Adverts

Jul 3, 2015

STARZ KUTUTOA MATONGO TONGO KESHO



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - RELEASE NO. 111
TAREHE 03 JULAI 2015


STARS KUWAVAA THE CRANES KESHO
Taifa Stars inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premieum Lager kesho jumamosi saa 10 kamili kwa saa za Afrika Mashariki itashuka dimba la Nakivubo kucheza na wenyeji Uganda.(The Cranes).

Mecho hiyo ya kesho ni mchez wa marudiano kuwania kufuzu kwa fainali za CHAN mwaka 2016 zitakazofanyika mapema mwezi Januari nchini Rwanda, mgeni rasmi atakua Rais wa Uganda Yoweri Mseveni.

Kikosi cha Taifa Stars chini ya kocha wake mkuu Charles Mkwasa, kiliwasili jijini Kampala jana usiku na kimefikia katika hoteli ya Grand Global iliyopo jirani na chuo kikuu cha Uganda Makerere.

Taifa Stars imefanya mazoezi leo jioni katika uwanja wa Nakivubo yakiwa ni mazoezi mepesi na mwisho kuzoea uwanja kabla ya mchezo wenyewe utakaofnayika kesho jioni.

Kocha Mkwasa akiongelea kuelekea mchezo huo amesema, anashukuru vijana wake wamefika salama wote, hali nzao ni nzuri, morali ni ya hali ya juu, kikubwa wanatambua wana deni kubwa kwa watanzania hivyo kesho watapambana kuhakikisha wanapata matokeo mazuri.

Akiongelea hali ya hewa na mazingira ya timu ilipofikia, Mkwasa amesema hali ya hewa ni ya kawaida baridi na mvua kidogo haina tofauti sana na Tanzania, mazingira ya hoteli ni mazuri na kusema kikubwa kilichobaki ni kusaka ushindi katika mchezo huo na vijana wake wapo tayari. 

Wakati huo huo mashabiki zaidi ya 50 kutoka nchini Tanzania wanatarajiwa kuwasili kesho jumamosi alfajiri wakitokea jijini Dar es salaam kuungana na watanzania wengine waishio nchini Uganda kuishangilia timu ya Tanzania itakapokuwa ikipimbana na Uganda katika uwanja wa Nakivubo.

Mawasiliano ya Afisa Habari wa TFF aliyepo Uganda ni +256 780 177008

NB: picha za mazoezi ya Taifa Stars Nakivubo leo zimeambatanishwa

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

KIMONDO YAAMUA KUMWAGA MBOGA, YAWEKA HADHARANI MIKATABA YA MWASHIUYA



Kimondo Super Sports Club
P.o Box 30, Mbozi.Mob.0755708828, 0764947555 E-mail:  kissc@gmail.com
OUR REF NO: KISSC/GC/02/07                                            03/07/2015
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KIMONDO BADO INATAMBUA KUWA GEOFREY B.MWASHIUYA NI MCHEZAJI WAKE MPAKA MSIMU WA 2017/2018
Klabu ya Kimondo Super Sports inayoshiriki ligi daraja la kwanza Tanzania yenye maskani yake wilayani Mbozi inapenda kutoa tamko juu ya mkanganganyiko wa taarifa za kuptosha za usajili wa mchezaji wake Geofrey Bahati Mwashiuya.
Klabu inasikitishwa saana na habari/taarifa zenye mkanganyiko zinazotolewa na msemaji wa timu ya Yanga,Katibu wa timu ya Yanga na mchezaji wetu Geofrey Mwashiuya katika vyombo mbalimbali vya habari;
Jerry Muro alisikika katika vyombo vya habari akijinadi kuwa klabu ya soka ya Yanga imemsajili Geofrey Mwashiuya tangu Oktoba,2014 kwa kandarasi ya miaka mitatu,wakati huohuo Katibu wa Yanga Dkt,Jonas Tiboroha alidai mchezaji huyu alisajiliwa na klabu ya Yanga tangu mwezi Februari,2015.
Klabu ya KIMONDO inasikitishwa na taarifa hizi zenye mkanganyiko mkubwa kuhusu suala la mchezaji huyu,na kwa kauli hizo mbili zinazokinzana Watanzania wanaweza kuona ukweli wa mambo ukoje.
Taarifa sahihi ni kwamba mchezaji Geofrey Mwashiuya ana mkataba wa miaka minne na timu yetu ya KIMONDO  na ndio muda sahihi ulioandikwa katika TMS na uliopo katika mkataba wa maandishi. Zaidi klabu ya KIMONDO inasikitishwa na taarifa hizi za upotoshwaji zinazofanywa na YANGA kwa makusudi kabisa kuwa mchezaji wetu hana mkataba na sisi,
Pia maneno ya mchezaji akijaribu kuudanganya umma wa Watanzania na wapenda soka kuwa alipewa kijikaratasi tu cha kujaza,alipokwenda TFF na Uongozi wa YANGA wakaarifiwa kuwa hiyo ni fomu ya uthibitisho wa mchezaji. Zaidi wanadai kuwa TFF iliwaambia kuwa mchezaji wa daraja la kwanza mara ifikapo mwisho wa msimu/ligi basi na mkataba wa mchezaji unakuwa umekwisha.
 Pia klabu ya KIMONDO ilisikia maneno hayo yaliyotamkwa na mchezaji yakiungwa mkono na katibu wa YANGA katika kipindi cha michezo cha anga la michezo cha Ebony Fm na mitandao ya kijamii siku ya jumatatu tarehe 29,June,2015 akijinasibu kuwa kwa uelewa wake ligi daraja la kwanza haina mikataba na mchezaji huwa huru mara ligi inapomalizika.Kwa msingi huo wanatambua kuwa ligi daraja la kwanza wachezaji wake wanakuwa na mikataba ,kama sivyo ni sababu zipi zilizowapelekea wao kudai kutuandikia barua sisi ya kutaka ufafanuzi wa mikataba ya wachezaji wetu na zaidi kwenda TFF?
 Klabu ya KIMONDO inahoji juu ya utaratibu huu,ni kwa namna gani mkataba uishe mara tu ligi inapokwisha? Na ni nini maana ya matumizi ya TMS kwa timu za VPL na FDL? Na ni kwanini katika utaratibu wa kutumia TMS kuna kipengele cha kuandika muda wa mkataba wa mchezaji na sio fixed time ya mwaka mmoja kama inavyodaiwa kwa timu za daraja la kwanza kama linavyozungumzwa na viongozi wa Yanga? Klabu ya KIMONDO inahoji ni kanuni ipi inayotumika/iliyotumika katika hili?
Kwa suala hili, Timu ya Kimondo isingependa kuona TFF ikipakwa matope kuwa ilishiriki kutoa go-ahead kwa timu ya Yanga kwa kigezo kuwa mchezaji wa ligi daraja la kwanza hawana mikataba, na usajiri wao huishia msimu unapomalizika. Tunaamini kuwa haya ni maelezo yaliyotolewa na uongozi wa Yanga kwa lengo la kutetea maslahi yao.
Kuhusiana na madai yanayotolewa na klabu ya YANGA kuwa klabu ya KIMONDO ilikuwa wapi tangu muda wote huo hadi kuja kuibuka na kudai kuwa mchezaji Geofrey Mwashiuya ni mali mara baada ya kung’ara katika mechi dhidi ya klabu ya Villa ya kutoka Uganda katika uwanja wa Taifa?
Klabu ya KIMONDO inaona hoja iliyotolewa na klabu ya YANGA ni dhaifu na haina mashiko kwakuwa klabu ya KIMONDO isingeweza kukurupuka pasi na ushahidi wowote kuwa klabu ya YANGA imemsajili mchezaji wetu zaidi ya hapo mwanzo kusikia tu kama tetesi katika vyombo vya habari. Kwa kutumia vyombo hivyohivyo vya habari klabu ya KIMONDO ilitoa angalizo dhidi ya timu zote zinazohitaji huduma ya mchezaji huyu zifuate utaratibu unaokubalika ka kuwasiliana na klabu yetu.
Katibu wa Yanga alienda mbali kwa kusema kwamba ,aliandika barua mwezi wanne kutaka kujua status za mchezaji Geofrey Mwashiuya na Mateo Danny Silavwe lakini hadi sasa hakupata majibu. Klabu inahoji kama alijua mchezaji mara ligi iishapo na mkataba unakwisha je alikuwa anaandika barua kutaka kujua endapo Geofrey ana mkataba na KIMONDO katika muktadha upi?na je hiyo barua alimwandikia  nani,na nani alipokea?Katika hili mnaweza kupima maelezo ya klabu ya YANGA dhidi yetu.
Uongozi wa KIMONDO unazidi kusisitiza kuwa mchezaji huyu ana mkataba nasi wa miaka minne na tunawashauri YANGA wafuate utaratibu unaotakiwa katika usajili na si vinginevyo.
Kama ni kweli walimsajili katika dirisha dogo mwezi Oktoba  basi kuna shida kubwa hapa,kwakuwa klabu ya KIMONDO ilimsajili mchezaji huyu mwezi wa nane tarehe 31,2014.Au kama ni kweli walimsajili mwezi wa pili,2015 ilhali KIMONDO ilimsajili mwezi wa nane tarehe 31 basi kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria za FIFA juu ya uhamisho/usajili wa wachezaji.Kwakuwa sheria zinasema mchezaji ataruhusiwa kufanya mazungumzo na klabu yoyote akiwa amebakiza miezi sita ya kumalizika kwa mkataba wake. Kwa mtizamo wao kuwa mchezaji wa FDL husajiliwa kwa mkataba wa mwaka mmoja mmoja.Izingatiwe kwamba kundi A ambalo klabu ya KIMONDO ilikuwepo mchezo namba moja ulikuwa dhidi ya KIMONDO  na VILLA SQUAD ulichezwa tarehe 11/10/2014 katika uwanja wa CCM –VWAWA MBEYA,mchezaji huyo alicheza akiwa amevalia jezi namba 22. Zaidi alicheza michezo yote mfululizo ya raundi ya kwanza hadi tarehe 20/11/2014.
Swali la kujiuliza,kama kweli mchezaji huyu alikuwa anaishi jangwani kuanzia mwezi Oktoba ,alikuwa anatokea Jangwani kwenda kucheza mechi za KIMONDO au alikuwa anacheza kwa mkopo?Tulitafakari hili kwa pamoja.Juu ya hili kumbukumbu zilizopo katika klabu yetu,Bodi ya Ligi na TFF zinaonyesha mchezaji huyu amecheza mchezo namba 129 wa tarehe 13/02/2015 kati ya KIMONDO dhidi ya MAJIMAJI FC ya Songea akiwa amevalia jezi namba 22.
Pamoja na hilo mchezaji huyu mwezi wa tatu mwaka huu amecheza katika ligi ya MSYETE CUP akichezea timu ya ISANSA BOYS FC  wakicheza na MPITO FC. Mwezi wan ne mwaka huu alikuwa akishiriki katika ligi ya JABU CUP hapo MPEMBA Katika viwanja vya Shule Ya Msingi Katete akiwa na timu ya NANSERE BOYS  FC ya Mpemba dhidi ya CHAPWA FC.
Kama hiyo haitoshi ameshiriki katika ligi ya KIMONDO CUP 13/05/2015 ,Pia tarehe 17/05/2015 amecheza katika ligi ya ZAMBI CUP katika fainali akiwa na ICHENJEZYA FC dhidi ya VWAWA SMALL BOYS. Kama hiyo haitoshi tarehe 24/05/2015 amecheza ligi ya DIWANI CUP  kata ya Halungu katika nusu fainali akichezea timu ya WASA FC  dhidi ya LWATI FC.
Tunajiuliza kwa michezo yote hiyo hiyo katika tarehe mbalimbali za michezo tajwa hapo juu je yote alikuwa anatokea jangwani? Na kama hakuwa anatokea jangwani kipindi chote hicho hawa Yanga wanajua alikuwa anakula,anavaa nini kama walivyodai katika hoja zao.
Katika mkataba wetu na mchezaji kipengele cha nne sehemu c kinachosema;
Katika kipindi chote cha mkataba mchezaji anaweza kufanya majaribio kwa makubaliano ya kimaandishi kutoka kwa klabu ,hivyo basi mchezaji amekiuka kipengele cha nne sehemu c.
Zaidi tunaamini klabu ya YANGA kwa makusudi imevunja kanuni hii ambayo ambayo inasema mchezaji hataruhusiwa kufanya majaribio bila kuwa na kibali au makubaliano ya kimaandishi na klabu yenye mkataba na mchezaji. Kama ambavyo wao YANGA hawakuafikiana na utaratibu uliofanywa na mchezaji wao SIMON MSUVA kwenda kufanya majaribio nchini Afrika ya Kusini ya bila kuwa na kibali kutoka kwao.
Tunapenda kuujulisha umma kuwa KIMONDO ndio klabu ya kwanza kumudu kusajili kwa wakati kwa kutumia mfumo wa TMS. Kwa mujibu wa barua ya pongezi tuliyoandikiwa na TFF ilisema kwamba endapo muda wa tarehe ya mwisho ya ufungaji wa dirisha la usajili usingeongezwa basi ni klabu moja tu ndio ingekuwa imekamilisha usajili kwa wakati nayo ni sisis KIMONDO SUPER SPORTS CLUB. Na pia hili lieleweke wazi kwamba usajili wa 2014/2015 hakukuwa na ujazaji wa fomu ya aina yoyote kwa timu zote za FDL na VPL kama ilivyodaiwa na mchezaji akichagizwa na uongozi alioandamana nao kwenda TFF na katika vyombo vya habari. Kwa nyongeza vitu vilivyotakiwa kuambatanishwa katika usajili ni vivuli vya mkataba,cheti cha kuzaliwa, na cheti cha daktari.Zaidi tumeelekezwa kuwa mfumo huu ndio utatumika tena kwa msimu wa 2015/2016 kuanzia tarehe       15/June hadi August/2015
Tunapenda kuufahamisha umma wa watanzania kuwa usajili wa dirisha dogo ulikuwa November hadi December 2015 na si kama ulivyoelezwa na uongozi wa Yanga kuwa walimsajili katika dirisha dogo la ,mwezi Oktoba.
Zaidi tunaamini Geofrey Bahati Mwashiuya ni mchezaji halali wa KIMONDO na atatumika kwa kipindi cha mkataba kama hakuna klabu itakayokuwa na uhitaji wa huduma yake kwa kufuata taratibu ,kanuni na sheria za usajili. Kama hakutakuwa na sababu nyingine yeyote ya kuvunja mkataba kwa pande zote mbili.
ASANTENI SAANA KWA KUNISIKILIZA

                                                            Imesainiwa na
Elick Ambakisye (0755-708828)
MKURUGENZI
Kimondo Super Sports Club