Adverts

Nov 29, 2011

SOKO LA KISIMANI MJI MDOGO WA TUNDUMA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO.

Soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma
Mkuu wa wilaya ya Mbozi Gabriel Kimolo akiwa eneo la Tukio

Soko la Mji wa Tunduma wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya limeteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo. Chanzo hakijaweza kubainishwa lakini inadaiwa kuwa Umeme uliporudi baada ya kukatika ndipo moto ulipoanza katikati ya Soko hilo
Vibanda vilivyokuwa vimejengwa kwa mbao vimeteketea na kubakia masalia ya mabati yaliyotumika kuezekea vibanda hivyo katika Soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya, jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo.
Kijana mmoja aliyevalia mwenye fulana ya Bluu akiwa amekamatwa wakati akijaribu kutorosha baadhi ya mali zilizokolewa katika moja ya maduka yaliyoteketea kwa moto katika soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya , jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo.
Baadhi ya wafanyabiashara wakiwa wamebeba mizigo ya mali zao mara baada ya kufanikiwa kuokoa mali zao katika Soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya lililoteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo.
Baadhi ya wafanyabiashara wakipakia mizigo ya mali zao katika gari mara baada ya kufanikiwa kuokoa mali zao katika Soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya lililoteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo.
Askali wa kampuni ya Ulinzi akitizama mali iliyookolewa katika moja ya maduka ambapo wananchi waligombania mali hizo na kuzichukua wakati Soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya likiendelea kuteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo.
Mbao zilizokuwa zimetumika kujengea vibanda vya biashara zikiwa zimevunjwa ikiwa ni moja ya njia ya kudhibiti moto kutoendelea kuteketeza vibanda, maduka na mali za wafanyabiashara katika soko la soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya lililoteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo.
Pichani ni duka ni moja wapo ambalo halikuweza kuteketea kwa moto, ambapo ukitazama juu ya paa Paka aliyekuwa na rangi Nyeusi hakuweza kutoweka hapo, licha wa moto kuendelea kuteketeza maduka na vibanda vya biashara katika soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya lililoteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo.
Magari ya kampuni ya Ujenzi wa barabara ya Tunduma mpaka Sumbawanga yalifika kutoa msaada wa kudibiti moto katika Soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya lililoteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo.
Gari la zimamoto likiwasili eneo la tukio kudhibiti moto kutoendelea kuteketeza maduka, vibanda vya biashara na bidhaa katika soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya lililoteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo.

Mzee huyu alishikwa na bumbuwazi la kutoamini duka lake likiteketea kwa moto ambapo hivi karibuni aliingiza mzigo wa bidhaa kutoka jijini Dar es salaam uliogharimu shilingi milioni Ishirini.
Na Ezekiel Kamanga
Moto mkubwa umeteketeza kabisa soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma wilaya mpya ya Momba mkoani Mbeya, jana na kusababisha hasara kubwa ya mali kuteketea na baadhi ya watu kujeruhiwa.

Zaidi ya wafanyabiashara elfu moja wameathiriwa kiuchumi kutokana na moto huo ulioanza majira ya saa 10 jioni mara umeme ulipo rudi baada ya kukatika na hivyo kusababisha moto kuzuka katikati ya vibanda ndani ya soko.

Juhudi za kuuzima moto huo zilichukua muda kutokana na mji huo wa kibiashara kukosa gari la zima moto, hali iliyolazimu magari ya maji(boza) yanayotumika kujenga barabara kutoka Mji wa Tunduma kwenda mkoani Rukwa kusaidia kudhibiti moto huo na kusaidiwa na magari mawili ya zima moto kutoka wilaya ya Nakonde ya nchini Zambia ambapo nayo yalishindwa kuzima moto huo.

Hata hivyo magari mawili kutoka jijini Mbeya yalifika eneo la tukio majira ya saa moja na robo usiku ili kudhibiti moto huo.

Uhaba wa maji katika mji huo umechangia kwa kiasi kikubwa kukwamisha shughuli za uzimaji moto huo kwani magari kutoka nchini Zambia yaliishiwa maji mapema.

Mkuu wa wilaya ya Mbozi Bwana Gilbert Kimolo alifika mapema kutoa pole kwa wahanga na kuwaomba kuwa watulivu kutokana na janga kubwa lililowakuta na kwamba serikali inafanya uchunguzi ili kuweza kubaini chanzo hicho cha moto.