Adverts

Feb 9, 2011

Walimu Kuajiriwa Moja Kwa Moja Bila Usaili

Walimu Kuajiriwa Moja Kwa Moja Bila Usaili: " SERIKALI imeamua kuwa kuanzia sasa walimu nchini, kama ilivyo kwa madaktari, wataajiriwa na kupangiwa moja kwa moja vituo vya kazi bila kufanya usaili ama kucheleweshwa na michakato na taratibu nyingine za kirasimu, ili mradi wawe wameshinda mitihani yao. Ili kutekeleza uamuzi huo wa Serikali, imeamuliwa kuwa walimu watapangiwa vituo vya kazi katika miezi ya mwisho ya mafunzo yao ili kuwawesha kuripoti moja kwa moja kwenye vituo vyao baada ya kumaliza masomo na mafunzo yao. Uamuzi huo wa Serikali ulifikiwa katika kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika wiki iliyopita, Alhamisi, Februari 3, 2011, mjini Dar es Salaam chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Baraza limefikia uamuzi huo kwa kutilia maanani uhaba wa walimu, kama walivyo madaktari nchini na, kwa nia ya kupanua na kuboresha kiwango cha huduma elimu. (Phillemon L. Luhanjo) KATIBU WA BARAZA LA MAWAZIRI 07 FEBRUARI, 2011
"