Na Kenny Katombe na Chrispin Mvano
KINSHASA (Reuters) – Mmoja wa walinzi wa Umoja wa Mataifa
kutoka nchini Tanzania  aliuawa na
mwingine kujeruhiwa wakati wa siku ya tatu ya mapigano kati ya vikosi vya
serikali na waasi katika mashariki ya Kongo siku ya Jumapili, wakati wakielekea
kwenye  ngome ya waasi wa Rutshuru .
Mkuu wa  vikosi vya Umoja
wa Mataifa nchini Kongo ( MONUSCO ) alisema mlinda amani kutoka Tanzania
aliuawa wakati wa kupambana na waasi wa M23 katika mji wa Kiwanja, kaskazini ya
mji mkuu wa mkoa Goma , mji mkubwa mashariki mwa Kongo.
"Askari alikufa wakati wa kulinda watu wa Kiwanja,
" Martin Kobler , mkuu wa MONUSCO, alisema katika taarifa. Katika awamu ya
kwanza  ya mapigano kati ya jeshi na
waasi mwishoni mwa Agosti , waasai hao waliwauawa  askari wawili wa kulinda amani wa Tanzania.
Kufuatia miezi miwili ya utulivu  katika ukanda  wa mapigano, mapigano yamelipuka ghafla Ijumaa
baada ya mazungumzo ya amani nchini Uganda kuvunjika baada ya  M23 kutaka viongozi wake wapewe msamaha kamili
. Kila upande umekuwa ukilaumiwa na mwingine kuhusika na kuanzisha  mapigano.
Rais Joseph Kabila, ambaye wiki iliyopita alitishia kurejea
kwenye  hatua za kijeshi , na kudai kuwa
msamaha pekee kwa VIONGOZI wa M23  bila  masharti si haikubaliki.
 

