Adverts

Apr 1, 2011

*POROFESA SAFARI AIPA KISOGO CUF NA KUJIUNGA NA CHADEMA

*POROFESA SAFARI AIPA KISOGO CUF NA KUJIUNGA NA CHADEMA: "
Mwenyekiti wa Chama cha CHADEMA, Freeman Mbowe (kulia) akimkabidhi kadi ya chama hicho, Profesa Abdallah Safari, aliyekuwa mshauri wa Mwenyekiti wa CUF Ibrahim Lipumba, aliyejiunga na Chama hicho, wakati wa mkutano na waandishi wa habari wa kumtangaza rasmi uliofanyika kwenye Ofisi za Chadema Kinondoni leo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Willbroad Slaa. Show all Hide all Mbowe akisaini kadi hiyo ya Safari kabla ya kumkabidhi rasmi, wakati wa hafla hiyo.
Mbowe akizungumza na waandsihi wa habari wakati wa mkutano huo.
Hafla hiyo nusu iingiwe na dosari baada ya waandishi wa habari kufika katika ofisi za Chadema kwa muda muafaka walioambiwa na kukuta hakuna hakuna hata kiongozi mmoja aliyekuwa amewasili kwa ajili ya mkutano huo, hadi ilipoanza kunyesha mvua kubwa iliyofanya eneo hilo la mkutano kuvuja na kuwafanya waandishi wa habari kuhaha kusaka mahala pa kujisitili. Hapa ni mmoja kati ya wafanyakazi wa ofisi hiyo akijaribu kuyatililisha maji hayo yaliyokuwa yametuama juu ya banda lililokuwa maalum kwa ajili ya mkutano huo.
Mvua ikitawala mahala hapo na kufanya Jukwaa kuu la Mkutano huo kulowana kabla ya kuanza kwa mkutano.
"