Adverts

Dec 29, 2014

MCHEZO WA KIMONDO NA KMC (TESSEMA) WARUDISHWA TAREHE 05/01


Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania TFF limefanya marekebisho ya Ratiba ya mchezo baina ya Kimondo SSC na KMC zamani TESSEMA uliopangwa awali kuchezwa January 07,2015 na sasa utachezwa January 05,2015.

hatua hiyo inatokana na maombi ya Timu ya Kimondo ambayo ina michezo ya ugenini mfululizo kuanzia kwa takribani siku 14 hivyo kuigharimu timu hiyo katika kuendesha kambi za ugenini

Kimondo iliwasilisha maombi yake TFF kuomba mchezo wake na KMC kurejeshwa nyuma ili kuipunguzia timu hiyo gharama kwakuwa ilikuwa na michezo miwili jijini Dar es salaam na baada ya hapo ingechukua siku 8 kusubiri mchezo na KMC hali ambayo ingeiathiri hasa kwenye suala zima la usafiri

Mabadiliko hayo kulingana na TFF yanahusisha mchezo namba 81 tu na kwamba michezo mingine itaendelea kama ilivyopangwa.