Adverts

Jul 22, 2016

Polisi Songwe yaja na Ligi ya vijana msimu wa mavuno


Jeshi la Polisi kwa kushirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo wilayani Mbozi katika mkoa wa Songwe  wanakusudia kuanzisha ligi ya vijana itakayoanza kulindima mwezi August, 2016

Akizungumza na mtandao huu, Mkuu wa polisi wilaya ya Mbozi Henry Kyssima amesema hatua hiyo inalenga kubaini vipaji vya vijana na hatimaye kutumia ligi hizo kuwaunganisha na timu mbalimbali zinazoanza ligi hivi karibuni

Ligi zinazokusudiwa kuwavizia wachezaji hao ni pamoja na zile za ligi kuu, daraja la kwanza na daraja la pili ambazo tayari kufuatia mwaliko huo kuna ugeni mkubwa ambao umeanza kuvinjali katika wilaya ya Mbozi na vitongoji vyake kwaajili ya kusaka vipaji hivyo

Kyssima amesema anatambua kuwa kipindi cha August kuna shughuli nyingi za kiuchumi zinazoendelea wilayani hivyo katika kuendesha ligi hiyo, itasaidia pia kutumia muda wa mapumziko katika michezo badala ya kuelekeza fedha na mapato yao kwenye matumizi ya dawa za kulevya na uhalifu

Amesema ligi hiyo itaendeshwa kwenye kanda tano na baadaye washindi wa kanda watakutanishwa hadi kupatikana kwa mshindi wa wilaya.