Adverts

Nov 11, 2011

MKUU WA MKOA WA MBEYA AKATISHA ZIARA MBOZI KUJA KUKUTANA NA WAMACHINGA

Taarifa zilizotufikia hivi sasa ni kwamba Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro amekatisha ziara yake wilayani Mbozi na alikuwa njiani kurudi jijini Mbeya kukutana na wamachinga waliouteka mji tangu asubuhi. Kinachosubiriwa ni iwapo wamachinga hao watakubali kuongea naye kwani walishatamka kuwa hawataki kumuona. Muda huu machinga walikuwa wakilazimisha kuingia katikati ya jiji kushinikiza kuachiwa kwa wenzao wanaoshikiliwa na polisi