Adverts

Jul 29, 2011

Taswira Mbalimbali Za Ziara Ya Kikazi Ya Rais Jakaya Kikwete Huko Mtwara




Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua ubanguaji unaofanywa na wakulima wadogo katika kijiji cha Kitama,Wilayani Tandahimba wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Mtwara.
Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la msingi katika ghala jipya za mazao wilayani Tandahimba.
Kaimu Mganga mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Dr.Zulkarnain Ikaji akimwonesha Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete gari la kubebea wagonjwa aina ya bajaj litakalotumika katika Zahanati ya Sengenya wilayani Nanyumbu jana
Rais dr.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua korosho iliyosindikwa kwa mashine katika kiwanda cha Rift Valey Foods, wilayani Tandahimba.
Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua chanzo cha Maji ya mradi wa Makonde Water Supply katika bonde la Kitangari wilayani, Newala, mkoani Mtwara wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Mtwara.
Rais Dr.Jakaya Mrisho kikwete na kaimu mganga mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Dr.Zulkarnain Ikaji wakifunua kitambaa katika jiwe la msingi kuashiria kuzindua rasmi Zahanati ya Sengenya, iliyopo wilayani Nanyumbu, mkoani Mtwara Jana.Picha na Freddy Maro-IKULU

"