Adverts

Nov 3, 2013

WAZAZI WAPONGEZA NECTA KUWAHI NA KUTOA MATOKEO SAHIHI

Baada ya NECTA kutoa matokeo ya darasa la saba haraka na kwakupitia wavuti yao, wazazi wamepokea matokeo hayo kwa mtazamo chanya huku wakisifu maboresho yaliyofanywa na NECTA
Kwa nyakati tofauti wazazi wanasema, NECTA imeondosha malalamiko ya muda mrefu juu ya mfumo wa usahihishaji ambao ulikuwa unalalamikiwa hasa kwa watu wenye mwandiko usio mzuri

Wanasema kupitia usahihishaji wa sasa Optical Mark Leader, unaonyesha kuwa  umeleta ufanisi na kuwahi kutoa matokeo kwa muda mfupi.