Adverts

Jan 2, 2012

Mkwere wa Mizengwe auga mwaka 2011 kwa kukimbia klabu ya makapera

Chereko, vifijo, shangwe, nderemo na vigelegele vilitawala kila kona ya ukumbi huku watu wakivunjika mbavu kwa vituko kwenye harusi ya komediani matata Bongo, Hemed Maliyaga ‘Mkwere’. Tukio hilo lilichukua nafasi kwenye Ukumbi wa Delux Hotel Sinza, Dar es Salaam, usiku wa Ijumaa baada ya Mkwere wa Kundi la Mizengwe, kufunga ndoa na Fatma Abdallah Massawa siku hiyo mchana Mabibo, Dar.
Picha kwa hisani ya Global Publishers.info.