Adverts

Jan 19, 2011

yale yaleeeeee....

yale yaleeeeee....: "
Arusha Airport

BARUA YA WAZI KWA MH. WAZIRI WA UJENZI

YAH: MATENGENEZO YA SEHEMU YA ABIRIA WANAOSAFIRI NA WANAOWASILI (ARRIVAL / DEPATURE LOUNGE)

Kichwa cha habari hapo juu chahusika.

Kuna habari zisizo rasmi kuwa mfanyabiasahra mwenye asili ya ki-asia anayeendesha bisahara ya mgahawa /restaurant katika kiwanja cha Arusha ndiye aliyepewa kazi ya kufanya matengenezo kuanzia mwezi march 2011 (jina tumelihifadhi).

Tumekuwa tukiona mkandarasi akiingia na kupima maduka ya wafanyakabisahara bila taarifa yeyote ya kimaandishi na hatujawahi kuona tangazo lolote linalohusu kufanyika matenegezo hayo, hivyo kuna uwezekano mkubwa kwamba taratibu za kumpata mzabuni hazikufuatwa.

Kwa maana hiyo kuna uwezekanao mkubwa wa mianya ya rushwa. Mfanyabishara huyo mwenye asili ya ki-asia anamiliki duka la Duty free kiwanja cha Julius nyerere pia kiwanja cha Kilimanjaro.

Sisi Wafanyabiashara tuna wasiwasi kwamba endapo ujenzi huo ambao hakufuata taratibu za gharama za juu sana za matengenezo hayo na kusababisha kodi za pango kuwa juu zaidi ya kawaida kwa wafanyabiahara na hivyo kuwafanya wafanyakabiashara washindwe kumudu gharama za pango maana ana tabia hiyo.

Tunapenda Kutoa Angalizo taratibu za zabuni zifuatwe na zabuni hiyo itangazwe kwenye vyombo vya habari(magazeti,mbao za matangazo n.k)

Tunaomba mamlaka husika zifuataitlie kwa umakini juu ya suala hili

WAFANYABIASHARA KIWANJA CHA NDEGE -ARUSHA

"