Adverts

May 28, 2011

BREACKING NEWS: BASI LA SUMRY KUTOKA ARUSHA-MBEYA LAPINDUKA NA KUSABABISHA VIFO VINGI!

Zaidi ya watu 12 wanahofiwa kupoteza maisha baada ya basi la Sumry High Class linalotoka Arusha kwenda Mbeya kupinduka eneo la Igawa.
Taarifa zilizoufikia mtandao wa www.dtwevetz.blogspot.com zinaeleza kuwa basi hilo limepinduka majira ya saa nne usiku likitokea Arusha ambapo limekatika kuanzia kwenye  vioo na cabin yote ya juu imetoweka.
Mmoja wa walioshuhudia ajali hiyo  Frank Tweve ambaye alikuwa safari kutoka Dar Es Salaam akiendesha gari jingine amesema, akipita hapo majira ya saa nane usiku wa kuamkia leo  ameshuhudia Maiti 7 za wanaume, 2 za watoto na 4 za wanawake na inaelezwa kuwa maiti zingingine tayari zilikuwa zimeondolewa eneo la ajali na maiti nyingine zikiwa zimebanwa na vyuma kwenye basi hilo..
Gari hilo kulingana na maelezo hayo liliburuzika kwa umbali mrefu. na Taarifa zaidi mtaendelewa kuletewa na blog hii, endelea kuwa na indaba africa.
Tayari  mtandao umetuma kamera ya matukio katika eneo la ajali na mtaanza kuzipata picha asubuhi hii kadiri tunavyounganishwa na mpiga picha aliyeko eneo la ajali.