Adverts

Jan 6, 2016

MADIWANI MBOZI WAPIGWA DARASA MBOZI

Madiwani wapya wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi kwa mfululizo wa siku mbili wamehudhulia mafunzo ya kuwajengea uwezo katika kutekeleza majukumu yao.
 Miongoni wa taasisi zilizoshiriki kuwajengea uwezo ni pamoja na Ofisi ya kanda ya maadili ya utumishi wa Umma, Ofisi ya katibu tawala mkoa na wakuu wa idara za halmashauri ya wilaya.Eneo pekee lililozua maswali mengi ni suala la maadili ya utumishi wa umma, mahusiano baina ya serikali kuu na serikali za mitaa ambapo masuala ya mwingiliano wa kiutendaji na masuala ya ufuatiliaji maadili ya watumishi yalijadiliwa kwa upana.