Adverts

Nov 5, 2013

SAFARI YA KICHAPO CHA M23 KATIKA PICHA

 HAPA ilikuwa Sept 15 ambapo mpaka baina  ya Kongo na Rwanda ulifungwa baada ya kutuhumiana  na hiii inafuatia Rwanda kudai Kongo imeua raia wake kwa kupiga kombora wakati ambapo kongo ilidai ni waaasi wa M23 walifanya hivyo kuongeza chumvi kwenye vita hiyo ili Rwanda aikasirikie kongo
 Hapa kikosi ch jeshi la Kongo kikisonga mbele baada ya kuanza kukomboa maeneo muhimu ya ngome ya waasi wa M23
 Baada ya mziki kuzidi jana usiku, M 23 Waliamua kuanza kuteketeza baadhi ya zana zilizokuwa zikiwasaidia, hii inaitwa bora wote tukose! hasa inapoonekana kuwa huna matumaini tena ya kwenda mbele zzaidi ya kutafuta mahala pa kujificha!!!
 Hii ndiyo iliyokuwa kambi ya M 23 Makao makuu yao, lakini baada ya kuvurumishwa wakaamua kuiteketeza kabisa jana na leo kabla ya kutangaza kisanii ati wameacha vita ili wafanye mazungumzo ya amani!
 Mateka na vijana waliojisalimisha kutoka kikundi cha M 23
 Zana zilizoharibiwa na kundi la M 23 baada ya maji kuwafika shingoni, hapa ni moja ya makambi yao katka eneo la Chanzo ambako ndiko makao makuu ya M23
 Upepo ulivyosoma vibaya waliamua kutelekeza mashine kama hizi za kivita na kutimua mbio kusikojulikana
 Kwaheri ya kuonana kifaa chetu, siye tunakwenda " ndivyo zana hii inavyoonekana kuachwa
 Hapa ndipo jamaa wa M23 walipojihifadhi kwa siku tatu za hivi karibuni lakini baada ya chai ya kuanzia jana jioni, usiku na hatimaye asubuhi ya leo wametangaza wenyewe kutupa chini mikoba
Hapa ni kambi yao iliyoharibiwa baada ya kukumbana na wakati mgumu wa jana na leo usiku!

Kiongozi wao amekuja na maelezo haya kwa kifaransa nitayafafanua


nnonce de fin de rébellion
Annonce de fin de rébellion

La Direction du Mouvement du 23 Mars annonce à l'opinion nationale et internationale qu'elle a décidé à dater de ce jour de mettre un terme à sa rébellion et de poursuivre, par des moyens purement politiques, la recherche des solutions aux causes profondes qui ont présidé à sa création.

A cet effet, le Chef d'Etat-major Général ainsi que tous les commandants des grandes unités de l'Armée Révolutionnaire Congolaise sont priés de préparer les hommes des troupes au processus de désarmement, démobilisation et réinsertion sociale dont les modalités sont à convenir avec le Gouvernement de la République Démocratique du Congo.

Fait à Kampala, le 05 Novembre 2013

Le Président du Mouvement du 23 Mars

Bertrand BISIMWA

Kwa kiswahili cha haraka haraka ni kwamba 


Mwisho wa Uasi
Mwisho wa Uasi
Kurugenzi ya  Movement on March 23 ama kwa kifupi M23 inalitangazia taifa na jumuiya ya kimataifa kuwa kuanzia tarehe ya siku ya leo kusitisha uasi wake, na sasa mazungumzo ya kisiasa yatachukua nafasi katika kutafuta suluhu  na kutafuta chanzo kilichotuleteleza kwenye hali hii ya mapigano

Kwa mwisho huu Amiri jeshi Mkuu na wakuu wa kamandi zake na vikosi  vyake (m23) wanatakiwa kuvunja vikosi  vyote, kuweka siraha chini  na kusitisha mapigano tena  ili kuunganisha nguvu na jamii ya watu wa kongo  wakati huu tuweze kutekeleza yale tuliyokubaliana na serikali ya jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo


Limetolewa hapa Kampala ,November 5, 2013

Rais wa Movement of March 23

Bertrand Bisimwa