Adverts

May 15, 2011

BONANZA JINGINE KATI YA MZUMBE NA HALMASHAURI YA MBOZI LAFANA

Mkuu wa chuo cha Mzumbe Tawi la Mbeya akibadilishana mawazo na kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi aliyevaa nyekundu kwenye mchezo wa Bonanza la wazee uliofanyika uwanja wa Magereza jana jioni


Timu ya Mzumbe ikiwa katika mapumziko baada ya kutoka nguvu sawa  na Mbozi kwa kufungana bao 1-1 katika kipindi cha kwanza, hata hivyo katika kipindi cha pili hali ilibadilika kwa Mbozi kuwaongezea kibano mzumbe na kuwachapa mbili moja


Timu ya Mbozi veteran ambayo iliibuka na ushindi wa bao 2-1 dhidi ya Mzumbe, michezo hiyo imepangwa kuendelea kwa kuhusisha pia timu za Tunduma kila week end katika viwanja vya Vwawa na Chapwa ambapo pia Mzumbe wamekubali kushiriki katika michezo hiyo.

Katika mchezo wa Volley Ball Mzumbe pia walifungwa seti 2 kwa 1 katika mchezo wa kirafiki kwenye bonanza hilo

Mchezaji wa MZUMBE akijaribu kunyanyua mpira kwaajili ya kupiga smash kwenye volley ball dhidi ya Timu ya Vwawa