Adverts

Jul 22, 2016

MKUU WA WILAYA YA MBOZI AWATAKA MADIWANI KUWAFUATILIA WALENGWA WA TASAF



Mkuu wa wilaya ya Mbozi Bw. John Palingo amewataka madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi kufanya ufuatiliaji kwa walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini unaotekelezwa chini ya TASAF awamu ya tatu.

Akitoa salamu za serikali, Mkuu wa wilaya ya Mbozi amesema kuwa hatua hiyo itawarudisha kwenye mstari walengwa kutokana na kuwepo taarifa za matumizi mabaya ya fedha wanazonufaika kupitia mpango huo

Katika hatua hiyo amesisitiza kuwa hatua hiyo itasaidia kutekeleza azma ya mpango huo kufikiwa .

Katika hatua nyingine mkuu huyo wa wilaya ametangaza nia ya kurejesha na kuzifungua barabara za katikati ya mji wa Vwawa  na kwamba kitaitishwa kikao cha wadau wa maendeleo mji wa Vwawa ili kujadili jambo hilo mchana wa leo ama kesho asubuhi ili hatimaye kufikia maamuzi ya pamoja ya namna bora ya uendelezaji wa huduma ya usafiri na uchukuzi mjini.

Polisi Songwe yaja na Ligi ya vijana msimu wa mavuno


Jeshi la Polisi kwa kushirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo wilayani Mbozi katika mkoa wa Songwe  wanakusudia kuanzisha ligi ya vijana itakayoanza kulindima mwezi August, 2016

Akizungumza na mtandao huu, Mkuu wa polisi wilaya ya Mbozi Henry Kyssima amesema hatua hiyo inalenga kubaini vipaji vya vijana na hatimaye kutumia ligi hizo kuwaunganisha na timu mbalimbali zinazoanza ligi hivi karibuni

Ligi zinazokusudiwa kuwavizia wachezaji hao ni pamoja na zile za ligi kuu, daraja la kwanza na daraja la pili ambazo tayari kufuatia mwaliko huo kuna ugeni mkubwa ambao umeanza kuvinjali katika wilaya ya Mbozi na vitongoji vyake kwaajili ya kusaka vipaji hivyo

Kyssima amesema anatambua kuwa kipindi cha August kuna shughuli nyingi za kiuchumi zinazoendelea wilayani hivyo katika kuendesha ligi hiyo, itasaidia pia kutumia muda wa mapumziko katika michezo badala ya kuelekeza fedha na mapato yao kwenye matumizi ya dawa za kulevya na uhalifu

Amesema ligi hiyo itaendeshwa kwenye kanda tano na baadaye washindi wa kanda watakutanishwa hadi kupatikana kwa mshindi wa wilaya.

Jan 21, 2016

UTOAJI WA CHAKULA MASHULENI BADO CHANGAMOTO

Baraza la Madiwani wilaya ya Mbozi leo limeelezwa kuwa suala la utoaji wa chakula shuleni, bado limeendelea kukwaza mafanikio ya utendaji na ufaulu wa watoto kwenye shule za msingi.

Hayo yamejitokeza wakati wa kikao cha baraza la madiwani kupitia taarifa za kata ambapo imebainika kuwa shule nyingi ambazo hazikufanya vizuri kwenye matokeo ya darasa la saba ni zile ambazo hazina mpango wa chakula.

Shule ya Izyaniche ambayo mwaka juzi iliongoza kiwilaya katika miaka miwili mfululizo imekuwa ya mwisho kiwilaya na ni miongoni mwa shule 10 kimkoa za mwisho


Jan 8, 2016

SAMMATA AIPAISHA TANZANIA ,ANYAKUA TUZO

Hatimaye Mbwana Ally Sammatta ameiwakilisha vyema Tanzania baada ya kushinda miongoni mwa wachezaji wazawa wa Afrika kama mchezaji bora wa Mwaka anayechezea ligi za ndani ya Afrika
 Samatta anaungana na Mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang kutoka Gabon kuwa vinara wa CAF kama wachezaji bora wa mwaka 2015 kwa mara ya kwanza.

Samatta anakuwa mchezaji wa kwanza ukanda wa Afrika Mashariki kutwaa tuzo hiyo akiwa mchezaji bora anayeshiriki ligi za ndani barani Afrika

Mbwana Samatta amewafunika wenzake akiwemo mchezaji mwenzie wa Tp Mazembe  na kipa wa DRC CONGO Robert Muteba Kidiaba ambaye aliinuka na pointi 88, na kufuatiliwa na mchezaji kutoka Lgeria Baghdad Bouneydjah aliyepata pointi 63
 Wakati utamu huo ukimjia Samatta na taifa lake Tanzania, Majonzi yamehamia kwa wachezaji wakongwe akiwemo Yaya Toure kutoka Ivorycost na Ayew Andre wa Ghana ambao wamenyanyasika mbele ya mchezaji kinda wa miaka 26 Aubameyang aliyezoa pointi 143 zikiwa saba zaidi ya alizopata Toure huku Ayew akipata 112
 chanzo vanguard








Jan 6, 2016

MADIWANI MBOZI WAPIGWA DARASA MBOZI

Madiwani wapya wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi kwa mfululizo wa siku mbili wamehudhulia mafunzo ya kuwajengea uwezo katika kutekeleza majukumu yao.
 Miongoni wa taasisi zilizoshiriki kuwajengea uwezo ni pamoja na Ofisi ya kanda ya maadili ya utumishi wa Umma, Ofisi ya katibu tawala mkoa na wakuu wa idara za halmashauri ya wilaya.Eneo pekee lililozua maswali mengi ni suala la maadili ya utumishi wa umma, mahusiano baina ya serikali kuu na serikali za mitaa ambapo masuala ya mwingiliano wa kiutendaji na masuala ya ufuatiliaji maadili ya watumishi yalijadiliwa kwa upana.


Jan 5, 2016

REA WAPOKELEWA VIJIJINI KWA SAHANGWE LAKINI....

Wakazi wa kata ya Kigala wamepongeza hatua ya wakala wa Umeme vijijini REA kutekeleza mpango wa usambazaji wa umeme katika kijiji kimoja cha kata hiyo, hata hivyo wameonyesha hofu yao kutokana na mradi huo kuonyesha dalili za kuishia kijiji kimoja!Ingawa hakuna maelezo ya kitaalamu juu ya sababu za mradi huo kusimama licha ya kazi ya survey kufanywa hadi kijiji cha Kigala,ni kijiji cha Mlengu pekee ambacho mradi huo umeshatekelezwa na mkandarasi anaonekana kumalizia usambazaji kwenye kijiji hicho pekee.Hali hiyo imemsukuma mheshimiwa Diwani wa kata hiyo Nguvila kuanza kufuatilia ngazi za juu kutokana na kuelezwa kuwa mkandarasi wa mradi wa kupeleka umeme kijiji cha Kigala ni mwingine.Kwa ujumla jitihada za kuunganisha umeme vijiji vya kata ya Ikuwo na Kigala katika wilaya ya Makete zimepokelewa kwa mikono miwili na wananchi wa maeneo hayo na kupongeza jitihada za mbunge wao aliyemaliza muda wake Dr Binirith Mahenge ambaye aliasisi mchakato huo na kuusimamia. Wanaeleza kuwa matarajio yao ni kuona kuwa Mbunge wa sasa Mh Dr Norman Sigala anatoa msukumo zaidi katika kuhakikisha vijiji vilivyopangwa kutekelezewa mradi huo vinanufaika.Kwa mazingira ya vijiji hivyo kupata umeme wanaona ni sawa ya ndoto ya mchana kwakuwa tangu uhuru wamekuwa wakihangaika na miundombinu hasa barabara na hawakutegemea suala la umeme hivyo hatua ya sasa ni dalili ya ukombozi kiuchumi kwa wananchi hao na kwamba kutachangia uanzishaji wa viwanda vingi vijijini.








Msimu wa upandaji miti Mkoa wa Njombe waanza

Wakazi wa mkoa wa Njombe wameanza msimu mpya wa upandaji miti ambapo shughuli hizo sasa zimepewa umuhimu mkubwa tofauti na hapo nyuma ambapo programu mbalimbali za uhifadhi mazingira zilitekelezwa na kuhamasisha wananchi bila mwitikio mzuri.
Katika vijiji vya Kigala, Mlengu, Ikuwo,Matenga na Nkondo,wananchi wamejiwekezea akiba zao kwenye upandaji miti ambapo sasa angalau kila kaya ina angalau ekari moja ya miti hali inayoashiria kuwa miaka michache ijayo kutakuwa na mabadiliko makubwa.
Tishio lililopo kwa sasa ni kuwepo kwa taarifa kuwa Pori la akiba la Mpanga -Kipengere linakusudiwa kupanuliwa hivyo kuvifuta baadhi ya vijiji, hali hii inapunguza ari ya wananchi kupanda miti kwa kasi katika maeneo yao licha ya kupokea vyema mpango wa upandaji miti.Mzee Mafundihano Nzilani pichani anaeleza kuwa amejijengea utamaduni wa kupanda miche 100 kila mwaka na kwamba tayari keshaanza kufaidi matunda ya miti aliyoipanda miaka 15 iliyopita.






TUMERUDI TDNA

Mtandao wa indaba africa umerejea tena baada ya kuwa nje ya mawasiliano na jamii kwa muda mrefu. Hii ilitokana na mwendeshaji kukabiliwa na majukumu yaliyomfanya ashindwe kuusimamia.kwa sasa wasomaji wataendelea kupata habari humu