Adverts

Apr 21, 2013

ISSUE YA UKIMWI-MADIWANI MBOZI WAPIGWA SHULE

 Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi wakisikiliza kwa makini wakti wakipata maelezo ya mchakato wa kuongeza hamasa ya kwa wananchi juu ya tohara, kwa ujumla mwitikio umekuwa mkubwa tangu operesheni ondoa mkono wa sweta iliyoanza mwezi huu kupitia hospitali ya wilaya ya Mbozi ambapo wastani wa watu 600 hujitokeza kila siku kunyofoa mikono ya sweta hata hivyo uwezo kwa siku ni watu 70tu!
 Mh Makunganya akiwa anafuatilia mijadala
 Mwenyekiti wa kamati ya Kudhibiti UKIMWI wilaya Mbozi CMAC mh Mgula akisoma kimemo "bila shaka kutoka kwa mmoja wa madiwani aliyetaka kujua vipande vya mikono ya sweta vinapelekwa wapi? kila anayefanyiwa suna angekuwa anapewa kipande chake akakifukie mwenyewe nyumbani!!!

 Mwezeshaji na mnasihi katika hospitali ya wilaya ya Mbozi Bi Fumbo akifafanua jambo ambapo alieleza kuwa asilimia 80 ya wanawake wanabakwa licha ya kupata watoto kwenye kaya zao hawajawahi fika mshindo katika tendo la ndoa kutokana na akina baba kuwafakamia bila kuwaandaaa





Halmashauri ya wilaya ya MBOZI kupitia kitengo cha kudhibiti UKIMWI imeendesha warsha ya siku moja kwa wenyeviti wa kamati za kudhibiti UKIMWI za kata pamoja na mambo mengine kuzungumzia kampeni ya tohara kwa wanaume inayoendelea kutekelezwa kupitia hospitali ya wilaya ya Mbozi

Akizungumza kwenye warsha hiyo mratibu wa Kudhibiti UKIMWI wilaya  Bwana Oscar Mgani alieleza kuwa katika kipindi kirefu wanachi wamekuwa wakihamasishwa kutoa mikono ya sweta, na sasa mwitikio umepanuka hadi kwa watoto wadogo 

Katika hali ya kuonyesha watu wanakumbwa na aibu kwa kuendelea kuwa na mkono wa sweta baadhi ya wazee wenye  umri mkubwa wamekuwa wakiongozana na watoto hadi hosipitalini wakidai wanawapeleka vijana wao kutahiri lakini wakishafika ndani  kwenye eneo la upasuaji mdogo wao wenyewe ndiyo wanaanza kuvua suruali ili wapate huduma!

katika mijadala mbalimbali iliyoendeshwa katika warsha hiyo miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa ni umuhimu wa kuhamamasisha wananchi wanaoishi na vvu kujiunga na vikundi vya waVIU vijijini ili waweze kunufaika na fulsa zinazotolewa na serikali za mitaa pamoja na program za UKIMWI wilayani.