya ufungaji kozi hiyo iliyoshirikisha makocha 32 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar na kuandaliwa na TOC kupitia Olympic Solidarity kwa ushirikiano na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) itafanyika saa 5 asubuhi kwenye hosteli za TFF zilizopo Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Kozi hiyo ya wiki mbili iliyoanza Oktoba 12 mwaka huu iliendeshwa na Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) Ulric Mathiot kutoka Shelisheli.

Makocha walioshiriki kozi hiyo ni Ahmed Suleiman Simba (Alliance), Akida Saidi (Lindi), Ally Bushir Mahmoud (Zanzibar), Aloyce Akwilin (Pwani), Amin Rashid Mdowe (Zanzibar), Augustino Dakto Damian (Katavi), Athuman Bilal (Shinyanga), Bakari Shime (Tanga), Charles Mayaya (Shinyanga) na Choki Abeid (Geita).

Wengine ni Edna Lema (Morogoro), George Melchior (Kagera), Godfrey Kapufi (Katavi), Hamis Mabo (Kigoma), Hawa Bajangero (TWFA), Ibrahim Mulumba (Geita), Jemedari Said (TAFCA), Kenny Mwaisabula (TAFCA), Madenge S. Omari (Mara), Milambo Camil (Tabora) na Mohamed D (Ruvuma).

Pia wapo Mohamed Ismail Laiser (Manyara), Mohamed Muya (Dodoma), Ngawina Ngawina (Mtwara), Nicholas Kiondo (Ilala), Osuri Charles Kosuri (Simiyu), Rachel Palangyo (TWFA), Salvatory Edward (Temeke), Seif Bausi Nassor (Zanzibar), Yusuf Macho (Kigoma), Wilfred Mollel (Iringa) na Zacharia Mgambwa (Rukwa).

Makocha watakaofaulu kozi hiyo watapewa Leseni C za CAF wakati watakaoshindwa watapewa vyeti vya ushiriki tu.  

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)