Adverts

Dec 28, 2014

KIMONDO YAANZA DURU YA PILI YA LIGI DARAJA LA KWANZA KWA KUMTOA NISHAI KOCHA WAKE ALIYELALA MBELE

TIMU ya Kimondo ya Mbozi, jana Jumamosi ilianza vyema safari ya kuwania kucheza ligi kuu baada ya kuibabadua timua Villa Squard ya Jijini Dar es salaam bao 1-0 katika mchezo mkali uliofanyika uwanja wa Karume.
Mchezo huo ambao ulichezwa kwa dakika 103 ulimalizika kwa ushindi huo mnono uliopatikana mnamo dakika ya 39 kupitia kwa Mwamba Timoth Mkumbwa

Licha ya jitihada za hapa na pale za kocha wa Villa Squard ambaye katika duru la kwanza alikuwa akiifundisha Kimondo kabla ya kuitekelekeza bila maelezo yoyote, alishuhudia jahazi lake likizama kwa bao hilo moja.