Adverts

Feb 17, 2011

Maafisa Mazingira wa Mikoa ya Nyanda za juu kusini wakutana kupigwa msasa mkoani ruvuma

Katibu Tawala wa Mkoa wa Songea Dk. A. H. Tarimo akifungua warsha kwa Maafisa Mazingira wa Mikoa ya Nyanda za juu kusini inayojumisha mikoa ya Iringa, Mbeya na Songea yenye lengo la kukuza uelewa wa mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabia Nchi, kulia kwake ni Dk. Costantine Shayo kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na Bw. Enock Bujah Mshauri wa Maliasili Mkoa wa Songea. Warsha hiyo inafanyika mkoani Ruvuma.
Baadhi ya washiriki wa warsha kwa Maafisa Mazingira wa Mikoa ya mikoa ya Iringa, Mbeya na Songea yenye lengo la kukuza uelewa wa mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabia Nchi. Warsha hiyo imeratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais na inafanyika Mkoani Ruvuma
Na Lulu Mussa Katika jitihada za kukuza weledi wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Idara ya Mazingira imefanya warsha kwa maafisa mazingira juu ya mikakati ya kuhimili mabadiliko ya Tabianchi. Akifungua warsha hiyo ya siku tatu, Katibu Tawala wa Mkoa wa Songea Dk. A.H. Tarimo amewataka wataalamu hao kusimamia vizuri sheria ya mazingira na kuwaasa watoe elimu kwa jamii juu ya hifadhi ya mazingira kuanzia ngazi ya kaya. Amesema katika kukabiliana na changamoto za mazingira Serikali imeendelea kutekeleza Sera, Sheria, Kanuni na mikakati inayolenga kuwa na matumizi endelevu ya rasilimali na maliasili kwa lengo la kufikia maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii. “Uharibifu wa mazingira ndio kiini cha kuenea kwa hali ya jangwa na ukame, kukauka kwa vyanzo vya maji, wingi wa mifugo unaozidi uwezo wa malisho, na migongano ya ardhi” alisisitiza Dk. Tarimo. Aidha, majadiliano kuhusu mpango wa muda mrefu wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi yalianza baada ya kuanzishwa kwa Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi mwaka 1992 na Mkataba mdogo wa Kyoto wa mwaka 1997 ambao Tanzania imeridhia. Warsha hii ya kukuza uelewa imeratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais na inafanyika Mkoani Ruvuma inahusisha Maafisa Mazingira kutoka mikoa ya Iringa, Mbeya na Songea.
"