Adverts

Aug 24, 2011

Waasi wayateka makazi ya Gaddafi mjini Tripoli

Victory in sight: Rebel fighters celebrate near a partially obscured golf buggy belonging to Gaddafi inside the leader's compoundWalibya wakishangilia kutekwa kwa makazi ya Gadhafi, Tripoli
Madarzeni ya makombora aina ya Grad yamevurumishwa mjini Tripoli mapema leo. Waasi wameyateka makazi ya kanali Gaddafi.
Mtu mmoja aliyeshuhudia ameiambia televisheni ya al-Arabiya kwamba barabara ya Al-Sour, karibu na makaazi ya Bab al-Aziziya ya kiongozi wa Libya kanali Muammar Gaddafi, inashambuliwa kwa makombora.
Waasi wameyateka makazi ya Gaddafi na kupandisha bendera yao, lakini hawamkumpata kiongozi huyo wala wanawe. Kumekuwa na shangwe na nderemo katika kiwanja cha Kijani na barabara za mji mkuu Tripoli. Wafuasi wa Gaddafi wangali wanaendeleza upinzani katika baadhi ya sehemu za mji huo, na wanaidhibiti hoteli ya Rixos, makao makuu ya waandishi wa habari wa nchi za kigeni, na wanawazuia wasitoke.
Gaddafi aapa kuichoma Libya
Kufikia sasa Gaddafi hajulikani aliko, lakini amesema katika hotuba iliyotangazwa na redio moja ya Tripoli, na kuripotiwa na televisheni ya Al-Orouba, kwamba kuondoka kwake kutoka makazi yake ni mbinu ya kivita. Gaddafi pia ameapa kufa kama shahidi au apate ushindi dhidi ya jumuiya ya kujihami ya NATO.
Mtu mmoja aliyeshuhudia ameiambia televisheni ya al-Arabiya kwamba barabara ya Al-Sour, karibu na makaazi ya Bab al-Aziziya ya kiongozi wa Libya kanali Muammar Gaddafi, inashambuliwa kwa makombora.
Waasi wameyateka makazi ya Gaddafi na kupandisha bendera yao, lakini hawamkumpata kiongozi huyo wala wanawe. Kumekuwa na shangwe na nderemo katika kiwanja cha Kijani na barabara za mji mkuu Tripoli. Wafuasi wa Gaddafi wangali wanaendeleza upinzani katika baadhi ya sehemu za mji huo, na wanaidhibiti hoteli ya Rixos, makao makuu ya waandishi wa habari wa nchi za kigeni, na wanawazuia wasitoke.
Gaddafi aapa kuichoma Libya
Kufikia sasa Gaddafi hajulikani aliko, lakini amesema katika hotuba iliyotangazwa na redio moja ya Tripoli, na kuripotiwa na televisheni ya Al-Orouba, kwamba kuondoka kwake kutoka makazi yake ni mbinu ya kivita. Gaddafi pia ameapa kufa kama shahidi au apate ushindi dhidi ya jumuiya ya kujihami ya NATO.
Fedha zilizowekwa na utawala wa Gaddafi katika nchi za kigeni, zilizuiliwa na Umoja wa Ulaya, Marekani na mataifa mengine ya magharibi, kufuatia hatua ya kiongozi huyo kukandamiza upinzani dhidi ya utawala wake. Bi Ashton amesema Libya ina uwezo wa kuimarisha uchumi wake kwa haraka na hatarajii kutolewa msaada wa kiuchumi kwa ajili ya nchi hiyo.
Ashton amesema wanataka uhuru na demokrasia katika maisha ya kila siku ya Walibya. Amependekeza mkutano mwingine Ijumaa wiki hii mjini New York wa kundi la Cairo kwa ajili ya Libya, mkutano unaowaleta pamoja viongozi wa Umoja wa Ulaya, Umoja wa Afrika na jumuiya ya nchi za Kiarabu. Umoja wa Ulaya utakuwa na jukumu muhimu katika kibarua kigumu cha kukusanya silaha zilizotapaa mjini Tripoli.
Waziri wa mashauri ya kigeni wa Uturuki, Ahmet Davutoglu, amesema jumuiya ya kujihami ya NATO itaendelea na harakati yake ya kijeshi nchini Libya mpaka usalama utakapoimarika kikamilifu.
Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari huko Benghazi, akiwa ameandamana na mwenyekiti wa baraza la kitaifa la mpito, Abdel Jalil, waziri Davutoglu alisema mali za Libya zinazozuiliwa zinapaswa kuachiwa kabla kumalizika kwa mwezi wa Ramadhani kwa manufaa ya Walibya.
Aliongeza kusema kuwa Walibya wanahitaji fedha kwa dharura kwa ajili ya kuijenga Libya huru na yenye demokrasia. Davutoglu alisisitiza umuhimu wa kuulinda umoja wa Libya na mipaka yake, na kuiahidi Libya msaada kamili wa umma wa Uturuki.
Wafadhili wakutana Doha
Mawaziri wa kigeni wa nchi za kiarabu wamewataka Walibya wajiepushe na kulipiza kisasi kwa ajili ya kuijenga Libya mpya. Mawaziri kutoka Qatar, Saudi Arabia na Misri waliokutana mjini Doha kwenye kikao cha kamati ya amani cha jumuiya ya nchi za kiarabu, pia wamelitaka baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kwa haraka kuachia dola bilioni 2.5 mali za Libya zinazozuiliwa, kulipa mishahara na kugharamia misaada ya kiutu nchini Libya.
Mawaziri hao wamependekeza kulialika baraza la kitaifa la waasi kwenye mkutano wa mawaziri wa kigeni wa jumuiya ya nchi za kiarabu utakaofanyika Jumamosi ijayo, kujadili matukio katika ulimwengu wa kiarabu, ikiwemo Libya na Syria.
Qatar leo itandaa mkutano wa mataifa fadhili kuliwezesha baraza la kitaifa la mpito kupata dola bilioni 2.4 ili kuliwezesha kulipa mishahara ya Walibya kabla siku kuu ya Eid na kugharamia matibabu na miguu bandia inayohitajika na watu waliojeruhiwa.
Mwandishi: Josephat Charo/RTRE/AFPE/DPAE