Adverts

Jan 22, 2011

MAFUNZO YA KUTENGENEZA WEBSITE

Ni wengi wetu tumekuwa tukitamani kutengeneza tovuti,iwe ni kwa ajili ya kibiashara au kwa matumizi binafsi.Ingawa siku hizi suala la kutengeneza website limekuwa rahisi zaidi kutokana na kuwepo kwa programu nyingi ambazo zinamsaidia mtengenezaji kufanya hilo kwa haraka zaidi,ila ukweli unabaki palepale,kwanza ni lazima ujue jinsi ya kutengeneza tovuti ndipo ufaidi msaada wa hizi programu.
Kwa kulitambua hilo,timu nzima ya AfroIT inakuletea mafunzo ya kutengeneza website Live kila Jumanne na Jumamosi saa kumi kamili ya Tanzania.Kwenye mafundisho hayo ya hatua kwa hatua ,kama upo darasani vile.Unapata wasaa wa kuuliza na kuchangia.

Mtoa mada: Mkata Nyoni(hatua ya kwanza)

Muda: Kila jumanne na Alhamisi,saa kumi jioni,1600hrs(kwa saa za afrika ya mashariki)

Link: Hapa

Idadi ya wanafuunzi:10

Level: Kwa wanaojua kutumia browser na internet kwa uchache wake

Ufafanuzi:Tembelea Hapa

Utaratibu wa mafundisho

Tutaanza mwanzo kabisa,tutatumia mtindo wa project ili kuhakikisha inakuwa na maana zaidi,sio kusoma tu halafu huoni kinachotokea.

Kwenye mafundisho haya ya moja kwa moja(Live),tutakuwa wote katika kutengeneza AfroIT Movie Store.Utaweza kujionea na kujifunza hatua baada ya hatua mbapo hadi unamaliza mafundisho,basi utaweza kutengeneza website yako ya kawaida.

Baada ya hapo,utajiunga na mkufunzi mwingine ambaye ataiendeleza AfroIT Movie Store kwa kuweka manjonjo na mididi zaidi(Advanced).

Katika hatua ya Mwisho(tatu) ndipo mutajiunga na wataalam ambao wataichukua website ya hatua ya pili na kuifanya kuwa dynamic ambapo kutakuwa na makundi mawili,moja ni wale wa PHP na lingine ni wale wa .NET.

Hadi mwisho wa safari,ni dhahiri utakuwa umewiva,tena bila gharama yoyote ya ziada.
Ukiwa na swali au utata,basi usisite kuwasiliana nasi kwa kutuandikia podcast@afroit.com au kutmbelea AfroIT Forums