Adverts

May 3, 2009

HONGERA DOROTH MWANYIKA, MBOZI WANAKUKUMBUKA KWA KUSIMAMIA VYEMA TANZA KESHO

Rais aliwaapisha pia Makatibu tawala wa mkoa wa Mwanza Bi.Doroth Mwanyika na katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bwana Yusuf Athumani Matumbo. Bi Mwanyika anakumbukwa vyema na wananchi wa wilaya ya Mbozi kwa jinsi alivyoweza kusimamia mradi wa TANZA KESHO-ama CAPACITY 21 uliokuwa ukitekelezwa na halmashauri ya wilaya ya Mbozi kwa ushirikiano na UNDP. Utendaji wake unatajwa kuwa ndiyo mafanikio yaliyomwezesha kufanya kazi maeneo mbalimbali, ofisi ya katibu tawala mkoa wa mbeya, UNICEF na sasa huko kwenye ukatibu TAWALA. Picha kwa hisani ya Blog ya Mawasiliano Ikulu.