Adverts

Sep 26, 2010

UCHAGUZI MKUU RIDHIWAN KIKWETE ATIA TIMU MBOZI

Mtoto wa mgombea urais kwa tiketi ya chama cha mapinduzi RIDHIWAN KIKWETE jana alipokelewa kwa mbwembwe na wanachama wa chama cha mapinduzi Mbozi akitokea wilayani Ileje. Ridhiwan ambaye ni Mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya umoja wa vijana Taifa pia akiwa mwenyekiti wa Miradi ya umoja wa Vijana wa CCM aliwasili katika ofisi za chama za wilaya Mbozi majira ya saa 11.20 Jioni. Inaelezwa kuwa pamoja na kuzungumzia masuala mbalimbali ya kuimarisha jumuiya za chama na nafasi ya vijana katika kuimarisha chama pia aliomba wanchama wa ccm kuimarisha harakati za kujenga mafiga matatu katika uchaguzi mkuu wa 2010. Hata hivyo wachunguzi wa mambo wametaja kuwa jitihada za Ridhiwan kutembelea wilaya ni katika kujiimarisha na mchakato wa kuandaa mazingira ya kugombea kupitia vijana kwenye ujumbe wa NEC hivyo kujipa nafasi ya kufahamika kwa wapiga kura kabla ya kufikia kwenye chekeche la uchaguzi.