Adverts

Jan 21, 2016

UTOAJI WA CHAKULA MASHULENI BADO CHANGAMOTO

Baraza la Madiwani wilaya ya Mbozi leo limeelezwa kuwa suala la utoaji wa chakula shuleni, bado limeendelea kukwaza mafanikio ya utendaji na ufaulu wa watoto kwenye shule za msingi.

Hayo yamejitokeza wakati wa kikao cha baraza la madiwani kupitia taarifa za kata ambapo imebainika kuwa shule nyingi ambazo hazikufanya vizuri kwenye matokeo ya darasa la saba ni zile ambazo hazina mpango wa chakula.

Shule ya Izyaniche ambayo mwaka juzi iliongoza kiwilaya katika miaka miwili mfululizo imekuwa ya mwisho kiwilaya na ni miongoni mwa shule 10 kimkoa za mwisho